Nenda kwa yaliyomo

Slovenia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Republika Slovenija
Jamhuri ya Slovenia
Bendera ya Slovenia Nembo ya Slovenia
Bendera Nembo
Kaulimbiu ya taifa: {{{national_motto}}}
Wimbo wa taifa: Zdravljica
Lokeshen ya Slovenia
Mji mkuu Lyublyana
46°03 N 14°30 E
Mji mkubwa nchini Lyublyana
Lugha rasmi Kislovenia, Kiitalia1, Kihungaria1
Serikali Jamhuri
Borut Pahor
Janez Janša
Uhuru
imetangazwa
25. Juni 1991
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
20,273 km² (ya 154)
0.6%
Idadi ya watu
 - Julai 2014 kadirio
 - 2002 sensa
 - Msongamano wa watu
 
2,061,085 (ya 144)
1,964,036
101/km² (ya 106)
Fedha Euro (EUR) tangu tarehe 1.1.2007 (SIT)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
CET (UTC+1)
CEST (UTC+2)
Intaneti TLD .si
Kodi ya simu +386

-

1 Katika miji yenye watu wengi wa utamaduni wa Kiitalia au Kihungaria.


Slovenia (jina rasmi: Jamhuri ya Slovenia) ni nchi ndogo ya Ulaya ya Kati. Inapakana na Italia magharibi, Austria kaskazini, Hungaria kaskazini mashariki, na Kroatia kusini na mashariki, huku ikipata ufukwe mfupi wa Bahari ya Adria magharibi kusini. Ina idadi ya watu takriban milioni 2.1, ikiwa ya 147 duniani. Mji mkuu na jiji kubwa zaidi ni Ljubljana. Slovenia ni sehemu ya Umoja wa Ulaya na ukanda wa euro, na inajulikana kwa mazingira yake ya kijani, milima ya Alps, maeneo ya mapango ya ajabu kama Postojna, na utamaduni wake unaochanganya Ulaya ya Kati na Bahari ya Mediterania.

Historia

[hariri | hariri chanzo]

Waslavi walihamia Slovenia ya leo katika karne ya 6 BK.

Tangu zamani waliishi chini ya utawala wa madola mbalimbali kama vile Dola la Roma, Austria na Yugoslavia hadi kupata uhuru wa kisiasa mara ya kwanza kabisa mwaka 1991 baada ya mwisho wa Shirikisho la Yugoslavia.

Kati ya nchi zote zilizotokana na Yugoslavia ya zamani Slovenia ni nchi yenye uchumi imara zaidi.

Watu wengi (83%) ni wa kabila la Waslovenia, wenye lugha ya Kislovenia ambayo ni kati ya lugha za Kislavoni.

Upande wa dini, 72.1% ni Wakatoliki. Waorthodoksi ni 3.7% na Waprotestanti 0.9%. Waislamu ni 3%. 10% wanajitambulisha kama Wakanamungu.

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
Wikimedia Commons ina media kuhusu:


Nchi za Umoja wa Ulaya Bendera ya Umoja wa Ulaya
Austria | Bulgaria | Eire | Estonia | Hispania | Hungaria | Italia | Kroatia | Kupro | Latvia | Lituanya | Luxemburg | Malta | Polandi | Slovakia | Slovenia | Romania | Ubelgiji | Ucheki | Udeni | Ufaransa | Ufini | Ugiriki | Uholanzi | Ujerumani | Ureno | Uswidi
Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Slovenia kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.