Bogota

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Bogotá)


Jiji la Bogota
Nchi Kolumbia
Tovuti:  www.bogota.gov.co
Kanisa kuu la kale la Bogota

Bogota (jina kamili: Santa Fe de Bogotá) ni mji mkuu wa Kolombia pia mji mkubwa wa nchi mwenye wakazi milioni saba takriban.

Mji uko katika nyanda za juu kwenye kimo cha 2,640 m juu ya UB kati ya milima ya Guadalupe (3,317 m) na Monserrate (3,100 m).

Mji ulianzishwa na Mhispania Gonzalo Jiménez de Quesada tar. 6 Agosti 1538 kwenye mahali pa soko la Wachibcha lililoitwa "Bacata". Quesada alitumia jina la "Santa Fe" (kihisp.: "imani takatifu") kutokana na mji wa Hispania alikotokea mwenyewe.

Baadaye mji uliongezewa jina la pili "Bogota" kutokana na jina asilia "Bacata". Jina kamili lilikuwa "Santa Fe de Bogota".

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu maeneo ya Amerika Kusini bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Bogota kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.