Umoja

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Nembo ya Taifa la Tanzania ikihimiza Umoja hasa katika nchi hiyo

Umoja katika hisabati unahusu sifa maalumu za namba moja na za mambo yote yasiyo na wingi.

Kutokana na maana hiyo ya msingi, neno umoja linatumika katika fani mbalimbali, kuanzia dini, ambapo katika imani ya wengi (kama vile Wayahudi, Wakristo na Waislamu) umoja ni hasa sifa ya Mungu.

Katika Ukristo, imani katika umoja wa Mungu katika Nafsi tatu (Baba, Mwana na Roho Mtakatifu) ndio msingi wa umoja wa Kanisa pia kadiri ya Kanuni ya Imani ya Nisea-Konstantinopoli kwa njia ya ubatizo uleule mmoja ambao waamini wote wanatakiwa kuupokea.