Nenda kwa yaliyomo

Ulaya

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Ulaya (asili ya jina ni neno la Kiarabu ولاية, wilaayatun[1]; inaitwa pia Uropa kutoka Kigiriki: "Ευρώπη", jina la mungu jike Europa) ni bara lililoko katika Kaskazini ya Dunia, likipakana na Bahari ya Aktiki upande wa kaskazini, Bahari ya Atlantiki upande wa magharibi, na Bahari ya Mediterania upande wa kusini. Mpaka wake wa mashariki kwa kawaida hufafanuliwa kupitia Milima ya Ural, Mto Ural, Bahari ya Kaspi, Milima ya Kaukazi, na Bahari Nyeusi, ingawa mipaka hii ni ya kijiografia na kihistoria zaidi kuliko ya kisiasa. Kwa eneo la takriban kilomita za mraba milioni 10.18, Ulaya ni bara dogo la pili baada ya Australia lakini lina idadi kubwa ya watu, ikifikia zaidi ya milioni 750, na hivyo kuwa moja ya maeneo yenye msongamano mkubwa wa watu duniani.

Ulaya ina historia ndefu na imechangia pakubwa katika maendeleo ya kisiasa, kiuchumi, na kitamaduni duniani. Bara hili lina mataifa 44 yanayotambulika kimataifa, yakiwemo mataifa makubwa kama Ujerumani, Ufaransa, na Uingereza, pamoja na madola madogo kama Vatikani na Liechtenstein. Umoja wa Ulaya (EU) ni moja ya miungano muhimu ya kisiasa na kiuchumi katika bara hili, ukiwa na wanachama 27. Aidha, Ulaya imekuwa kitovu cha mapinduzi mbalimbali, kuanzia Mapinduzi ya Kitaaluma na ya Viwanda hadi maendeleo ya demokrasia ya kisasa, na imeendelea kuwa na ushawishi mkubwa katika masuala ya kimataifa.

Ramani

Ulaya kutoka angani.
Ulaya duniani.
Lugha za Ulaya.
Kanda za kiutamaduni za Ulaya kadiri ya Ständiger Ausschuss für geographische Namen (StAGN) ya Ujerumani.
Ulaya mwaka 1000 hivi.

Utawala

Katika karne ya 20, baada ya vita kuu mbili, nchi mbalimbali za Ulaya zilianza kushirikiana kwa njia mbalimbali:

Kanda za Ulaya

Katika orodha inayofuata kanda zinatajwa katika utaratibu wa Umoja wa Mataifa (UN categorisations/map). Lakini utaratibu huo haukubaliki ndani ya Ulaya kwa nchi za Ulaya ya Kati. Wajerumani, Waaustria, Waswisi, Wacheki, Waslovakia na Wapolandi hukubaliana ya kwamba wenyewe si Ulaya ya Magharibi wala ya Mashariki ila Ulaya ya Kati. Kuna majadiliano kuhusu mipaka ya kanda hili yasiyokwisha bado, kwa mfano suala la Hungaria au Latvia.

Ulaya Mashariki

NchiBenderaMji MkuuIdadi ya Watu (2024)
BelarusMinsk9,200,000
BulgariaSofia6,400,000
Jamhuri ya CzechPrague10,500,000
HungaryBudapest9,600,000
MoldovaChisinau2,500,000
PolandWarsaw37,700,000
RomaniaBucharest19,000,000
RussiaMoscow144,000,000
SlovakiaBratislava5,400,000
UkraineKyiv36,000,000

Ulaya ya Kaskazini

NchiBenderaMji MkuuIdadi ya Watu (2024)
DenmarkCopenhagen5,900,000
EstoniaTallinn1,300,000
FinlandHelsinki5,600,000
IcelandReykjavik380,000
IrelandDublin5,100,000
LatviaRiga1,800,000
LithuaniaVilnius2,700,000
NorwayOslo5,500,000
SwedenStockholm10,500,000
UingerezaLondon68,000,000

Ulaya ya Magharibi

NchiBenderaMji MkuuIdadi ya Watu (2024)
AustriaVienna9,100,000
UbelgijiBrussels11,800,000
UfaransaParis65,000,000
UjerumaniBerlin83,000,000
LiechtensteinVaduz39,000
LuxembourgLuxembourg (jiji)660,000
MonacoMonaco (jiji)39,000
UholanziAmsterdam17,800,000
UswisiBern8,800,000

Ulaya ya Kusini

NchiBenderaMji MkuuIdadi ya Watu (2024)
AlbaniaTirana2,800,000
AndorraAndorra la Vella79,000
Bosnia na HerzegovinaSarajevo3,200,000
KroatiaZagreb3,800,000
CyprusNicosia1,200,000
UgirikiAthens10,200,000
ItaliaRome59,000,000
MaltaValletta520,000
MontenegroPodgorica620,000
Macedonia KaskaziniSkopje1,800,000
San MarinoSan Marino (mji)34,000
SerbiaBelgrade6,600,000
SloveniaLjubljana2,100,000
HispaniaMadrid47,800,000
Vatican CityVatican City (mji)800
UrenoLisbon10,100,000

Nchi za Ulaya

Orodha kamili ya nchi za Ulaya ikitaja ukubwa wa eneo, idadi ya watu, miji mikuu na miji mikubwa zaidi pamoja na lugha rasmi. Orodha hii haionyeshi ukanda wa nchi husika. Tazama juu kupata kanda za Ulaya.

Orodha ya Nchi na Maeneo ya Ulaya
BenderaNchi/MaeneoEneo (km²)Idadi ya WatuMji MkuuJiji KubwaLugha Rasmi
Albania28,7482,829,741TiranaTiranaKialbania
Andorra46879,034Andorra la VellaAndorra la VellaKihispania
Armenia29,7432,767,923YerevanYerevanKiarmenia
Austria83,8799,006,398ViennaViennaKijerumani
Azebajani (zaidi ni Asia)86,60010,353,269BakuBakuKiazabajani
Aislandi103,000366,425ReykjavikReykjavikKiaislandi
Ayalandi70,2734,994,724DublinDublinKiingereza, Kigaeli
Belarusi207,6009,349,645MinskMinskKibelarusi, Kirusi
Bulgaria110,9936,447,710SofiaSofiaKibulgaria
Bosnia na Herzegovina51,1973,276,000SarajevoSarajevoKiserbia, Kikroeshia, Kibosnia
Estonia45,2271,331,796TallinnTallinnKiestonia
Hungaria93,0289,606,259BudapestBudapestKihungaria
Italia301,34060,317,116RomeRomeKiitalia
Jojia (zaidi ni Asia)69,7003,688,600TbilisiTbilisiKijojia
Korasia56,5943,850,695ZagrebZagrebKikorasia
Kosovo10,8871,798,188PristinaPristinaKikosovo
Kupro9,2511,244,188NicosiaNicosiaKigiriki, Kituruki
Latvia64,5891,882,000RigaRigaKilatvia
Liechtenstein16039,315VaduzSchaanKijerumani
Lithuania65,3002,794,000VilniusVilniusKilithuania
Luxembourg2,586634,814Luxembourg CityLuxembourg CityKifaransa, Kijerumani, Kiluxembourg
Malta316514,564VallettaBirkirkaraKimalta, Kiingereza
Moldova33,8462,603,000ChisinauChisinauKimoldova
Monako2.0239,511MonacoMonacoKifaransa
Norwei385,2075,391,369OsloOsloKinorwei
Polandi312,69638,265,017WarsawWarsawKipolandi
San Marino6133,600San MarinoSan MarinoKiitalia
Ubelgiji30,68911,584,008BrusselsAntwerpKiholanzi, Kifaransa, Kijerumani
Ucheki78,86610,686,269PraguePragueKicheki
Udeni42,9255,932,654CopenhagenCopenhagenKideni
Ufaransa551,69568,042,591ParisParisKifaransa
Ufini338,4245,541,037HelsinkiHelsinkiKifini, Kiswidi
Ufalme wa Muungano243,61067,736,802LondonLondonKiingereza
Ugiriki131,95710,724,599AthensAthensKigiriki
Uhispania505,99047,450,795MadridMadridKihispania
Uholanzi41,54317,407,585AmsterdamRotterdamKiholanzi
Ujerumani357,02283,190,556BerlinBerlinKijerumani
Ureno92,09010,295,909LisbonLisbonKireno
Urusi (Sehemu ya Ulaya)17,098,242146,599,183MoscowMoscowKirusi
Vatikani0.49825Vatican CityVatican CityKilatini, Kiitalia

Tanbihi

1. Kanda zinazotajwa (Ulaya ya Kusini – magharibi n.k.) zinafuata utaratibu wa Umoja wa Mataifa UN categorisations/map. Nchi kadhaa zinazotajwa hapo chini zinaweza kuhesabiwa kuwa sehemu ya Ulaya na pia bara nyingine (Asia, Afrika, au Oceania). Hii inategemea na namna ya kugawa kontinenti; pia wakazi wenyewe wanaweza kujielewa tofauti na majirani yao.

2. Urusi ni nchi ya kontinenti mbili za Ulaya ya Mashariki na Asia; namba za wakazi na za eneo zimetasjwa kwa ajili ya sehemu ya Kiulaya pekee.

3–5. Guernsey, Kisiwa cha Man, and Jersey ni maeneo ya kujitegemea chini ya Taji la Ufalme wa Uingereza.

6. Namba za Ureno hazijumlishi Visiwa vya Madeira, ambazo ni sehemu ya Ureno magharibi ya Marokko katika Afrika.

7. Namba za Hispania hazijumlishi Visiwa vya Kanari magharibi ya Marokko katika Afrika, wa maeneo ya Ceuta na Melilla ambayo ni sehemu za Hispania kwenye pwani ya Moroko, Afrika ya Kaskazini.

8. Namba za Ufaransa hazijumlishi maeneo yake yaliyopo Amerika ya Kati au Kusini, Bahari Hindi au Oceania.

9. Uholanzi: Idadi ya wakazi ni ya 2004; Amsterdam ni Mji Mkuu lakini Den Haag ni makao makuuy a serikali.

10. Armenia huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Mashariki

11. Azerbaijan huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Mashariki; idadi ya wakazi na eneo zimetajwa za sehemu ya Ulaya pekee.

12. Kupro huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Kusini; idadi ya wakazi na eneo zimetajwa za sehemu zisozo chini ya Dola ya Kituruki ya Cyprus.

13. Georgia huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Mashariki; idadi ya wakazi na eneo zimetajwa za sehemu ya Ulaya pekee.

14. Uturuki ni nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Kusini; namba zinazotajwa zinahusiana na sehemu ndogo ya Magharibi pakee iliyomo Ulaya hasa jimbo lote la Istanbul.

15. Kazakhstan huhesabiwa mara nyingi kuwa nchi ya kimabara katika Asia ya Magharibi (kufuatana na kanda za UM) na Ulaya ya Mashariki; idadi ya wakazi na eneo zimetajwa za sehemu ya Ulaya pekee.

Tazama pia

Marejeo

  1. Hivyo asili ya neno "Ulaya" ni sawa na "wilaya"; Krapf 1882 Swahili-English dictionary anaeleza: ""ULAYA (WALAYA au WILAYA ya) ... mother-country in contradistinction to colonies, foreign possessions or parts"; Sacleux 1939 Dictionnaire Swahili-Francais anataja kama etimolojia ya Ulaya "Ar. Hind. ولاية wilaya, pays etranger" (=nchi ya kigeni); Madan 1903 "Wilaya, n. (1) native land, home, but commonly used of foreigners, and so (2) Europe. Ulaya Uzungu, Europe. U, Hindi, India. Ulaya wa Wareno, Portugal