Paramaribo
Jiji la Paramaribo | |
Nchi | Surinam |
---|
Paramaribo (jina fupi: Par'bo) ni mji mkuu wa Surinam. Ina wakazi 250,000. Iko kando la mto Surinam takriban 20 km kutoka mwambao wa Bahari ya Karibi. Anwani ya kijiografia ni 5°52' N, 55°10' W.
Historia[hariri | hariri chanzo]
Jina la Paramaribo limetokana na kijiji cha wenyeji asilia "Parmirbo". Mwaka 1613 Waholanzi walijenga kituo cha biashara karibu na kijiji hiki. 1651 eneo lilikuwa chini ya utawala wa Uingereza waliojenga hapa Fort Willoughby. Waholanzi walirudi mwaka 1667 wakatwaa eneo lote na kuita kituo Fort Zeelandia na kijiji mbele yake "Nieuw Middelburgh". 1683 nyumba 27 zilihesabiwa zilizoongezeka hadi 1790 kuwa zaidi ya 1000.
Mji wa kale ulichomwa moto mara mbili 1821 na 1832.
Baada ya mwisho wa utumwa mwaka 1863 wengi waliowahi kuwa watumwa walihamia mjini na kusababisha kukua kwa Maracaibo. Tangu 1975 imekuwa mji mkuu wa Surinam
Uchumi[hariri | hariri chanzo]
Biashara ya nje kutoka Paramaribo ni hasa boksiti, sukari, mpunga, kokoa, kahawa na ubao. Kuna viwanda vya saruji, rangi na bia.
Utamaduni[hariri | hariri chanzo]
Utamaduni wa Paramaribo una pande nyingi kutokana na mchanganyiko wa watu wenye asili ya Uhindi, Afrika, Indonesia, Uchina na Ulaya. Wenyeji wanapenda mashindano ya uimbaji wa ndege wanaofugwa kwa kusudi hii. Mashindano haya hutokea kila Jumapili.
Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]
- Map of Paramaribo
- Page with some basic information and images
- Small Paramaribo gallery
- Clickable map
- (Kiingereza) Audio interview with Paramaribo resident about life in Paramaribo Archived Novemba 17, 2007 at the Wayback Machine.
- Image gallery Archived Oktoba 12, 2007 at the Wayback Machine.
- Paramaribo photo gallery
- Photo gallery
- 1st gamers site in surinam
![]() |
Makala hii kuhusu maeneo ya Amerika Kusini bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Paramaribo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |