Venezuela

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Venezuela


Ramani ya Venezuela.

Venezuela ni nchi kaskazini mwa Amerika ya Kusini.

Imepakana na Brazil, Guyana na Kolombia.

Mbele ya pwani ya Bahari ya Karibi kuna madola ya visiwani ya Aruba, Antili za Kiholanzi na Trinidad na Tobago.

Venezuela ilikuwa koloni la Hispania hadi mwaka 1811 na lugha ya Kihispania ni lugha ya kitaifa.

Kikatiba Venezuela ni shirikisho la jamhuri.

Mji mkuu ni Caracas.

Asili ya jina "Venezuela"[hariri | hariri chanzo]

Jina la nchi ni umbo la Kihispania la jina la mji wa Venezia (Italia). Amerigo Vespucci, mpelelezi Mwitalia katika utumishi wa mfalme wa Hispania, aliona vijiji vya wenyeji waliojenga nyumba juu ya maboriti yaliyosimamishwa katikati ya maji karibu na mwambao pasipo kina. Vijiji vilimkubusha mji wa Venezia uliojengwa vilevile. Venezuela yamaanisha "Venezia Ndogo" katika Kihispania.

Jiografia[hariri | hariri chanzo]

Nyumba ya "palafito" jinsi ilivyoonekana zamani za Amerigo Vespucci.

Venezuela ina eneo la km² 916,445 (kama Namibia) ikiwa na pwani yenye urefu wa km 2,800. Asilimia 39 za eneo hili ni misitu, mashamba ya kulimwa ni 4%, eneo la mifugo 20%, mazao ya kudumu kama kahawa 1%.

Kuna kanda nne za kijiografia:

Milima ya meza[hariri | hariri chanzo]

Nyanda za juu za Guayana zina milima ya pekee: kuna milima ya meza 115 inayoitwa "tepui" katika lugha ya wakazi asilia. Kiekolojia hilo ni eneo muhimu kwa sababu milima mingi ina mimea na wanyama wa pekee, tofauti na milima jirani, na inapatikana hapa tu kote duniani.

Maporomoko marefu duniani yatelemka kutoka milima hii kama vile maporomoko ya Salto del Angel ("anguko la malaika") ambako maji huanguka mita 965.

Mito[hariri | hariri chanzo]

Mto mkubwa wa Venezuela ni Orinoco wenye urefu wa km 2574 unaoishia katika Atlantiki. Lakini mkono wa Brazo Casiquiare unajitenga na kuishia katika mto wa Amazonas nchini Brazil.

Matawimto muhimu ya Orinoco ni Rio Apure na Rio Caroni.

Majimbo katika shirikisho[hariri | hariri chanzo]

Tazama pia Majimbo ya Venezuela
Mlima wa meza Mt. Roraima
Los Barrios ni mitaa ya vibanda vya Caracas


Venezuela ni shirikisho la madola au majimbo 23 ya kujitawala, maeneo yasiyojitawala na mkoa wa shirikisho wa Caracas.

Jimbo Mji Mkuu Wakazi Eneo Kanda
Amazonas Puerto Ayacucho 70,464 180,144 km² Guayana
Anzoátegui Barcelona 1,222,225 43,300 km² Nor - Oriental
Apure San Fernando de Apure 377,756 76,500 km² Llanos
Aragua Maracay 1,449,616 7,014 km² Central
Barinas Barinas 624,508 35,200 km² Andean
Bolívar Ciudad Bolívar 1,214,846 238.000 km² Guayana
Carabobo Valencia 1,932,168 4,650 km² Central
Cojedes San Carlos 253,105 14,800 km² Central
Delta Amacuro Tucupita 97,987 40,200 km² Guayana
Falcón Coro 763,180 24,800 km² Central - Occidental
Guárico San Juan de los Morros 627,086 64,986 km² Llanos
Lara Barquisimeto 1,556,415 19,800 km² Central - Occidental
Mérida Mérida 715,268 11,300 km² Andean
Miranda Los Teques 2,330,872 7,950 km² Capital
Monagas Maturín 712,626 28,930 km² Nor - Oriental
Nueva Esparta La Asunción 712,626 1,150 km² Insular
Portuguesa Guanare 725,740 15,200 km² Central - Occidental
Sucre Cumaná 786,483 11,800 km² Nor - Oriental
Táchira San Cristóbal 992,669 11,100 km² South - Occidental
Trujillo Trujillo 608,563 7,400 km² Andean
Vargas La Guaira 298,109 1,496 km² Capital
Yaracuy San Felipe 499,049 7,100 km² Central - Occidental
Zulia Maracaibo 2,983,679 63,100 km² Zulian
Dependencias Federales (maneo chini ya shirikisho) - 2,245 342 km² Insular (visiwa)
Distrito Federal Caracas (Mkoa wa shirikisho) - 2,284,921 433 km² Capital (mji mkuu)

Watu[hariri | hariri chanzo]

Wakazi wengi (51.6%) wanajiainisha kama machotara wa Kizungu-Kiindio. Wazungu ni 43.6%, wenye asili ya Afrika ni 3.5% na Waindio 2.6%. Utafiti wa DNA unaonyesha kwamba urithi wa jeni kwa asilimia 60.6 ni wa Kizungu, 23 ni wa Kiindio na 16.3 ni wa Kiafrika.

Lugha rasmi na ya kawaida ni Kihispania, ingawa lugha asilia zinakubalika kwa Waindio, na lugha nyingine zinatumiwa na wahamiaji.

Upande wa dini, 88% ni Wakristo, hasa wa Kanisa Katoliki (71%) na madhehebu mbalimbali ya Uprotestanti (17%).

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Nchi na maeneo ya Amerika Kusini

Argentina | Bolivia | Brazil | Chile | Ekuador | Guyana | Guyani ya Kifaransa | Kolombia | Paraguay | Peru | Surinam | Uruguay | Venezuela

Makala hii kuhusu maeneo ya Amerika Kusini bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Venezuela kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.