Nenda kwa yaliyomo

Luxemburg

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Luxemburg
Groussherzogtum Lëtzebuerg (lb)
Grand-Duché de Luxembourg (fr)
Großherzogtum Luxemburg (de)
Kaulimbiu: "Mir wëlle bleiwe wat mir sinn" (Kiluxemburg kwa "Tunataka kubaki jinsi tulivyo")
Wimbo wa taifa: "Ons Heemecht"
Eneo la Luxemburg
Mji mkuu
na mkubwa
Luxemburg
Lugha rasmiKifaransa, Kijerumani, Kiluxemburg
Kabila (2025)
Dini (2021)53% Ukristo
38% Wasio na dini
SerikaliUkuu wa kikatiba
  Mtemi mkuu
Wiliamu V wa Luxemburg
  Waziri Mkuu
Luc Frieden
Uhuru kutoka Uholanzi
  Kutoka Himaya ya Ufaransa na kupandishwa hadhi kuwa Utemi Mkuu wa Luxemburg
9 Juni 1815
  Uhuru kutoka Uholanzi
19 Aprili 1839
  Katiba ya kwanza
17 Oktoba 1868
  Katiba ya sasa
1 Julai 2023
Eneo
  Jumlakm2 2,586.4 (ya ya 167)
  Maji (asilimia)0.6%
Idadi ya watu
  Kadirio la 2025681,973 [1]
  Msongamano264/km2
PLT (PPP)Kadirio la 2024
  Jumla $112.2 bilioni [1] (ya 103)
  Kwa kila mtu $177,900 [1](ya 1)
PLT (Kawaida)Kadirio la 2024
  Jumla $98.6 bilioni [1]
  Kwa kila mtu $156,400 [1]
HDI (2022) 0.926
juu sana
SarafuEuro (€) EUR
Majira ya saaUTC+1 CET
Upande wa magariKulia
Msimbo wa simu+352
Jina la kikoa.lu
Ramani ya Luxemburg.

Luxemburg (pia Lusembagi, jina rasmi: Utemi Mkuu wa Luxemburg, ni nchi ndogo katika Ulaya ya Magharibi, inayopakana na Ubelgiji kaskazini na magharibi, Ufaransa kusini, na Ujerumani mashariki. Ina idadi ya watu takriban 681,973 [1], ikiwa ya 163 duniani. Jiji lake kubwa zaidi ni Luxemburg, ambalo pia ni mji mkuu. Luxemburg imegawanyika katika majimbo 3—Diekirch, Grevenmacher, na Luxemburg. Inajulikana kwa kuwa moja ya nchi tajiri zaidi duniani,

Historia

[hariri | hariri chanzo]

Luxemburg kama nchi ndogo ilikuwa mara nyingi chini ya athira ya majirani wakubwa waliotawala juu yake kwa vipindi mbalimbali.

Kwa vipindi vingi vya historia yake Luxemburg ilikuwa sehemu ya Ujerumani.

Katika karne ya 14 watemi wa Luxemburg walichaguliwa kuwa wafalme wa Ujerumani.

Baada ya vita za Napoleoni, Ufaransa na Prussia zilivutana juu ya Luxemburg. Walipatana kwenye Mkutano wa Vienna (1815) ya kurudisha Luxemburg kama nchi ya pekee itakayotawaliwa na Mtemi Mkubwa. Mfalme wa Uholanzi alikuwa mtemi wa Luxemburg na nchi yenyewe iliungwa katika Shirikisho la Ujerumani.

Baada ya mwisho wa Shirikisho la Ujerumani (1866) Luxemburg haikujiunga (1870) na Dola jipya la Ujerumani.

Badiliko la familia ya kifalme katika Uholanzi lilisababisha uchaguzi wa mtemi wa pekee (1890).

Demografia

[hariri | hariri chanzo]

Ina wakazi 681,973 (Januari 2025) katika eneo la km² 2,586 pekee.

Kati yao 47% ni wahamiaji kutoka Ureno (13.2% za wakazi wote), Ufaransa (7.2%), Italia (3.7%), na nchi nyingine.

Lugha ya taifa ni Kiluxemburg ambayo ni lahaja ya Kijerumani yenye athira nyingi za Kifaransa. Karibu wakazi wote huweza kuongea lugha hizo zote tatu na Kiingereza, lakini zaidi Kifaransa.

Upande wa dini, 46% wanajitambulisha kama Wakatoliki na 7% wanajitambulisha kama Wakristo wa madhehebu mengine. Waislamu ni 2.3%. Wasio na dini ni 38%.

Tazama pia

[hariri | hariri chanzo]
  • Kreins, Jean-Marie (2003). Histoire du Luxembourg (kwa French) (tol. la 3rd). Paris: Presses Universitaires de France. ISBN 978-2-13-053852-3.{{cite book}}: CS1 maint: unrecognized language (link)
  • Thewes, Guy (Julai 2003). Les gouvernements du Grand-Duché de Luxembourg depuis 1848 (PDF) (kwa French) (tol. la Édition limitée). Luxembourg City: Service Information et Presse. ISBN 2-87999-118-8. Iliwekwa mnamo 10 Julai 2007.{{cite book}}: CS1 maint: date auto-translated (link) CS1 maint: unrecognized language (link)

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:


Nchi za Umoja wa Ulaya Bendera ya Umoja wa Ulaya
Austria | Bulgaria | Eire | Estonia | Hispania | Hungaria | Italia | Kroatia | Kupro | Latvia | Lituanya | Luxemburg | Malta | Polandi | Slovakia | Slovenia | Romania | Ubelgiji | Ucheki | Udeni | Ufaransa | Ufini | Ugiriki | Uholanzi | Ujerumani | Ureno | Uswidi
Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Luxemburg kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
  1. 1 2 3 4 5 6 "Luxembourg GDP". 2024. Hitilafu ya kutaja: Invalid <ref> tag; name "auto1" defined multiple times with different content