Luxemburg

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Utemi mkubwa wa Luxemburg
Groussherzogtum Lëtzebuerg
Grand-Duché de Luxembourg
Großherzogtum Luxemburg
Bendera ya Luxemburg Nembo ya Luxemburg
Bendera Nembo
Kaulimbiu ya taifa: Kiluxemburg: Mir wëlle bleiwe wat mir sinn
(Kiingereza: "Tunataka kukaa jinsi tulivyo")
Wimbo wa taifa: Ons Hémécht
("Nchi yetu")
WImbo wa kifalme: De Wilhelmus 1
Lokeshen ya Luxemburg
Mji mkuu Luxemburg
49°36′ N 6°7′ E
Mji mkubwa nchini Luxemburg
Lugha rasmi Kifaransa, Kijerumani, Kiluxemburg
Serikali
Mtemi mkubwa
Waziri Mkuu
Utemi Mkubwa
Mtemi Mkubwa Henri
Luc Frieden
Uhuru
Ilitangazwa
Ilithebitishwa
1815
1839
1867
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
2,586 km² (ya 167)
--
Idadi ya watu
 - 2019 kadirio
 - 2001 sensa
 - Msongamano wa watu
 
613 894 (ya 164)
439,539
233.7/km² (ya 58)
Fedha Euro ()2 (EUR)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
CET (UTC+1)
CEST (UTC+2)
Intaneti TLD .lu3
Kodi ya simu +352

-


Ramani ya Luxemburg.

Luxemburg (pia: Lasembagi) ni nchi ndogo katika Ulaya. Imepakana na Ubelgiji, Ufaransa na Ujerumani.

Ni nchi mwanachama wa Umoja wa Ulaya, tena ilikuwa kati ya nchi sita zilizoanzisha Jumuiya ya Kiuchumi ya Ulaya mwaka 1957.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Luxemburg kama nchi ndogo ilikuwa mara nyingi chini ya athira ya majirani wakubwa waliotawala juu yake kwa vipindi mbalimbali.

Kwa vipindi vingi vya historia yake Luxemburg ilikuwa sehemu ya Ujerumani.

Katika karne ya 14 watemi wa Luxemburg walichaguliwa kuwa wafalme wa Ujerumani.

Baada ya vita za Napoleoni, Ufaransa na Prussia zilivutana juu ya Luxemburg. Walipatana kwenye Mkutano wa Vienna (1815) ya kurudisha Luxemburg kama nchi ya pekee itakayotawaliwa na Mtemi Mkubwa. Mfalme wa Uholanzi alikuwa mtemi wa Luxemburg na nchi yenyewe iliungwa katika Shirikisho la Ujerumani.

Baada ya mwisho wa Shirikisho la Ujerumani (1866) Luxemburg haikujiunga (1870) na Dola jipya la Ujerumani.

Badiliko la familia ya kifalme katika Uholanzi lilisababisha uchaguzi wa mtemi wa pekee (1890).

Watu[hariri | hariri chanzo]

Ina wakazi 613,894 (Januari 2019) katika eneo la km² 2,586 pekee. Kati yao 49.1% ni wahamiaji kutoka Ureno (18.2% za wakazi wote), Ufaransa (13.5%), Ujerumani (10.3%), Italia (3.4%), Ubelgiji (3.3%), na nchi nyingine.

Lugha ya taifa ni Kiluxemburg ambayo ni lahaja ya Kijerumani yenye athira nyingi za Kifaransa. Karibu wakazi wote huweza kuongea lugha hizo zote tatu na Kiingereza, lakini zaidi Kifaransa.

Upande wa dini, 68.7% wanajitambulisha kama Wakatoliki na 3.7% wanajitambulisha kama Wakristo wa madhehebu mengine. Waislamu ni 2.3%. Wasio na dini ni 26.8%.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:


Nchi za Umoja wa Ulaya Bendera ya Umoja wa Ulaya
Austria | Bulgaria | Eire | Estonia | Hispania | Hungaria | Italia | Kroatia | Kupro | Latvia | Lituanya | Luxemburg | Malta | Polandi | Slovakia | Slovenia | Romania | Ubelgiji | Ucheki | Udeni | Ufaransa | Ufini | Ugiriki | Uholanzi | Ujerumani | Ureno | Uswidi
Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Luxemburg kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.