Nenda kwa yaliyomo

Indonesia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Jamhuri ya Indonesia
Republik Indonesia (Kiindonesia)
Kaulimbiu: Bhinneka Tunggal Ika (Kijava cha Kale)
"Umoja katika Tofauti"
Wimbo wa taifa: "Indonesia Raya"
Eneo la Indonesia katika ASEAN
Indonesia katika dunia
Mji mkuu
na mkubwa
Jakarta
Lugha rasmiKiindonesia
SerikaliJamhuri ya kirais ya muungano
  Rais
Prabowo Subianto
  Makamu wa Rais
Gibran Rakabuming Raka
  Uhuru kutangazwa
17 Agosti 1945
  Kutambuliwa rasmi
27 Desemba 1949
Eneo
  Jumlakm2 1,904,569 (ya ya 14)
  Maji (asilimia)4.85%
Idadi ya watu
  Kadirio la 2024 284,973,643
  Msongamano143/km2
PLT (PPP)Kadirio la 2025
  Jumla $4.98 trilioni
  Kwa kila mtu $17,520
PLT (Kawaida)Kadirio la 2025
  Jumla $1.49 trilioni
  Kwa kila mtu $5,248
HDI (2023)0.728 juu
Gini (2024)37.9
SarafuRupia ya Indonesia (Rp)
Majira ya saaUTCUTC+7, +8, +9 (WIB, WITA, WIT)
Upande wa magariKushoto
Msimbo wa simu++62
Jina la kikoa.id

Indonesia ni nchi ya visiwa katika Asia ya Kusini-Mashariki. Iko upande wa Kusini-Mashariki kati ya Bahari ya Hindi na Pasifiki. Visiwa vyake ni sehemu ya Funguvisiwa la Malay, ingawa Guinea Mpya kwa kawaida haihesabiwi katika fungu hilo. Indonesia imepakana na Papua Guinea Mpya kwenye kisiwa cha Guinea Mpya, pia na Timor ya Mashariki kwenye kisiwa cha Timor, halafu na Malaysia kwenye kisiwa cha Borneo. Nchi nyingine zilizo karibu ni Australia, Singapuri na Ufilipino.

Indonesia ni taifa lenye wakazi wengi wa Kiislamu duniani, likiwa na watu wanaozidi milioni 280, na hivyo kuifanya kuwa nchi ya nne kwa idadi ya watu duniani. Mji mkuu wake ni Jakarta, jiji kubwa lenye shughuli nyingi za kisiasa, kiuchumi na kitamaduni. Lugha rasmi ni Kiindonesia (Bahasa Indonesia): ingawa kuna zaidi ya lugha 700 zinazozungumzwa nchini humo, lugha hiyo inatumika kama chombo cha kuunganisha wananchi wa makabila mbalimbali.

Historia ya Indonesia imeathiriwa na mchanganyiko wa dini, biashara na ukoloni. Kabla ya ukoloni, Indonesia ilikuwa nyumbani kwa falme mbalimbali zenye ushawishi mkubwa kama vile Srivijaya na Majapahit. Katika karne ya 16, Wareno na baadaye Waholanzi walifika na kudhibiti maeneo mengi, hasa kupitia Kampuni ya Kiholanzi ya India ya Mashariki. Indonesia ilijipatia uhuru kutoka kwa Uholanzi mwaka 1945 chini ya uongozi wa Sukarno. Tangu wakati huo, nchi imepitia vipindi mbalimbali vya kisiasa, ikiwa ni pamoja na utawala wa kijeshi, hadi kuanzishwa kwa demokrasia ya kisasa mwishoni mwa karne ya 20.

Jiografia

[hariri | hariri chanzo]

Indonesia ni nchi ya visiwa karibu 18,000 ilhali zaidi ya 6,000 kati ya hivyo vinakaliwa na watu.

Visiwa vikubwa vyenye wakazi wengi ni hasa vitano:

Historia

[hariri | hariri chanzo]

Visiwa vya Indonesia viliathiriwa na utamaduni wa Uhindi. Kisiasa kulikuwa na falme nyingi.

Tangu karne ya 17 Waholanzi walianza kujenga vituo na kueneza utawala wao. Waliita koloni lao "Uhindi wa Kiholanzi" ("Nederlands-Indie").

Wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia Japani ikatwaa visiwa na kuwafukuza Waholanzi.

Mwisho wa vita kiongozi Sukarno akatangaza Indonesia kama nchi huru. Waholanzi walijaribu kurudisha utawala wao lakini walilazimishwa na Marekani kukubali uhuru wa nchi.

Demografia

[hariri | hariri chanzo]

Nchi ina wakazi 270,203,917 (2020) hivyo ina nafasi ya nne kati ya mataifa makubwa duniani. Ni nchi yenye Waislamu wengi kuliko nyingine zote duniani. Makabila asili ni 300 hivi; kubwa zaidi ni Wajava (40.2 %).

Lugha rasmi ni Bahasa Indonesia (Kiindonesia) iliyoundwa katika karne ya 20 kama lugha ya taifa kutokana na lahaja ya Kimalay. Nchini kote kuna lugha za asili zaidi ya 700 (angalia orodha ya lugha za Indonesia). Jawa pia ina sanaa ya mwandiko wa kipekee maarufu kama mwandiko wa Batiki (Batik Tulus) unaochorwa kwa jora za nguo.[1]

Idadi kubwa ya wakazi (87.1 %) wanahesabiwa kuwa Waislamu (karibu wote Wasuni), 10.45 % kama Wakristo (Waprotestanti 7.38 %, Wakatoliki 3.07 %), 1.7 % kama Wahindu (hasa kwenye kisiwa cha Bali) na 0.7 % kama Wabuddha. Hizo zote ni dini zilizotambulika rasmi pamoja na ile ya Konfusio (0.05 %).

Mandhari

[hariri | hariri chanzo]

Tazama pia

[hariri | hariri chanzo]
  1. Batik S128. "Handwriting Batik (Batik Tulis) and Cities In Indonesia That Produce It". Toko Batik Online 2019. Iliwekwa mnamo 2019-05-11.{{cite web}}: CS1 maint: numeric names: authors list (link)

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
Serikali
Taarifa za jumla
WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Nchi na maeneo ya Asia

Afghanistan | Armenia2 | Azerbaijan | Bahrain | Bangladesh | Bhutan | Brunei | China | Falme za Kiarabu | Georgia2 | Hong Kong3 | Indonesia | Iran | Iraq | Israel | Jamhuri ya China (Taiwan) | Japani | Kamboja | Kazakhstan | Kirgizia | Korea Kaskazini | Korea Kusini | Kupro2 | Kuwait | Laos | Lebanoni | Macau3 | Malaysia | Maldivi | Mongolia | Myanmar | Nepal | Omani | Pakistan | Palestina | Qatar | Saudia | Singapuri | Sri Lanka | Syria | Tajikistan | Timor ya Mashariki | Turkmenistan | Ufilipino | Uhindi | Urusi1 | Uthai | Uturuki1 | Uzbekistan | Vietnam | Yemen | Yordani

1. Nchi ina maeneo katika Asia na Ulaya. 2. Nchi iko Asia lakini inahesabiwa pia kati ya nchi za Ulaya kwa sababu za historia au utamaduni. 3. Eneo la pekee la China.