Nenda kwa yaliyomo

Hong Kong

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mkoa Maalum wa Utawala wa Hong Kong
香港特別行政區 (Xianggang Tebie Xingzhengqu)
Wimbo wa taifa: "March of the Volunteers"

Wimbo wa Kujitolea (Wimbo wa Taifa la China)
Mahali pa Hong Kong
Miji mikuuHakuna rasmi (Makao makuu ya serikali yako Tamar, Admiralty)
Mji mkubwaHong Kong
Lugha rasmiKichina (Kikantoni) na Kiingereza
 • Mkuu wa Mtendaji
John Lee
Uhuru kutoka Uingereza
 • Makoloni ya Uingereza
26 Januari 1841
 • Kukabidhiwa kwa China
1 Julai 1997
Eneo
 • Jumlakm2 1,110.18 (ya 167)
 • Maji (asilimia)59.70%
Idadi ya watu
 • Kadirio la 20247,492,000
 • Msongamano6,801/km²/km2
PLT (PPP)Kadirio la 2024
 • Jumla $569.83 Bilioni [1]
 • Kwa kila mtu $75,410 [1]
PLT (Kawaida)Kadirio la 2024
 • Jumla $401.75 Bilioni [1] (ya 46)
 • Kwa kila mtu $53,160 [1]
HDI (2021) 0.952 (ya 4)
juu sana
Gini (2016)Ongezeko hasi 53.9
SarafuDola ya Hong Kong
Majira ya saaUTC+8 (HKT)
Upande wa magariKushoto
Msimbo wa simu+852
Jina la kikoa.hk
Hong Kong

Hong Kong (Kichina: 香港; pinyin: Xiānggǎng) ni Mkoa Maalum wa Utawala (SAR) wa China. Upo kusini mwa pwani ya nchi, kando ya Bahari ya Kusini ya China. Inajumuisha Kisiwa cha Hong Kong, Rasi ya Kowloon, na New Territories. Jiji la Hong Kong, lililopo kwenye Kisiwa cha Hong Kong, ndilo jiji kubwa na idadi ya watu katika mkoa. Hong Kong lina takriban milioni 7.5 katika eneo la kilomita za mraba 1,110

Hong Kong ilikuwa koloni la Uingereza katika pwani ya China kwa zaidi ya miaka 99. Hong Kong ilirudishwa kwa China kutoka Uingereza mnamo Julai 1, 1997, chini ya makubaliano ya "nchi moja, mifumo miwili," ikiruhusu Hong Kong kudumisha uhuru wake wa kisiasa na kiuchumi kwa miaka 50. Hata hivyo, kwa muda, China imeongeza udhibiti wake, hasa kupitia maandamano ya kupinga muswada wa kukabidhi wahalifu wa 2019 na Sheria ya Usalama ya Kitaifa ya 2020, ambayo ilipunguza uhuru na haki za Hong Kong.

Historia

[hariri | hariri chanzo]

Baada ya China kushindwa na Dola la Uingereza katika Vita vya kwanza vya Afyuni (1839-1842), Hong Kong ikawa koloni la Uingereza kuanzia Kisiwa cha Hong Kong, ikifuatiwa na Musoma ya Kowloon mwaka 1860 na mkataba wa miaka 99 kwa Majimbo Mapya katika 1898.

Baada ya kumilikiwa na Japan wakati wa Vita Kuu ya Pili (1941-1945), Waingereza waliiteka tena hadi Juni 30, 1997.

Kuelekea mwishoni mwa miaka ya 1970, Hong Kong ikawa imara kama mlango mkuu kati ya dunia nzima na China.

Kama matokeo ya mazungumzo kati ya China na Uingereza, Hong Kong ilirudishwa kwa Jamhuri ya Watu wa China chini ya Azimio la Pamoja la mwaka 1984. Mji ukawa wa kwanza kati ya Mikoa yenye utawala maalumu nchini China tarehe 1 Julai 1997 chini ya kanuni ya "nchi moja, mifumo miwili". Siku hiyo inaitwa 香港回歸 (xiāng gǎng huí guī), kwa Kiswahili "unganisho jipya la Hong Kong". Jina lingine ni 香港回歸祖國 (xiāng gǎng huí guī zǔ guó), kwa Kiswahili "Hong Kong kurudishwa kwa nchi mama".

Demografia

[hariri | hariri chanzo]
Kitovu cha Hong Kong wakati wa usiku

Hong Kong ni maalumu kwa ajili ya mandhari yake pana, bandari asili ya kina na msongamano wa watu (milioni saba na nusu juu ya nchi ya Km² 1108 (sq mi 428).

Asili/Kabila

[hariri | hariri chanzo]

Idadi ya sasa ya wakazi wa Hong Kong inajumuisha 92% ya Wachina asilia. Wengine ni Wafilipino (2.5%), Waindonesia (2.1%) n.k.

Sehemu kubwa ya wakazi wanazungumza Kichina cha Canton (Kikantoni), Hong Kong ikiwa jirani na jimbo la Guangdong, ambalo wafanyakazi wenye ujuzi walikimbia baada ya serikali ya Kikomunisti kuchukua China mwaka 1949 na baadaye husafishwa idadi ya watu mwaka 1960.

Upande wa dini, wengi hawana au wanafuata kidogo jadi, lakini kuna uhuru wa dini mkubwa. 56.1% hawana dini yoyote, Wabuddha na Watao ni 21.3%, Wakristo ni 12% (6.5% Waprotestanti na 5.1% Wakatoliki), Waislamu ni 4%.

Mji una maendeleo makubwa kabisa duniani kama kitovu cha biashara na kituo cha fedha, inachukuliwa kuwa mji katika dunia na mmoja wa Alpha + majiji nane.

Inashika nafasi ya tano katika 2014 Global Miji Index baada ya jiji la New York, London, Tokyo na Paris.

Mji wa kumi kwa kipato cha juu cha kila mwananchi katika dunia, lakini pia inaongozaongoza miongoni mwa nchi zenye uchumi mkubwa kwa kukosa usawa wa kipato cha wakazi.

Hong Kong ni ya tatu kama kituo cha biashara muhimu zaidi baada ya New York na London. Huduma uchumi, kwa kodi ya chini na biashara huria, imekuwa huru sana, na fedha yake, dola ya Hong Kong, ni ya 13 kutumika zaidi duniani.

Udogo wa eneo ulileta haja ya miundombinu mingi jirani, na mji ukawa katikati ya vielelezo vya usanifu wa kisasa upande wa majengo, na kuipa Hong Kong mandhari ya mji unaoelekea juu wima.

Hong Kong ina maendeleo makubwa hata upande wa usafiri wa umma duniani ukiwa na mtandao wa asilimia 90, kiwango cha juu zaidi duniani, na inategemea wingi wa watu kupita kwa njia ya barabara au reli.

Uchafuzi wa hewa bado ni mkubwa, viwango vya uzalishaji vikiwa tatizo. Hata hivyo wakazi wa Hong Kong wana matarajio ya kuishi kirefu kuliko watu wengine duniani.

Watalii huenda Hong Kong kwa mvuto wa utamaduni, chakula pamoja na sinema, muziki wa Wachina.

Ingawa Hong Kong ina watu wengi wa matabaka mbalimbali, chakula kwa kawaida huwa kimetokana na utamaduni wa Cantonese au Guangdong cuisine. Wali huliwa kwa wingi pamoja na kuku na mboga zilizotoka mashambani. Chakula huliwa mara tano kwa siku yaani: staftahi, chakula cha mchana, chai ya adhuhuri, chakula cha jioni na siu yeh ambacho ni chakula cha kuliwa kabla uende ukalale.

Mambo ya kuona Hong Kong ni kama vile Kisiwa cha Lantau ambapo kivutio kikubwa ni Giant Buddha, mchongo ulio mkubwa sana wa Buddha, The Peak ambapo utaona Victoria Harbour, Hong Kong Disney Land Resort na Ocean Park Theme.

Tazama pia

[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Serikali
Biashara
Nchi na maeneo ya Asia

Afghanistan | Armenia2 | Azerbaijan | Bahrain | Bangladesh | Bhutan | Brunei | China | Falme za Kiarabu | Georgia2 | Hong Kong3 | Indonesia | Iraq | Israel | Jamhuri ya China (Taiwan) | Japani | Kamboja | Kazakhstan | Kirgizia | Korea Kaskazini | Korea Kusini | Kupro2 | Kuwait | Laos | Lebanoni | Macau3 | Malaysia | Maldivi | Mongolia | Myanmar | Nepal | Omani | Pakistan | Palestina | Qatar | Saudia | Singapuri | Sri Lanka | Syria | Tajikistan | Timor ya Mashariki | Turkmenistan | Uajemi | Ufilipino | Uhindi | Urusi1 | Uthai | Uturuki1 | Uzbekistan | Vietnam | Yemen | Yordani

1. Nchi ina maeneo katika Asia na Ulaya. 2. Nchi iko Asia lakini inahesabiwa pia kati ya nchi za Ulaya kwa sababu za historia au utamaduni. 3. Eneo la pekee la China.


Makala hii kuhusu maeneo ya China bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Hong Kong kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
  1. 1.0 1.1 1.2 1.3 IMF. "Hong Kong GDP peofile" (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2025-02-20.