Wamagoma

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Wamagoma ni kabila la watu wa Tanzania wanaoishi katika Mkoa wa Njombe, Wilaya ya Makete hasa maeneo kama vile [[Ubiluko, Ipelele na Kidope: hayo ni baadhi ya maeneo ambako Wamagoma wanapatikana kwa wingi.

Lugha yao ni Kimagoma.

Kabila hilo lina koo chache sana, kwa mfano koo zifuatazo zinapatikana katika kabila hilo: Fungo, Mbilinyi, Tweve na Mbogela.

Wamagoma wanajulikana sana kwa ufanyaji kazi kwa bidii na kwa kujituma hasa kazi za mashambani, pia ni kabila ambalo ni waaminifu na wana bidii katika utendaji kazi.

Makala hii kuhusu utamaduni wa Tanzania bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Wamagoma kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.