Uzito

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kifaa cha kupimia uzito.

Uzito wa kitu (jinsi chembe zilivyowekwa kwenye maada) ni kipimo cha kani inayoathiri kitu hiko kwa sababu ya uvutano au mchapuko. Uzito haupaswi kuchanganywa na dhana inayohusiana na tungamo. Kwa vitu vidogo duniani (au katika violwa vengine vya angani), uzito inaelekezwa kuelekea katikati ya sayari.

Kwa lugha ya kawaida, uzito unaweza kueleweka kirahisi pale unapopimwa karibu na dunia au kwenye uso wa dunia. Uzito kwa kawaida hupimwa kwa kutumia vizio vya tungamo kama vile kilogramu, gramu n.k., lakini kizio chake ni Newton (kifupi "N").

Kwa miaka mingi ya historia ya binadamu uzito umekuwa ukipimwa katika uso wa dunia. Uzito una uwiano sawa na tungamo. Kitu chochote chenye tungamo sawa kina uzito sawa. Imekuwa kawaida kuvitumia vitu hivyo viwili kila siku kwa pamoja. Kwa kawaida inawachanganya watu wengi kuhusiana na vitu hivyo viwili, tungamo na uzito.

Makala hii kuhusu mambo ya fizikia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Uzito kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.