Guyana ya Kifaransa
Région Guyane Lagwiyann | |
---|---|
![]() |
![]() |
Jina la Kifaransa | Région Guyane (Kikrioli: Lagwiyann) |
Jina la kawaida | Guyana ya Kifaransa |
Mji Mkuu | Cayenne |
Eneo | 83,846 km² |
Mkuu wa Mkoa | Rodolphe Alexandre |
Idadi ya wakazi | 296,711 |
Sensa ya mwaka | 2019 |
Wakazi kwa km² | 3.2 |
Wilaya (arrondissements) | 2 |
Ramani | ![]() |
Guyana ya Kifaransa (kwa Kifaransa: Guyane française au La Guyane pekee, kwa Kikrioli cha Guyana Lagwiyann) ni eneo la ng'ambo la Ufaransa ("département d'outre-mer" au DOM) katika Amerika Kusini.
Imepakana na Brazil na Surinam.
Pwani ya Bahari ya Karibi (Atlantiki) iko upande wa kaskazini.
Ilikuwa koloni la Ufaransa; sasa imekuwa sehemu kamili ya Ufaransa kisiasa na kisheria. Wakazi ni raia wa Ufaransa. Eneo lina hali ya mkoa (departement) na pia kanda (region) katika Ufaransa. Hivyo Guyana ni sehemu ya Umoja wa Ulaya. Pesa yake ni Euro.
Makao makuu ya Guyana ni mji wa Cayenne.
Watu
Idadi ya wakazi imekadiriwa kuwa 296,711 katika mwaka 2019 na inaendelea kuongezeka kwa uzazi na uhamiaji.
Wakazi walio wengi ni wa asili ya Afrika au wa mchanganyiko wa Kiafrika-Kizungu (60-70%). Asilimia 14 ni Wazungu, hasa kutoka Ufaransa; wengine ni Waindio asilia (3-4%), Wachina (3-4%), Wahindi na wahamiaji wa hivi karibuni kutoka Laos (1-2%), Vietnam, Lebanoni n.k.
Lugha rasmi na ya kawaida ni Kifaransa.
Upande wa dini, wakazi walio wengi ni Wakristo wa Kanisa Katoliki (66.7%).
Tazama pia
Viungo vya nje
Nchi na maeneo ya Amerika Kusini |
Argentina | Bolivia | Brazil | Chile | Ekuador | Guyana | Guyana ya Kifaransa | Kolombia | Paraguay | Peru | Surinam | Uruguay | Venezuela |
![]() |
Makala hii kuhusu maeneo ya Amerika Kusini bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Guyana ya Kifaransa kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |