Serbia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Jamhuri ya Serbia
Република Србија
Republika Srbija
Bendera ya Serbia Nembo ya Serbia
Bendera Nembo
Kaulimbiu ya taifa: {{{national_motto}}}
Wimbo wa taifa: Bože pravde
Mungu wa haki
Lokeshen ya Serbia
Mji mkuu  Belgrad
44°48′ N 20°28′ E
Mji mkubwa nchini Belgrad
Lugha rasmi Kiserbia kinachoandikwa
kwa Mwandiko wa kikirili(1)
Serikali Jamhuri
Aleksandar Vučić
Ana Brnabić
Kutokea kwa taifa la Serbia
Kuzaliwa kwa taifa
Uhuru
kuanzishwa kwa Ufalme
kutwaliwa na Dola la Uturuki
Uasi wa kwanza
Katiba ya kwanza
Kutambuliwa na Mkutano wa Berlin
Yugoslavia
Serbia na Montenegro

karne ya 8
1166
1077
1459
14 Februari 1804
15 Februari 1835
1878
1918
5 Juni 2006
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
88,361 km² (ya 113)
0.13
Idadi ya watu
 - [[{{{population_estimate_year}}}]] kadirio
 - 2011 sensa
 - Msongamano wa watu
 
{{{population_estimate}}} ({{{population_estimate_rank}}})
7,186,862
92.8/km² (ya 112)
Fedha Dinari ya Serbia (2) (RSD)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
CET (UTC+1)
{{{time_zone_DST}}} (UTC{{{utc_offset_DST}}})
Intaneti TLD .yu (.rs) (3)
Kodi ya simu +381 (4)
1 Jimboni Vojvodina zifuatazo ni lugha rasmi kieneo: Kihungaria, Kislovakia, Kiromania, Kirusyn na Kikroatia. Katiba mpya imepanga pia kukubaliwa kwa mwandiko wa Kilatini kwa Kiserbia pamoja kikirili. Jimboni Kosovo lugha rasmi ni pia Kialbania na Kiingereza.
2 Euro hutumiwa jimboni Kosovo pamoja na dinar.
3 ".rs" ni rasmi tangu Septemba 2006 lakini anwani zenye ".yu" bado zinatumiwa.
4 pamoja na Montenegro hadi 2007.



Serbia (kwa Kiserbokroatia: Република Србија au Republika Srbija) ni nchi ya Ulaya kwenye rasi ya Balkani.

Imepakana na Hungaria, Bulgaria, Romania, Masedonia Kaskazini, Kosovo (au Albania), Montenegro, Bosnia na Herzegovina na Kroatia.

Mji mkuu ni Belgrad, wenye watu milioni 1,2.

Nchi ni mwanachama wa Umoja wa Mataifa na inatarajia kujiunga na Umoja wa Ulaya.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Waslavi walihamia Balkani baada ya karne ya 6.

Kati yao, Waserbia waliunda falme mbalimbali mwanzoni mwa Karne za Kati.

Mwaka 1217 Ufalme wa Serbia ulitambuliwa na Roma na Bizanti na mwaka 1346 ulifikia kilele cha ustawi wake kama Dola la Serbia.

Hali hiyo haikudumu muda mrefu, tena katikati ya karne ya 16 eneo lote la Serbia ya leo lilitekwa na Waosmani, ingawa pengine sehemu yake ilitawaliwa na Dola la Wahabsburg.

Mwanzoni mwa karne ya 19, mapinduzi ya Serbia ilileta ufalme wa kikatiba wa kwanza katika Balkani.

Ufalme huo ulizidi kuenea na baada ya vita vikuu vya kwanza vilivyosababisha vifo vingi vya raia zake, Serbia iliungana na makabila kuanzisha Yugoslavia iliyodumu hadi miaka ya 1990 iliposambaratika kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Mwaka 2006 hata Montenegro ilitengana na Serbia, ila kwa amani.

Mwaka 2008 bunge la jimbo la Kosovo lilijitangazia uhuru.

Watu[hariri | hariri chanzo]

Nchi, ukiondoa Kosovo, ina wakazi 7,186,862 kwenye eneo la km² 88.361. Wengi wao wana asili ya Kislavoni.

Upande wa dini 85% ni Waorthodoksi, 5% Wakatoliki, 3% Waislamu, 1% Waprotestanti.

Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Serbia kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.