Uthai

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ufalme wa Uthai
ราชอาณาจักรไทย
Ratcha Anachak Thai
Bendera ya Uthai Nembo ya Uthai
Bendera Nembo
Kaulimbiu ya taifa: {{{national_motto}}}
Wimbo wa taifa: Phleng Chat
Wimbo la kifalme: Phleng Sansoen Phra Barami
Lokeshen ya Uthai
Mji mkuu Bangkok (Krung Thep)
13°44′ N 100°30′ E
Mji mkubwa nchini Bangkok
Lugha rasmi Kithai
Serikali Ufalme wa kikatiba
Maha Vajiralongkorn
Srettha Thavisin
Formation
Sukhothai Mfalmedom
Ufalme wa Ayutthaya
Ufalme wa Thonburi
Ufalme wa Chakri

1238–1368
1350–1767
1767 hadi 7 Aprili 1782
7 Aprili 1782 hadi leo
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
513,120 km² (ya 51)
0.4
Idadi ya watu
 - Julai 2014 kadirio
 - 2010 sensa
 - Msongamano wa watu
 
67,091,1201 (ya 20)
64,785,909
132.1/km² (ya 882)
Fedha Baht (฿) (THB)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
(UTC+7)
(UTC+7)
Intaneti TLD .th
Kodi ya simu +66

-


Uthai (pia: Siam, Thailand, Tailandi, Thailandi, Tailendi) ni ufalme katika Asia ya Kusini-Mashariki.

Imepakana na Laos, Kambodia, Malaysia na Myanmar.

Ina pwani kwenye Ghuba ya Uthai ya Bahari ya Kusini ya China upande wa kusini na Bahari Hindi upande wa magharibi.

Nchi ina wakazi zaidi ya milioni 67, hivyo inashika nafasi ya 20 duniani.

Mji mkuu na mji mkubwa ni Bangkok (ukiwa na wakazi milioni 8).

Historia[hariri | hariri chanzo]

Uthai ilikuwa nchi pekee ya Asia Kusini Mashariki iliyofaulu kukwepa ukoloni.

Nchi iliitwa rasmi 'Siam (สยาม) hadi mwaka 1939, tena kati ya 1945 na 1949.

Neno Thai (ไทย) linamaanisha "uhuru" kwa Kithai ni pia jina la kundi kubwa la watu nchini ambao ni Wathai (75-85%), mbali na Wathai-Wachina (12%).

Tangu tarehe 19 Septemba 2006 nchi imetawaliwa na kamati ya jeshi. Jeshi ilipindua serikali ya waziri mkuu Thaksin Shinawatra bila kumwaga damu. Viongozi wa kijeshi walipatana na mfalme kwamba wataandaa uchaguzi mpya.

Lakini hata baada ya chaguzi huru kadhaa nchi haijatulia kisiasa.

Watu[hariri | hariri chanzo]

Nchini Uthai kuna lugha za asili 73 (angalia orodha ya lugha za Uthai). Kati yake, Kithai ndiyo lugha rasmi.

Wathai walio wengi (94.5%) hufuata dini ya Ubuddha katika madhehebu ya Theravada. Kusini, mpakani kwa Malaysia, kuna Waislamu (4.3%). Wakristo ni 1.2%.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Serikali
Taarifa za jumla
Utalii
  1. Thailand travel dictionary
Vingine
Nchi na maeneo ya Asia

Afghanistan | Armenia2 | Azerbaijan | Bahrain | Bangladesh | Bhutan | Brunei | China | Falme za Kiarabu | Georgia2 | Hong Kong3 | Indonesia | Iraq | Israel | Jamhuri ya China (Taiwan) | Japani | Kamboja | Kazakhstan | Kirgizia | Korea Kaskazini | Korea Kusini | Kupro2 | Kuwait | Laos | Lebanoni | Macau3 | Malaysia | Maldivi | Mongolia | Myanmar | Nepal | Omani | Pakistan | Palestina | Qatar | Saudia | Singapuri | Sri Lanka | Syria | Tajikistan | Timor ya Mashariki | Turkmenistan | Uajemi | Ufilipino | Uhindi | Urusi1 | Uthai | Uturuki1 | Uzbekistan | Vietnam | Yemen | Yordani

1. Nchi ina maeneo katika Asia na Ulaya. 2. Nchi iko Asia lakini inahesabiwa pia kati ya nchi za Ulaya kwa sababu za historia au utamaduni. 3. Eneo la pekee la China.


Makala hii kuhusu maeneo ya Asia bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Uthai kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.