Kijerumani
Kijerumani (pia: Kidachi, kwa Kijerumani: Deutsch au (die) deutsche Sprache) ni lugha ya Kigermanik ya magharibi katika jamii ya lugha za Kihindi-Kiulaya.
Huzungumzwa hasa katika nchi za Ujerumani, Austria, Uswisi, Liechtenstein na Luxemburg.
Kuna pia wasemaji asilia katika nchi jirani za Ujerumani / Austria kama Ubelgiji, Uholanzi, Ufaransa, Denmark, Poland na Italia ya kaskazini. Nchi nyingi za Ulaya ya Mashariki zilikuwa na wasemaji wa Kijerumani lakini wengi walifukuzwa au kuondoka wakati wa vita kuu ya pili ya dunia; vikundi vimebaki hasa katika Hungaria, Romania, Uceki, Urusi na Kazakhstan.
Vikundi vidogo vya watu waliohamia katika karne za 19 na 20 wanaoendelea kutumia Kijerumani wako katika Amerika ya Kaskazini (Marekani, Kanada), Amerika Kusini (Brazil, Chile) na Afrika (hasa Namibia na Afrika Kusini).
Kijerumani huzungumzwa na watu milioni 100 katika Ulaya. Ni lugha ya pili katika Ulaya baada ya Kirusi kushinda Kifaransa na Kiingereza.
Kijerumani kama lugha ya kitaifa[hariri | hariri chanzo]
Kijerumani kinatumiwa kama lugha rasmi kitaifa katika nchi zifuatazo:
- Ujerumani
- Austria
- Liechtenstein
- Uswisi (pamoja na Kifaransa, Kiitalia na Kirumanj)
- Luxemburg (pamoja na Kiluxemburg na Kifaransa )
- Ubelgiji (pamoja na Kifaransa na Kiholanzi lugha rasmi ya kitaifa, katika wilaya za Eupen na Sankt Vith ni lugha rasmi ya utawala pamoja na Kifaransa)
- Namibia (Kijerumani ni kati ya lugha 20 zinazotambuliwa kuwa lugha za kitaifa; ilikuwa lugha rasmi ya kitaifa pamoja Kiingereza na Kiafrikaans hadi 1990)
Lugha rasmi kieneo[hariri | hariri chanzo]
Kijerumani kinatumiwa kama lugha rasmi ya utawala kieneo (ama kimkoa au kwenye ngazi ya miji / tarafa tu) katika nchi zifuatazo:
- Italia (katika wilaya ya Bolzano ya Italia kaskazini pamoja na Kiitalia)
- Hungaria (lugha rasmi kieneo mjini Ödenburg / Sopron baada ya Kihungaria)
- Rumania (lugha rasmi kieneo pamoja na Kiromania)
- Urusi (lugha ya utawala kieneo kwenye wilaya za tabia ya kitaifa Asowo na Halbstadt katika Siberia ya magharibi)
Umoja wa Ulaya[hariri | hariri chanzo]
Kijerumani ni kati ya lugha rasmi za Umoja wa Ulaya pamoja na Kiingereza na Kifaransa. Kati ya lugha ndani ya Umoja ni lugha yenye wasemaji wengi kushinda nyingine zote.
Maneno machache[hariri | hariri chanzo]
hujambo? – sijambo | Wie geht es dir? – Mir geht es gut. |
jambo | Hallo! |
ndiyo | ja |
hapana | nein |
mgeni | Gast, Fremder |
rafiki | Freund |
karibu | Willkommen! |
kwa heri | Auf Wiedersehen! |
asante | Danke! |
asante sana | Vielen Dank! |
safari | Reise |
ninakupenda | Ich liebe dich. |
hatari | Gefahr |
daktari | Doktor |
polepole | langsam |
Afya! (wakati wa kunywa na mwingine) | Prost! |
kijiji | Dorf |
mji | Stadt |
Lugha inayofundishwa[hariri | hariri chanzo]
Kijerumani kama lugha ya kigeni kinafundishwa shuleni au kwenye taasisi za elimu ya watu wazima katika nchi nyingi. Mwaka 2004 idadi ya wanafunzi wa Kijerumani ilikuwa kama ifuatayo:
- Urusi: 4.657.500 (3,26%)
- Poland: 2.202.708 (5,70 %)
- Ufaransa: 1.603.813 (2,52 %)
- Ucheki: 799.071 (7,80 %)
- Ukraine: 629.742
- Hungaria: 629.472
- Kazakhstan: 629.874
- Uholanzi: 591.190
- Marekani: 551.274
Kijerumani ni lugha ya pili katika mtandao (intaneti) baada ya Kiingereza. Takriban nusu ya kurasa zote mtandaoni ni za Kiingereza, lakini Kijerumani kinafuata kikiwa na 8% za kurasa zote.
Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]
- makala za OLAC kuhusu Kijerumani
- lugha ya Kijerumani katika Glottolog
- (en) Muhtasari kuhusu Kijerumani kwenye Ethnologue
- Kamusi Archived 11 Februari 2010 at the Wayback Machine.
- Kozi
- xLingua-Kamusi Kijerumani-Kiswahili / Kiswahili-Kijerumani Archived 21 Agosti 2011 at the Wayback Machine.