Euro

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ishara ya Euro.

Euro ni sarafu ya pamoja katika baadhi ya nchi za Ulaya. Wakazi wake 350,000,000 (2023) wanatumia kwa kawaida pesa hiyo. Watu wengine 210,000,000 wanatumia pesa zilizoungwa na euro, hasa barani Afrika.

Tangu mwaka 2002 nchi 13 za EU zilifuta sarafu ya kitaifa ili kutumia Euro tu. Siku hizi ni 20.

Euro moja imegawanyika katika senti 100.

Kuna benknoti za € 5 (kijivu), € 10 (nyekundu), € 20 (buluu), € 50 (machungwa), € 100 (kijani), € 200 (njano), € 500 (nyekundu).

Kuna sarafu za metali 8 za € 0,01, € 0,02, € 0,05, € 0,10, € 0,20, € 0,50, € 1, € 2.

Pesa ya karatasi inatolewa na benki kuu ya Ulaya na ni sawa kote.

Sarafu zinatolewa na nchi wanachama na zinatofautiana upande mmoja, lakini sarafu zote hutumika kote.

Ishara ya Euro[hariri | hariri chanzo]

Ishara ya Euro ni herufi ya Kigiriki epsilon (E) yenye mistari miwili ya kulala: .

Nchi wanachama wa Euro[hariri | hariri chanzo]

Ramani ya uenezi wa Euro.
  1. Austria
  2. Ubelgiji
  3. Ufini
  4. Ufaransa
  5. Ujerumani
  6. Ugiriki
  7. Ueire
  8. Italia
  9. Latvia
  10. Luxemburg
  11. Ureno
  12. Hispania
  13. Uholanzi
  14. Slovakia
  15. Slovenia
  16. Kupro
  17. Malta
  18. Estonia
  19. Lithuania
  20. Kroatia

Nchi 6 zifuatazo hutumia pia Euro kama pesa pekee bila kuwa sehemu za mapatano, ila 4 za kwanza kwa makubaliano maalumu, nyingine 2 kwa kujiamulia:

Pesa za nchi zifuatazo zimeungwa na Euro:

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu mambo ya uchumi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Euro kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.