Amazonas (mto)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mto Amazonas ni mto mkubwa kuliko mito yote duniani


Mto wa Amazonas
Beseni ya Amazonas
Chanzo mlima Nevado Mismi (Peru)
Mdomo Atlantiki
Nchi Brazil (62.4%), Peru (16.3%)
Bolivia (12.0%), Kolombia (6.3%)
Ekuador (2.1%)
Urefu 6,400 km
Kimo cha chanzo takriban 5,597 m
Tawimito upande wa kulia Purus, Madeira, Tapajós, Xingu, Tocantins
Tawimito upande wa kushoto Marañón, Japurá, Rio Negro
Mkondo 219,000 m³/s
Eneo la beseni 6,915,000 km²
Miji mikubwa kando lake Manaus, Macapa, Santarem

Mto Amazonas (kwa Kireno: Rio Amazonas) ndio mto mkubwa kuliko yote duniani. Unabeba maji zaidi kuliko mito ya Nile, Mississippi na Yangtse kwa pamoja.

Una chanzo chake katika milima ya Andes inavuka beseni lake hadi Atlantiki kupitia eneo kubwa la misitu minene. Sehemu kubwa ya mwendo wake iko katika nchi ya Brazil.

Kuhusu urefu hakuna bado mapatano ya kitaalamu kama Nile au Amazonas ndio mto mrefu duniani. Makadirio hutegemea ni tawimto lipi lenye chanzo cha mbali zaidi linaokubaliwa na wataalamu. Mwaka 1969 urefu wake ulipimwa kuwa km 6.400.

Amazonas ina matawimto zaidi ya 10,000 na kati ya hayo 17 yana urefu wa zaidi ya km 1,600 yakishinda mito kama Senegal, Gambia au Nile ya buluu.

Upana wa mto ni wa kilomita kadhaa kufikia hadi 100 wakati wa mafuriko ya kila mwaka. Delta ya Amazonas ina upana wa kilomita mia kadhaa; ndani yake kuna kisiwa cha Marajó chenye eneo la km² 49,000 ambalo ni kubwa kushinda nchi kama Rwanda au Burundi.

Amazonas ni njia muhimu ya mawasiliano na usafiri nchini Brazil. Meli kubwa za baharini zinaweza kuingia hadi bandari ya Manaus iliyoko km 800 ndani ya bara. Meli ndogo za baharini hadi uzito wa tani 3,000 zinaweza kuvuka Brazil yote hadi kufika Peru.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu maeneo ya Amerika Kusini bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Amazonas (mto) kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.