Wilaya ya Mbinga Vijijini

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Wilaya ya Mbinga)
Mahali pa Mbinga (kijani) katika mkoa wa Ruvuma.

Wilaya ya Mbinga ni wilaya moja ya Mkoa wa Ruvuma yenye postikodi namba 57400 .[1]. Katika sensa ya mwaka 2012, idadi ya wakazi wa wilaya hiyo ilihesabiwa kuwa 353,683 [2].

Wilaya hii imepakana na mkoa wa Iringa upande wa kaskazini, wilaya za Songea mjini na Songea vijijini upande wa mashariki, Msumbiji upande wa kusini na Ziwa Nyassa upande wa magharibi.

Sehemu kubwa ya eneo lake iko ndani ya milima inayoongozana na pwani la ziwa pamoja na mwambao wa ziwa. Wilaya imeona maendeleo kadhaa kutokana na barabara mpya na kilimo cha kahawa inayostawi vizuri katika hali ya hewa mlimani. Mwaka 2012 maeneo ya wilaya ya Mbingwa yalitengwa kuwa wilaya ya Nyasa.

Mji wa Mbinga ni makao makuu ya dayosisi ya Kikatoliki.

Mwaka 2015 mji wa Mbinga ulitengwa na wilaya hiyo na kuwa halmashauri ya pekee.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]

Living space Mbinga (tovuti ya kikatoliki) Archived 7 Februari 2017 at the Wayback Machine.

Flag of Tanzania.svg Kata za Wilaya ya Mbinga - Mkoa wa Ruvuma - Tanzania Flag of Tanzania.svg

Amani Makolo | Kambarage | Kigonsera | Kihangi Mahuka | Kipapa | Kipololo | Kitumbalomo | Kitura | Langiro | Linda | Litembo | Litumbandyosi | Lukurasi | Maguu | Mapera | Matiri | Mbuji | Mhongozi | Mikalanga | Mkako | Mpapa (Mbinga) | Muungano | Namswea | Ngima | Nyoni | Ruanda (Mbinga) | Ukata | Wukiro


Flag-map of Tanzania.svg Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Ruvuma bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Wilaya ya Mbinga Vijijini kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno.