Lituanya

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Lituanya


Lituanya (au Lituania) ni nchi huru iliyoko Kaskazini Mashariki mwa Ulaya. Inajulikana rasmi kama Jamhuri ya Lituania.

Inapakana na Latvia, Belarus, Polandi na Russia.

Ni mwanachama wa Umoja wa Ulaya.

Mji mkuu wa Lituania ni Vilnius.

Jiografia[hariri | hariri chanzo]

Lituanya iko kwenye mwambao wa Bahari ya Baltiki.

Miji mikubwa[hariri | hariri chanzo]

Vilnius

Historia[hariri | hariri chanzo]

Lituania kuanzia karne ya 13 ilikuwa nchi huru na imara iliyoteka maeneo mengi; kufikia karne ya 15, ikiwa pamoja na Polandi, ilikuwa kubwa kuliko nchi zote za Ulaya.

Mwaka 1795 nchi hizo mbili zilifutwa, na Lituania ikawa sehemu ya Dola la Urusi.

Mwaka 1918, ikawa tena nchi huru, lakini mwaka 1940 Warusi waliiteka tena.

Miaka 1940 - 1990 nchi ilikuwa jamhuri mwanachama wa Umoja wa Kisovyeti.

Baada ya umoja huo wa majimbo 15 kusambaratika, Lituania ilijitangaza nchi huru.

Lituania imekuwa nchi mwanachama ya Umoja wa Ulaya tangu tarehe 1 Mei 2004.

Wakazi[hariri | hariri chanzo]

Wananchi kwa asilimia 84 wanaongea Kilituania ambacho pamoja na Kilatvia ndizo lugha hai pekee za jamii ya lugha za Kibaltiki kati ya lugha za Kihindi-Kiulaya. Ndiyo lugha rasmi.

Mbali na Walituania asili (86.7%), kuna Wapolandi (5.6%), Warusi (4.8%) na wengineo.

Dini ya wananchi ni Ukristo wa Kanisa Katoliki (77.2%), mbali ya Waorthodoksi (4.9%) na Waprotestanti (0.8%). Wasio na dini yoyote ni 6.1%.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:


Serikali
Taarifa za jumla
Safari


Nchi za Umoja wa Ulaya Bendera ya Umoja wa Ulaya
Austria | Bulgaria | Eire | Estonia | Hispania | Hungaria | Italia | Kroatia | Kupro | Latvia | Lituanya | Luxemburg | Malta | Polandi | Slovakia | Slovenia | Romania | Ubelgiji | Ucheki | Udeni | Ufaransa | Ufini | Ugiriki | Uholanzi | Ujerumani | Ureno | Uswidi
Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Lituanya kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.