Bolivia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Bolivia
Bendera
Nembo
Mji mkuu (na mkubwa zaidi){{{mji_mkuu}}}
16°29′ S 68°8′ W
Lugha rasmi{{{lugha_rasmi}}}
Serikali{{{serikali}}}
{{{vyeo_viongozi}}}{{{majina_viongozi}}}
{{{muundo_uhuru}}}{{{tarehe_uhuru}}}
Eneo
 • Eneo la jumla{{{eneo_jumla}}}
 • Maji (%){{{maji}}}
Idadi ya watu
Pato la TaifaKadirio la 2023
 • Jumla{{{pato}}}
 • Kwa kila mtu{{{pato_kwa_mtu}}}
Pato Halisi la TaifaKadirio la 2023
 • Jumla{{{pato_halisi}}}
 • Kwa kila mtu{{{pato_halisi_kwa_mtu}}}
Maendeleo ({{{mwaka_maendeleo}}}){{{maendeleo}}}
Fedha{{{fedha}}}
Majira ya saa{{{majira_saa}}}
Muundo wa tareheDD/MM/YYYY
Ramani ya Bolivia
Mji wa La Paz
Uyuni

Bolivia (jina linatokana na shujaa Simon Bolivar) ni nchi isiyo na mwambao wa bahari katika Amerika Kusini.

Imepakana na Brazil, Paraguay, Argentina, Chile na Peru.

Jiografia[hariri | hariri chanzo]

Nchi inakatwa na safu mbili za milima ya Andes zenye kimo hadi mita 6500 juu ya UB.

Nyanda za juu (kwa Kihispania: "Altiplano") zinakaliwa na wakazi wengi (80%) ziko kwenye kimo cha mita 3.000 hadi 4.000. Altiplano ni takriban theluthi moja ya eneo la nchi; sehemu nyingi ni tambarare ya "llanos" ambayo ni nchi ya chini yenye joto ambayo ina sehemu mbili: savana kavu za Gran Chaco na misitu minene ya beseni ya Amazonas.

Ziwa la Titicaca liko kwenye Altiplano.

Bolivia ni kati ya nchi maskini zaidi za Amerika Kusini.

Watu[hariri | hariri chanzo]

Tofauti na nchi nyingine za bara hilo, wakazi asilia (Waindio) ni sehemu kubwa ya wananchi (55%), wakifuatwa na machotara (30%) na watu wenye asili ya Ulaya (15%).

Lugha rasmi ziko 37, kuanzia Kihispania na lugha nyingi asilia.

Upande wa dini, Kanisa Katoliki linaongoza (78%), likifuatwa na Uprotestanti (19%).

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Nchi na maeneo ya Amerika Kusini

Argentina | Bolivia | Brazil | Chile | Ekuador | Guyana | Guyani ya Kifaransa | Kolombia | Paraguay | Peru | Surinam | Uruguay | Venezuela

Makala hii kuhusu maeneo ya Bolivia bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Bolivia kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.