Amerika ya Kusini

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Amerika Kusini)
Mahali pa Amerika ya Kusini duniani.
Waindio kama hao Wayuu nchini Venezuela ni wenyeji asilia wa Amerika Kusini hata kama leo hii wamekuwa wachache katika nchi nyingi za bara hili

Amerika ya Kusini ni bara la magharibi ambalo kwa kiasi kikubwa sana linaenea upande wa kusini wa Ikweta.

Inapakana na Bahari ya Pasifiki upande wa Magharibi, na Bahari ya Atlantiki upande wa Mashariki.

Kaskazini inaunganika na Amerika ya Kaskazini kwa njia ya shingo ya nchi ya Panama.

Jina la "Amerika"[hariri | hariri chanzo]

Neno "Amerika" limetokana na jina la kwanza la Mwitalia Amerigo Vespucci (1451-1512). Vespucci alikuwa baharia na mfanyabiashara katika utumishi wa familia ya Medici kutoka Firenze (Italia). Tangu mwaka 1499 alisafiri kwenye pwani za Amerika ya Kusini na Amerika ya Kati akaandika kitabu juu ya safari zake. Humo aliandika ya kwamba hakukubaliana na Kristoforo Kolumbus ya kwamba visiwa na nchi zilizofikiwa na Kolumbus zilikuwa sehemu ya Uhindi. Amerigo alipendekeza ya kwamba zilikuwa sehemu za "dunia mpya" au bara jipya akiwa mtu wa kwanza kuandika hivyo.

Mwanajiografia Mjerumani Martin Waldseemüller alitumia jina la "Amerika" kwa heshima ya Amerigo alipochora ramani yake ya dunia ya mwaka 1507.

Jiografia ya Amerika Kusini[hariri | hariri chanzo]

Topografia ya Amerika Kusini (milima, mito, tambarare)

Amerika ya kusini huwa na kanda 3 kubwa:

  • Milima ya Andes inayoelekea upande wa magharibi kutoka kaskazini hadi kusini
  • Mabeseni ya mito upande wa mashariki wa Andes
  • maeneo ya nyanda za juu upande wa mashariki wa Andes

Zote ziko juu ya bamba la Amerika ya Kusini

Andes ni safu ya milima ndefu zaidi duniani, ikiwa na urefu wa kilomita 7,500 kuanzia Venezuela hadi Patagonia (Argentina).

Kutokea kwa milima hii kulisababishwa na mgongano wa mabamba ya gandunia ya Amerika Kusini na Nasca, ilhali bamba la Nasca linasukumwa chini ya bamba la Amerika ya Kusini na kulipandisha juu, hapo pia milima ya Andes inakunjwa juu na mchakato huu unaendelea. Ndiyo asili ya mitetemeko ya ardhi inayotikisisha pwani ya Pasifiki mara kwa mara.

Mlima mrefu ni Aconcagua yenye kimo cha mita 6962 juu ya UB; uko mpakani kati ya Argentina na Chile.

Sehemu ya kusini kabisa ni rasi ya Cape Hoorn.

Tambarare kubwa ni beseni ya mto Amazonas ulio na urefu wa kilomita 6,448 na matawimto 10,000. Mto Amazonas unapokea maji yake hasa kutoka Andes.

Upande wa kaskazini liko beseni la Orinoco linalotengwa na Amazonas na milima ya Guayana.

Kusini mwa bara liko beseni la mto Paraguay na mto Parana inayokutana katika Rio de la Plata.

Nyanda za juu ziko Guayana, Brasil na Patagonia ya mashariki (Argentina).

Kuna visiwa ambavyo kisiasa ni sehemu ya nchi za Amerika Kusini ingawa kijiografia ziko nje ya bara lenyewe:

Biolojia na wanyama[hariri | hariri chanzo]

Mla sisimizi ni mwenyeji wa Amerika Kusini.
Mwendapole anapendelea kutembea mitini akijitundika matawini.

Kibiolojia Amerika ya Kusini ni eneo lenya tabia za pekee pamoja na spishi nyingi za mimea na wanyama zinazopatikana huko tu. Sababu yake ni kwamba katika historia ya sayari yetu bara hili lilikaa miaka milioni 100 bila kugusana na mabara mengine, hadi kutokea kwa shingo ya nchi ya Panama miaka milioni 3 iliyopita. Kwa hiyo huko zilitokea spishi ambazo hazipatikani kwenye sehemu nyingine za dunia.

Kati ya wanyama ambao ni wa pekee kuna

Historia[hariri | hariri chanzo]

Kabla ya kuingia kwa Wazungu[hariri | hariri chanzo]

Mji wa Kifalme wa Inka katika Andes ya Peru.
Inka Pachacutec akisali katika hekalu la mungu jua. Dini hiyo ilidai watu wengi wachinjwe kama kafara.

Kufuatana na wachunguzi wengi, watu wa kwanza waliingia Amerika takriban miaka 15,000 - 20,000 iliyopita kutoka Asia.

Jenetikia inaonyesha kuwa DNA za Waindio na za wakazi asilia wa Siberia (Asia ya Kaskazini) zinaonyesha urithi wa pamoja [1].

Wakati wa enzi ya barafu kulikuwa na shingo ya nchi baina ya Asia na Amerika kwa sababu uwiano wa bahari ulikuwa wa chini zaidi kuliko leo; hapo vikundi vya wawindaji na wavuvi waliweza kupita[2][3].

Wachunguzi wengine huona ya kwamba uhamiaji huu ulianza mapema zaidi, labda miaka 40,000 hivi iliyopita.[4][5]

Kutoka Alaska na Amerika ya Kaskazini waliendelea kuelekea kusini; wanaaminiwa walifika karibu na ncha ya bara.

Dalili za kwanza za kilimo zinajulikana kutoka beseni ya Amazonas tangu miaka 8,500 iliyopita. hapo watu walianza kulima viazi, pilipili na maharagwe.

Ufugaji wa Lama na alpaka ulianza mnamo mwaka 3500 KK.

Mabaki ya vijiji na miji ya kudumu katika Andes yanajulikana tangu milenia ya pili KK.

Tamaduni za Waindio wa Amerika Kusini ziliboresha kilimo na kugundua mazao mengi ambayo yanatupa leo hii vyakula muhimu kama vile mahindi, viazi, viazi vitamu, muhogo na karanga.

Watu hao walianza pia kujenga jamii kubwa zilizoendelea kuwa madola na milki na kuendesha biashara ya mbali. Kabla ya kuja kwa Wahispania mnamo mwaka 1500 ni hasa milki ya Inka iliyounganisha sehemu kubwa ya nchi za Andes.

Jamii hizo ziliweza kuwasiliana katika maeneo makubwa sana na kujenga miji mikubwa.

Mafanikio yao ya kijamii, ya kiuchumi na ya kisanii ni ya ajabu kwa sababu katika teknolojia waliendesha shughuli bila matumizi ya vyombo vya metali. Ingawa walitengeneza mapambo mazuri sana ya dhahabu, fedha, shaba na bronzi, kuna mifano michache sana ya matumizi ya bronzi au metali nyingine kwa vifaa na silaha.

Kuna makadirio ya kwamba idadi ya wakazi asilia, yaani Waindio, ilikuwa milioni 30 hivi katika Amerika ya Kusini kabla ya kufika kwa Wazungu.

Kipindi cha ukoloni[hariri | hariri chanzo]

Kufika kwa Wareno kwenye pwani ya Brazil mnamo mwaka 1500 (taswira ya mwaka 1922).
Kikosi cha Wahispania wanavamia Chile mnamo mwaka 1530: silaha za feleji, askari farasi na mbwa wakali walihakikisha ushindi wao dhidi ya wenyeji wenye silaha za mawe tu; taswira ya karne ya 19.

Mwaka 1492 Kristoforo Kolumbus alifika kwenye visiwa vya Karibi na kwenye safari yake ya tatu mwaka 1498 alipita kwenye pwani ya Venezuela.

Nchi mbili jirani za Hispania na Ureno, zilizokuwa viongozi wa teknolojia ya usafiri kwa bahari wakati ule, zilifanya mkataba wa kugawana dunia kati yao. Kutokana na mkataba huo maeneo ya Brazil ya leo yalikuwa chini ya Ureno na sehemu nyingine za Amerika Kusini chini ya Hispania.

Nchi zote mbili zilituma wamisionari Wakatoliki na kuruhusu Kanisa Katoliki pekee kufanya kazi kule. Hapo ndipo msingi kwa lugha za Kihispania na Kireno kuwa lugha ya watu wengi kwenye bara hili na asilimia kubwa kuwa wafuasi wa Kanisa Katoliki hadi leo.

Wahispania wachache walifaulu kuvamia na kuteka madola yote ya wenyeji. Sababu muhimu ilikuwa tofauti kubwa ya teknolojia, maana wakazi asilia bado walitumia zaidi silaha za mawe na ubao, ilhali Wahispania walifika na panga za feleji, gobora na farasi wa vita.

Sababu nyingine ni ya kibiolojia, kwa sababu Wazungu walileta magonjwa yasiyojulikana kwa wenyeji wa Amerika. Kuna makadirio ya kwamba magonjwa hayo yaliua mamilioni ya Waindio na hivyo kudhoofisha upinzani wao dhidi ya wavamizi Wazungu waliokuwa wachache kwa miaka mingi.

Kiutawala Wahispania waliunda majimbo makubwa yaliyosimamiwa na afisa mwenye cheo cha "mfalme mdogo" (his. virrei, ing. viceroy). Majimbo hayo yalikuwa chini ya serikali kuu ya Madrid, lakini yalijitawala chini ya wafalme wadogo waliotumwa kutoka Hispania.

Majimbo ya kwanza yalikuwa "Hispania Mpya" (Meksiko na Venezuela) na "Peru" (maeneo makubwa ya Andes pamoja na Panama). Mwaka 1717 maeneo ya Ekuador, Kolombia na Venezuela yalikunganishwa kuwa jimbo kubwa la "Granada Mpya". Mwaka 1776 Bolivia, Chile, Argentina na Paraguay zilikuwa "Rio de la Plata".

Fedha kutoka migodi ya Peru ilikuwa msingi wa utajiri wa Hispania na nafasi yake kama dola muhimu katika Ulaya.

Kijamii kulikuwa na matabaka. Tabaka la juu walikuwa Wahispania waliotumwa kutoka kwao pamoja na familia wenyeji Wahispania. Sehemu kubwa ya wakazi walikuwa na asili ya mchanganyiko wa Wazungu na Waindio; katika nchi kadhaa, hasa katika nyanda za juu za Andes na katika misitu ya mvua kulikuwa bado na idadi kubwa ya Waindio. Kwenye maeneo ya pwani watumwa kutoka Afrika waliingizwa. Serikali ya Kihispania ilijaribu kuwatenganisha wakazi kufutana na rangi na kutenga vyeo vya juu kwa Wazungu watupu, lakini hii ilikuwa vigumu kutokana na asilimia kubwa ya mchanganyiko.

Uhuru[hariri | hariri chanzo]

Tangazo la uhuru wa Peru mwaka 1821.

Mnamo mwaka 1800 harakati ya kutafuta uhuru ilipata nguvu. Kwa upande moja walowezi Wahispania walisikia juu ya uhuru wa makoloni ya Uingereza katika Marekani. Walisikitika pia kutawaliwa na nchi iliyo mbali katika Ulaya, ambayo haikuangaliwa tena na sehemu ya wenyeji kama nchi mama. Kwa upande mwingine Hispania ilidhoofika kutokana na vita za Napoleon, uvamizi wa Wafaransa na mapinduzi katika Hispania.

Tangu mwaka 1808 Simon Bolivar aliongoza kikosi cha wanamgambo na kupigana na jeshi la kikoloni hadi kushinda mwaka 1813. Argentina ilifuata mwaka 1816 na kujitangazia uhuru, Chile na Kolombia zikafuata mwaka 1818. Mapigano ya mwisho yalitokea mwaka 1824 huko Peru: waasi walishinda na Hispania iliondoka katika Amerika ya Kusini ikibaki kwenye visiwa vya Karibi.

Baada ya uhuru sehemu kubwa ya Amerika Kusini iliunganishwa katika "Kolombia Kubwa" lakini hili dola jipya haikudumu, hivyo tangu mwaka 1832 madola ya leo yalitokea.

Urithi wa ukoloni: lugha na utamaduni[hariri | hariri chanzo]

Kwa lugha zake mbalimbali bara linahesabiwa katika "Amerika ya Kilatini" kwa sababu wakazi wengi hutumia lugha za Kirumi, hasa Kihispania na Kireno, zilizotokana na Kilatini.

Sababu yake ni ya kwamba sehemu kubwa ya bara hili lilikuwa koloni la Hispania. Brazil ilikuwa koloni la Ureno. Nchi zote mbili ziliacha tabia za utamaduni wao pamoja na dini (Kanisa Katoliki) na lugha zilizokuwa lugha za kitaifa.

Nchi za Guyana pekee zilikuwa makoloni ya mataifa mengine ya Ulaya zilizoacha lugha zao:

Orodha ya nchi na maeneo[hariri | hariri chanzo]

Katika bara hilo kuna nchi huru zifuatazo:

Maeneo chini ya utawala wa mataifa ya nje ni:

Taarifa zaidi zinapatikana katika jedwali lifuatalo:

Jina la nchi au eneo,
bendera
Eneo
(km²)
Wakazi
(2007)
Wakazi kwa km² Mji mkuu
Argentina
2,766,890  40,677,348 14.3 Buenos Aires
Bolivia
1,098,580   9,247,816 8.1 La Paz, Sucre
Brazil
8,514,877 191,908,598 22.0 Brasilia
Chile
756,950  16,454,143 21.1 Santiago de Chile
Kolombia
1,138,910  45,013,674 37.7 Bogotá
Ekuador
283,560  13,927,650 47.1 Quito
Falkland Islands
(Ufalme wa Muungano)
12,173       3,140[6] 0.26 Port Stanley
Guyana ya Kifaransa
(Ufaransa)
91,000     221,450 (Jan. 2008)[7] 2.7 Cayenne
Guyana
214,970     770,794 3.6 Georgetown
Paraguay
406,750   6,347,884 15.6 Asunción
Peru
1,285,220  28,220,764 21.7 Lima
Visiwa vya South Georgia na South Sandwich
(Ufalme wa Muungano)
3,093           20 0 Grytviken
Surinam
163,270     438,144 2.7 Paramaribo
Uruguay
176,220   3,477,778 19.4 Montevideo
Venezuela
912,050  26,414,815 27.8 Caracas
Jumla &Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ","..Expression error: Unrecognized punctuation character ",".17,824,513 &Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ",".Expression error: Unrecognized punctuation character ","..Expression error: Unrecognized punctuation character ",".382,426,313 21.5

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu maeneo ya Amerika Kusini bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Amerika ya Kusini kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.