Umoja wa Afrika : Tofauti kati ya masahihisho
Tags: Mobile edit Mobile web edit |
No edit summary |
||
Mstari 1: | Mstari 1: | ||
[[Picha:Flag African Union 02.svg|thumb|200px|Bendera ya Umoja wa Afrika]] |
[[Picha:Flag African Union 02.svg|thumb|200px|Bendera ya Umoja wa Afrika]] |
||
[[Picha:Map of the African Union.svg| |
[[Picha:Map of the African Union.svg|400px|thumbnail|right|Ramani ya Umoja wa Afrika. Nchi zote za Afrika ni wanachama (baada ya [[Moroko]] kujiunga upya tarehe [[30 Januari]] [[2017]]).]] |
||
'''Umoja wa Afrika (UA)''' (kwa [[Kiingereza]]: '''African Union (AU)'''; [[Kifaransa]]: '''Union Africaine (UA)'''; [[Kihispania]]: '''Unión Africana (UA) '''; [[Kireno]]: '''União Africana (UA) ''') <ref> [http://au.int/en/sites/default/files/PROTOCOL_AMENDMENTS_CONSTITUTIVE_ACT_OF_THE_AFRICAN_UNION.pdf Official Languages AU "Art. 11 AU" Protocol on amendments to the constitutive act of the African Union] </ref> ni muungano wa nchi 55 za [[Afrika]] ulioanzishwa mnamo Julai [[2002]]. |
'''Umoja wa Afrika (UA)''' (kwa [[Kiingereza]]: '''African Union (AU)'''; [[Kifaransa]]: '''Union Africaine (UA)'''; [[Kihispania]]: '''Unión Africana (UA) '''; [[Kireno]]: '''União Africana (UA) ''') <ref> [http://au.int/en/sites/default/files/PROTOCOL_AMENDMENTS_CONSTITUTIVE_ACT_OF_THE_AFRICAN_UNION.pdf Official Languages AU "Art. 11 AU" Protocol on amendments to the constitutive act of the African Union] </ref> ni muungano wa nchi 55 za [[Afrika]] ulioanzishwa mnamo Julai [[2002]]. |
||
Pitio la 09:20, 20 Machi 2019
Umoja wa Afrika (UA) (kwa Kiingereza: African Union (AU); Kifaransa: Union Africaine (UA); Kihispania: Unión Africana (UA) ; Kireno: União Africana (UA) ) [1] ni muungano wa nchi 55 za Afrika ulioanzishwa mnamo Julai 2002.
Umoja huu unaendeleza kazi za Umoja wa Muungano wa Afrika (kwa Kiingereza: Organisation of African Union - OAU) uliokuwepo 1963 hadi 2002.
Nia ya umoja huu ni kujenga muundo na mfumo wa kisiasa, wa kiuchumi, na wa kijamii ili kufikia wakati ambapo bara la Afrika litakuwa na bunge moja, benki moja, jeshi moja, rais mmoja, sarafu moja, n.k.
Dhumuni kubwa la umoja huu ni kuunganisha nguvu za mataifa ya Afrika ili kuweza kutatua matatizo yanayokabili bara hili kama vile vita, njaa, Ukimwi, n.k.
Nchi wanachama
Umoja wa Afrika ina nchi wanachama 55, yaani nchi zote za bara la Afrika (baada ya kurudi kwa Moroko, iliyokuwa imejiondoa mwaka 1985 kwa sababu UA ilitambua Sahara ya Magharibi kuwa nchi ya kujitegemea wakati Moroko inadai ya kwamba ni eneo la majimbo yake ya kusini). [2]Hata hivyo mwaka 2016 Moroko ilionyesha nia ya kujiunga tena na UA.[3]
Mkutano wa kwanza wa Bunge la Umoja wa Afrika ulifanyika mwaka 2004 huko Afrika Kusini.
Mikutano mikuu ya UA
- Durban (Afrika Kusini): 9-11 Jul. 2002.
- Maputo (Msumbiji): 10-11 Jul. 2003.
- Sirte (Libya), mkutano wa dharura: Feb. 2004.
- Addis Ababa (Ethiopia): 6-8 Jul. 2004.
- Abuja (Nigeria): 24-31 Jan. 2005.
- Sirte (Libya): 28 Jun. - 5 Jul. 2005.
- Khartoum (Sudan): 16-24 Jan. 2006.
Viongozi
- Thabo Mbeki 9 July 2002 10 July 2003 South Africa
- Joaquim Chissano 10 July 2003 6 July 2004 Mozambique
- Olusegun Obasanjo 6 July 2004 24 January 2006 Nigeria
- Denis Sassou-Nguesso 24 January 2006 24 January 2007 Jamhuri ya Kongo
- John Kufuor 30 January 2007 31 January 2008 Ghana
- Jakaya Kikwete 31 January 2008 2 February 2009 Tanzania
- Muammar al-Gaddafi 2 February 2009 31 January 2010 Libyan Arab Jamahiriya
- Bingu wa Mutharika 31 January 2010 31 January 2011 Malawi
- Teodoro Obiang Nguema Mbasogo 31 January 2011 29 January 2012 Equatorial Guinea
- Yayi Boni 29 January 2012 27 January 2013 Benin
- Hailemariam Desalegn 27 January 2013 30 January 2014 Ethiopia
- Mohamed Ould Abdel Aziz 30 January 2014 30 January 2015 Mauritania
- Robert Mugabe 30 January 2015 30 January 2016 Zimbabwe
- Idriss Déby 30 January 2016 madarakani Chad
Mwenyekiti wa Kamati Kuu ya UA ni N. Dlamini-Zuma.
Spika wa Bunge la Umoja wa Afrika ni Roger Nkodo Dang.
Tanbihi
- ↑ Official Languages AU "Art. 11 AU" Protocol on amendments to the constitutive act of the African Union
- ↑ [1]
- ↑ "Morocco seeks to rejoin African Union after 32 years". BBC News. 18 July 2016. Retrieved 18 July 2016.
Viungo vya nje
- (Kiingereza) Tovuti ya Umoja wa Afrika
Makala hii kuhusu mambo ya siasa bado ni mbegu. Unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuongezea habari. |