Guernsey

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Guernsey pamoja na visiwa vya kando
Mahali pa Visiwa vya Mfereji wa Kiingereza

Guernsey ni kisiwa kikubwa cha pili kati ya Visiwa vya mfereji wa Kiingereza chenye wakazi 63,000 hivi (2019). Kipo karibu na pwani ya Ufaransa lakini ni eneo chini ya taji la Uingereza isipokuwa si sehemu ya Uingereza wenyewe.

Mji pekee ni St Pierre Port wenye wakazi 16,000.

Lugha inayotumiwa ni hasa Kiingereza. Kuna bado wasemaji 2,000 wa lugha asilia ya Kiguernsey (Dgèrnésiais) lakini idadi yao inazidi kupungua.

Guernsey ni pia jina la jumla la tarafa inayounganisha kisiwa cha Guernsey pamoja na visiwa vidogo vya Alderney, Sark, Herm, Jethou, Brecqhou na Burhou. Pamoja na tarafa ya Jersey ni eneo la pili la visiwa vya mfereji wa Kiingereza.

Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Guernsey kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.