Guyana ya Kifaransa

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Région Guyane
Lagwiyann
Nembo
Jina la Kifaransa Région Guyane
(Kikrioli: Lagwiyann)
Jina la kawaida Guyana ya Kifaransa
Mji Mkuu Cayenne
Eneo 83,846 km²
Mkuu wa Mkoa Rodolphe Alexandre
Idadi ya wakazi 296,711
Sensa ya mwaka 2019
Wakazi kwa km² 3.2
Wilaya (arrondissements) 2
Ramani
-- Kwa nchi jirani angalia makala Guyana--

Guyana ya Kifaransa (kwa Kifaransa: Guyane française au La Guyane pekee, kwa Kikrioli cha Guyana Lagwiyann) ni eneo la ng'ambo la Ufaransa ("département d'outre-mer" au DOM) katika Amerika Kusini.

Imepakana na Brazil na Surinam.

Pwani ya Bahari ya Karibi (Atlantiki) iko upande wa kaskazini.

Ilikuwa koloni la Ufaransa; sasa imekuwa sehemu kamili ya Ufaransa kisiasa na kisheria. Wakazi ni raia wa Ufaransa. Eneo lina hali ya mkoa (departement) na pia kanda (region) katika Ufaransa. Hivyo Guyana ni sehemu ya Umoja wa Ulaya. Pesa yake ni Euro.

Makao makuu ya Guyana ni mji wa Cayenne.

Watu

Idadi ya wakazi imekadiriwa kuwa 296,711 katika mwaka 2019 na inaendelea kuongezeka kwa uzazi na uhamiaji.

Wakazi walio wengi ni wa asili ya Afrika au wa mchanganyiko wa Kiafrika-Kizungu (60-70%). Asilimia 14 ni Wazungu, hasa kutoka Ufaransa; wengine ni Waindio asilia (3-4%), Wachina (3-4%), Wahindi na wahamiaji wa hivi karibuni kutoka Laos (1-2%), Vietnam, Lebanoni n.k.

Lugha rasmi na ya kawaida ni Kifaransa.

Upande wa dini, wakazi walio wengi ni Wakristo wa Kanisa Katoliki (66.7%).

Tazama pia

Viungo vya nje

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Nchi na maeneo ya Amerika Kusini

Argentina | Bolivia | Brazil | Chile | Ekuador | Guyana | Guyana ya Kifaransa | Kolombia | Paraguay | Peru | Surinam | Uruguay | Venezuela

Makala hii kuhusu maeneo ya Amerika Kusini bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Guyana ya Kifaransa kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.