Georgia
Georgia საქართველო (Kigeorgia) | |
---|---|
Kaulimbiu: ძალა ერთობაშია "Nguvu ni Umoja" | |
Wimbo wa taifa: Tavisupleba ("Uhuru") | |
Mji mkuu na mkubwa | Tbilisi |
Lugha rasmi | Kigeorgia (pia Kiabkhazi katika Abkhazia) |
Kabila |
|
• Rais | Salome Zourabichvili |
• Waziri Mkuu | Irakli Kobachidze |
Historia | |
• Ufalme wa Kolkhis na Iberia | mnamo 2000 KK |
• Ufalme wa Georgia | 1008 |
• Jamhuri ya Kwanza | 26 Mei 1918 |
• Uhuru kutoka Umoja wa Kisovyeti | 9 Aprili 1991 |
Eneo | |
• Jumla | km2 69,420 (ya ya 120) |
Idadi ya watu | |
• Kadirio la 2017 | 3,718,200 |
• Msongamano | 53.5/km2 |
PLT (PPP) | Kadirio la |
• Jumla | $35.91 bilioni |
• Kwa kila mtu | $3,400 |
HDI (2022) | 0.814 juu sana |
Sarafu | GEL |
Majira ya saa | UTCMoscow Time (MSK) |
Msimbo wa simu | ++995 |
Jina la kikoa | .ge |
Georgia ni nchi iliyoko kati ya Ulaya ya Mashariki na Asia ya Magharibi. Ni sehemu ya eneo la Kaukazi, ikipakana na Bahari Nyeusi upande wa magharibi, Urusi upande wa kaskazini na kaskazini-mashariki, Uturuki upande wa kusini-magharibi, Armenia upande wa kusini, na Azerbaijan upande wa kusini-mashariki.
Georgia inachukua eneo la kilomita za mraba 69,700 (maili za mraba 26,900). Ina idadi ya watu milioni 3.7, ambapo zaidi ya theluthi moja wanaishi katika mji mkuu na mji mkubwa zaidi, Tbilisi. Wenyeji wa Georgia, ambao ni asili ya eneo hilo, wanaunda sehemu kubwa ya idadi ya watu wa nchi hiyo na ndio taifa kuu.
Jiografia
[hariri | hariri chanzo]Georgia ni nchi ya milima inayofikia kimo cha mita 5,068. Kati ya safu mbili za milima kuna tambarare ya Kolkhis.
Upande wa magharibi unafaidika zaidi na Bahari Nyeusi, hivyo una hali ya hewa safi na mvua nyingi inayofaa kwa kilimo hasa cha mizabibu.
Historia
[hariri | hariri chanzo]Georgia ilikuwa sehemu ya Umoja wa Kisovyeti lakini imekuwa nchi huru tangu 1991.
Maeneo ya Abkhazia na Ossetia ya Kusini yamedai uhuru pia na kwa sasa hayapo chini ya serikali kuu, lakini hayatambuliki kimataifa.
Utamaduni
[hariri | hariri chanzo]Wakazi walio wengi (71%) huzungumza lugha ya Kigeorgia lakini kuna vikundi vya wazungumzaji wa Kirusi (9%), Kiarmenia (7%), Kiazeri (6%) na lugha nyingine.
Wageorgia wengi ni Wakristo wanaofuata Kanisa la Kiorthodoksi la Georgia (83.9%). Kuna pia wafuasi wa Kanisa la Kitume la Armenia (3.9%) na Wakatoliki (0.8%). Waislamu ni 9.9%, wakati Wayahudi wanazidi kuhama.
Watu maarufu
[hariri | hariri chanzo]Mgeorgia anayejulikana zaidi duniani alikuwa Josef Stalin, mtawala wa Urusi wakati wa Ukomunisti.
Tazama pia
[hariri | hariri chanzo]Tanbihi
[hariri | hariri chanzo]Viungo vya nje
[hariri | hariri chanzo]- Serikali
- President of Georgia Ilihifadhiwa 7 Aprili 2013 kwenye Wayback Machine.
- Government of Georgia Ilihifadhiwa 27 Aprili 2011 kwenye Wayback Machine.
- Ministry of Foreign Affairs of Georgia Ilihifadhiwa 4 Mei 2011 kwenye Wayback Machine.
- Department of Tourism and Resorts Ilihifadhiwa 5 Januari 2009 kwenye Wayback Machine.
- American Chamber of Commerce in Georgia
- Chief of State and Cabinet Members Ilihifadhiwa 24 Juni 2013 kwenye Wayback Machine.
- Taarifa za jumla
- Georgia entry at The World Factbook
- Georgia Ilihifadhiwa 7 Juni 2008 kwenye Wayback Machine. at UCB Libraries GovPubs
- Georgia katika Open Directory Project
- Georgia profile from the BBC News
- Wikimedia Atlas of Georgia
- Association of Modern Scientific Investigation – (AMSI)
- News media
- Civil Georgia, daily news about Georgia
- Crisis profile, Georgia, Abkhazia, S. Ossetia Ilihifadhiwa 10 Juni 2009 kwenye Wayback Machine. From Reuters Alertnet Ilihifadhiwa 11 Machi 2009 kwenye Wayback Machine.
- Georgian Daily Ilihifadhiwa 17 Oktoba 2008 kwenye Wayback Machine., all the latest news from Georgia and related to Georgia
- NewsGeorgia Google Translation into English from the NewsGeorgia (Russian Language) site
- GeorgiaCaucasus.com GeorgiaCaucasus.com – online info Magazine dedicated to Georgia and Caucasus
Nchi na maeneo ya Asia |
Afghanistan | Armenia2 | Azerbaijan | Bahrain | Bangladesh | Bhutan | Brunei | China | Falme za Kiarabu | Georgia2 | Hong Kong3 | Indonesia | Iran | Iraq | Israel | Jamhuri ya China (Taiwan) | Japani | Kamboja | Kazakhstan | Kirgizia | Korea Kaskazini | Korea Kusini | Kupro2 | Kuwait | Laos | Lebanoni | Macau3 | Malaysia | Maldivi | Mongolia | Myanmar | Nepal | Omani | Pakistan | Palestina | Qatar | Saudia | Singapuri | Sri Lanka | Syria | Tajikistan | Timor ya Mashariki | Turkmenistan | Ufilipino | Uhindi | Urusi1 | Uthai | Uturuki1 | Uzbekistan | Vietnam | Yemen | Yordani |
1. Nchi ina maeneo katika Asia na Ulaya. 2. Nchi iko Asia lakini inahesabiwa pia kati ya nchi za Ulaya kwa sababu za historia au utamaduni. 3. Eneo la pekee la China. |
![]() |
Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Georgia kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
![]() |
Makala hii kuhusu maeneo ya Asia bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Georgia kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |