Nenda kwa yaliyomo

Georgia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Georgia (nchi))
Georgia
საქართველო (Kigeorgia)
Kaulimbiu: ძალა ერთობაშია
"Nguvu ni Umoja"
Wimbo wa taifa: Tavisupleba ("Uhuru")
Eneo la Georgia katika ramani ya Dunia
Mji mkuu
na mkubwa
Tbilisi
Lugha rasmiKigeorgia (pia Kiabkhazi katika Abkhazia)
Kabila
  • 86.8% Wajojia
  • 6.2% Wazerbaijani
  • 4.5% Waarmenia
  • 0.7% Warusi
  • 2.1% Wengine
 • Rais
Salome Zourabichvili
 • Waziri Mkuu
Irakli Kobachidze
Historia
 • Ufalme wa Kolkhis na Iberia
mnamo 2000 KK
 • Ufalme wa Georgia
1008
 • Jamhuri ya Kwanza
26 Mei 1918
 • Uhuru kutoka Umoja wa Kisovyeti
9 Aprili 1991
Eneo
 • Jumlakm2 69,420 (ya ya 120)
Idadi ya watu
 • Kadirio la 20173,718,200
 • Msongamano53.5/km2
PLT (PPP)Kadirio la
 • Jumla$35.91 bilioni
 • Kwa kila mtu$3,400
HDI (2022)0.814 juu sana
SarafuGEL
Majira ya saaUTCMoscow Time (MSK)
Msimbo wa simu++995
Jina la kikoa.ge

Georgia ni nchi iliyoko kati ya Ulaya ya Mashariki na Asia ya Magharibi. Ni sehemu ya eneo la Kaukazi, ikipakana na Bahari Nyeusi upande wa magharibi, Urusi upande wa kaskazini na kaskazini-mashariki, Uturuki upande wa kusini-magharibi, Armenia upande wa kusini, na Azerbaijan upande wa kusini-mashariki.

Georgia inachukua eneo la kilomita za mraba 69,700 (maili za mraba 26,900). Ina idadi ya watu milioni 3.7, ambapo zaidi ya theluthi moja wanaishi katika mji mkuu na mji mkubwa zaidi, Tbilisi. Wenyeji wa Georgia, ambao ni asili ya eneo hilo, wanaunda sehemu kubwa ya idadi ya watu wa nchi hiyo na ndio taifa kuu.

Jiografia

[hariri | hariri chanzo]

Georgia ni nchi ya milima inayofikia kimo cha mita 5,068. Kati ya safu mbili za milima kuna tambarare ya Kolkhis.

Upande wa magharibi unafaidika zaidi na Bahari Nyeusi, hivyo una hali ya hewa safi na mvua nyingi inayofaa kwa kilimo hasa cha mizabibu.

Historia

[hariri | hariri chanzo]

Georgia ilikuwa sehemu ya Umoja wa Kisovyeti lakini imekuwa nchi huru tangu 1991.

Maeneo ya Abkhazia na Ossetia ya Kusini yamedai uhuru pia na kwa sasa hayapo chini ya serikali kuu, lakini hayatambuliki kimataifa.

Utamaduni

[hariri | hariri chanzo]

Wakazi walio wengi (71%) huzungumza lugha ya Kigeorgia lakini kuna vikundi vya wazungumzaji wa Kirusi (9%), Kiarmenia (7%), Kiazeri (6%) na lugha nyingine.

Wageorgia wengi ni Wakristo wanaofuata Kanisa la Kiorthodoksi la Georgia (83.9%). Kuna pia wafuasi wa Kanisa la Kitume la Armenia (3.9%) na Wakatoliki (0.8%). Waislamu ni 9.9%, wakati Wayahudi wanazidi kuhama.

Watu maarufu

[hariri | hariri chanzo]

Mgeorgia anayejulikana zaidi duniani alikuwa Josef Stalin, mtawala wa Urusi wakati wa Ukomunisti.

Tazama pia

[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Serikali
Taarifa za jumla
News media
Nchi na maeneo ya Asia

Afghanistan | Armenia2 | Azerbaijan | Bahrain | Bangladesh | Bhutan | Brunei | China | Falme za Kiarabu | Georgia2 | Hong Kong3 | Indonesia | Iran | Iraq | Israel | Jamhuri ya China (Taiwan) | Japani | Kamboja | Kazakhstan | Kirgizia | Korea Kaskazini | Korea Kusini | Kupro2 | Kuwait | Laos | Lebanoni | Macau3 | Malaysia | Maldivi | Mongolia | Myanmar | Nepal | Omani | Pakistan | Palestina | Qatar | Saudia | Singapuri | Sri Lanka | Syria | Tajikistan | Timor ya Mashariki | Turkmenistan | Ufilipino | Uhindi | Urusi1 | Uthai | Uturuki1 | Uzbekistan | Vietnam | Yemen | Yordani

1. Nchi ina maeneo katika Asia na Ulaya. 2. Nchi iko Asia lakini inahesabiwa pia kati ya nchi za Ulaya kwa sababu za historia au utamaduni. 3. Eneo la pekee la China.


Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Georgia kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Makala hii kuhusu maeneo ya Asia bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Georgia kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.