Igawilo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru


Kata ya Igawilo
Kata ya Igawilo is located in Tanzania
Kata ya Igawilo
Kata ya Igawilo

Mahali pa Igawilo katika Tanzania

Majiranukta: 8°53′24″S 33°25′48″E / 8.89000°S 33.43000°E / -8.89000; 33.43000
Nchi Tanzania
Mkoa Mbeya
Wilaya Mbeya Mjini
Idadi ya wakazi
 - Wakazi kwa ujumla 25,004

Igawilo ni kata ya Mbeya Mjini katika Mkoa wa Mbeya, Tanzania. Iko jirani na Uyole kando ya barabara inayopanda Uporoto kuelekea Tukuyu na Malawi.

Katika sensa iliyofanyika mwaka 2022 wakazi walihesabika kuwa 25,004 [1]. Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 17,300 [2] walioishi humo.

Wakazi wengi wa sehemu hii ni wakulima wa mazao ya chakula pamoja na bustani. Kuna shule ya sekondari ijulikanayo kama Igawilo.

Baadhi ya mamwene au machifu wa Kisafwa walioishi katika eneo hili ni: Mwene Male Mwashinga na Mwene Paul Mwashinga.

Msimbo wa posta ni 53106.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. https://www.nbs.go.tz
  2. "Sensa ya 2012, Mbeya - Mbeya MC". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2004-01-02. Iliwekwa mnamo 2017-03-14. 
Kata za Jiji la Mbeya - Tanzania

ForestGhanaIdudaIganjoIganzoIgawiloIlemiIlombaIsangaIsyesyeItaganoItendeIteziItijiIwambiIyelaIyungaIziwaKalobeMaangaMabatiniMaendeleoMajengoMbalizi RoadMwakibeteMwasangaMwasenkwaNondeNsalagaNsohoNzovweRuandaSindeSisimbaTembelaUyole


Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Mbeya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Igawilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno.