Bangladesh

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Bangladesh
Bendera
Nembo
Mji mkuu (na mkubwa zaidi){{{mji_mkuu}}}
23°42′ N 90°22′ E
Lugha rasmi{{{lugha_rasmi}}}
Serikali{{{serikali}}}
{{{vyeo_viongozi}}}{{{majina_viongozi}}}
{{{muundo_uhuru}}}{{{tarehe_uhuru}}}
Eneo
 • Eneo la jumla{{{eneo_jumla}}}
 • Maji (%){{{maji}}}
Idadi ya watu
 • Kadirio la 2023{{{watu_kadirio}}}
Pato la TaifaKadirio la 2023
 • Jumla{{{pato}}}
 • Kwa kila mtu{{{pato_kwa_mtu}}}
Pato Halisi la TaifaKadirio la 2023
 • Jumla{{{pato_halisi}}}
 • Kwa kila mtu{{{pato_halisi_kwa_mtu}}}
Maendeleo ({{{mwaka_maendeleo}}}){{{maendeleo}}}
Fedha{{{fedha}}}
Majira ya saa{{{majira_saa}}}
Muundo wa tareheDD/MM/YYYY

Bangladesh (pia: Bangla Desh; kwa Kibengali: বাংলাদেশ, bāṃlādeś) ni nchi ya Asia ya Kusini.

Imepakana na Uhindi pande zote barani isipokuwa mpaka mfupi wa km 193 na Myanmar upande wa kusini-mashariki na pwani ya Ghuba ya Bengali.

Jiografia[hariri | hariri chanzo]

Sehemu kubwa ya nchi ni delta ya mito Ganga na Brahmaputra.

Uso wa nchi ni tambarare na mita chache tu juu ya uwiano wa bahari. Hivyo wananchi huteswa mara nyingi na mafuriko makali.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Bangladesh ni sehemu ya mashariki ya Bengali ya kihistoria ambayo ilikuwa ndani ya Uhindi wa Kiingereza hadi 1947.

Mwaka 1857 Wahindi walipinga utawala wa Kampuni ya Kiingereza kwa Uhindi wa Mashariki. Matokeo yake utawala ulishikwa na serikali yenyewe ya Uingereza kama koloni (1858).

Mwisho wa karne ya 19 harakati za Wahindi kutafuta uhuru zilianza upya. Mwaka 1885 chama cha INC (Indian National Congress) kiliundwa na Wahindu na Waislamu pamoja waliodai uhuru.

Mwaka 1906 viongozi Waislamu walitoka katika INC na kuunda "Shirikisho la Waislamu".

Mwaka 1917 Uingereza ulitamka ya kwamba ulitaka kuelekea polepole hali ya kujitawala kwa Wahindi. Viongozi wa wenyeji hawakuridhika na mkasi wa mabadiliko. Chini ya uongozi wa Mahatma Ghandi mwendo wa kupigania uhuru bila mabavu ulipata nguvu. Ghandi alipigania hasa umoja wa Wahindu na Waislamu lakini alipingwa na viongozi wenye itikadi kali wa pande zote mbili.

Baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia Waingereza walikubali kujiondoa katika Uhindi. Swali kubwa lilikuwa kama nchi itabaki kama nchi moja au kama maeneo ya Waislamu yatajitenga.

Tarehe 14/15 Agosti 1947 utawala wa Uingereza ulikwisha. Bara Hindi iligawanywa katika nchi mbili za Uhindi na Pakistan. Mgawanyo wa Uhindi ulikuja na vita na kumwaga kwa damu nyingi. Bengali yenyewe iligawanyika kwa sababu wakazi wengi wa mashariki walikuwa Waislamu, tofauti na Wabengali wengine waliokuwa Wahindu.

Tarehe 30 Januari 1948 Ghandi mwenyewe aliuawa na Hindu mkali aliyemchukia kwa sababu alitaka usawa wa Waislamu na Wahindu.

Wakati ule Bengali ya mashariki ilikuwa nchi moja pamoja na Pakistan ya leo, bila kujali umbali mkubwa kati ya pande hizo mbili zilizounganishwa na dini.

Iliitwa "Pakistan ya Mashariki" mpaka mwaka 1971 ilipojitenga na Pakistan kwa msaada wa India katika Vita vya Uhuru vya Bangla Desh.

Watu[hariri | hariri chanzo]

Kati ya nchi kubwa, Bangladesh inaongoza kwa msongamano wa watu. Uzazi umepunguzwa sana na kampeni za udhibiti wake zilizofanywa miaka ya mwisho.

Wabengali ni asilimia 98 za wakazi, lakini kuna pia makabila madogo 11.

Asilimia hizohizo wanaongea Kibengali, ambacho ndicho lugha rasmi. Kiingereza pia kinatumika sana.

Upande wa dini, Waislamu ni asilimia 86-90 (wengi wakiwa Wasuni), Wahindu ni asilimia 8-12, Wabuddha ni asilimia 0.6 na Wakristo (hasa Wakatoliki, halafu Waprotestanti) asilimia 0.4.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Baxter, C (1997). Bangladesh, from a Nation to a State. Westview Press. ISBN 0-8133-3632-5. OCLC 47885632. 
  • Iftekhar Iqbal (2010) The Bengal Delta: Ecology, State and Social Change, 1840–1943, Cambridge Imperial and Post-Colonial Studies, Palgrave Macmillan, Pages: 288, ISBN 0230231837
  • M. Mufakharul Islam (edited) (2004) Socio-Economic History of Bangladesh: essays in memory of Professor Shafiqur Rahman, 1st Edition, Asiatic Society of Bangladesh, Kigezo:Oclc
  • M. Mufakharul Islam (2007), Bengal Agriculture 1920–1946: A Quantitative Study, Cambridge South Asian Studies, Cambridge University Press, Pages: 300, ISBN 0521049857
  • Meghna Guhathakurta & Willem van Schendel (Edited) (2013) The Bangladesh Reader: History, Culture, Politics (The World Readers), Duke University Press Books, Pages: 568, ISBN 0822353040
  • Sirajul Islam (edited) (1997) History of Bangladesh 1704–1971(Three Volumes: Vol 1: Political History, Vol 2: Economic History Vol 3: Social and Cultural History), 2nd Edition (Revised New Edition), The Asiatic Society of Bangladesh, Pages: 1846, ISBN 9845123376
  • Sirajul Islam (Chief Editor) (2003) Banglapedia: A National Encyclopedia of Bangladesh.(10 Vols. Set), (written by 1300 scholars & 22 editors) The Asiatic Society of Bangladesh, Pages: 4840, ISBN 9843205855
  • Srinath Raghavan (2013) ‘1971: A Global History of the Creation of Bangladesh’, Harvard University Press, Pages: 368, ISBN 0674728645

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Nchi na maeneo ya Asia

Afghanistan | Armenia2 | Azerbaijan | Bahrain | Bangladesh | Bhutan | Brunei | China | Falme za Kiarabu | Georgia2 | Hong Kong3 | Indonesia | Iraq | Israel | Jamhuri ya China (Taiwan) | Japani | Kamboja | Kazakhstan | Kirgizia | Korea Kaskazini | Korea Kusini | Kupro2 | Kuwait | Laos | Lebanoni | Macau3 | Malaysia | Maldivi | Mongolia | Myanmar | Nepal | Omani | Pakistan | Palestina | Qatar | Saudia | Singapuri | Sri Lanka | Syria | Tajikistan | Timor ya Mashariki | Turkmenistan | Uajemi | Ufilipino | Uhindi | Urusi1 | Uthai | Uturuki1 | Uzbekistan | Vietnam | Yemen | Yordani

1. Nchi ina maeneo katika Asia na Ulaya. 2. Nchi iko Asia lakini inahesabiwa pia kati ya nchi za Ulaya kwa sababu za historia au utamaduni. 3. Eneo la pekee la China.


Makala hii kuhusu maeneo ya Asia bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Bangladesh kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.