Kihispania

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Kihisp.)
Kihispania duniani leo.

Kihispania ("español", kwa Kiingereza: Spanish) ni lugha ya kimataifa ambayo ni lugha ya kwanza kwa watu milioni 493; kwa jumla pamoja na wasemaji wa Kihispania kama lugha ya pili kuna milioni 568 duniani wanaosema vizuri Kihispania.

Historia ya lugha[hariri | hariri chanzo]

Asili ya lugha hiyo ni katika nchi ya Hispania (Ulaya kusini magharibi), lakini kutokana na historia ya ukoloni na ya biashara lugha hiyo imesambaa sana, hasa Amerika ya Kusini na ya Kati.

Lugha iliyozaa Kihispania ni Kilatini cha Waroma wa Kale waliotawala kwa muda mrefu Hispania. Ndiyo sababu maneno yake yanatokana na Kilatini kwa asilimia 80, lakini pia na Kiarabu kwa asilimia 8.

Kati ya lugha za Kirumi Kihispania ni lugha ya kisasa ambayo ni karibu zaidi na lugha ya kale, isipokuwa Kisardinia na Kiitalia.

Nchi zinazotumia Kihispania kama lugha rasmi[hariri | hariri chanzo]

Amerika ya Kati na Karibi[hariri | hariri chanzo]

Amerika ya Kusini[hariri | hariri chanzo]

Afrika[hariri | hariri chanzo]

Nchi zenye wasemaji wengi wa Kihispania[hariri | hariri chanzo]

  • Nchini Marekani Kihispania ni lugha ya pili baada ya Kiingereza hasa katika majimbo ya Kusini zilizokuwa zamani sehemu za Mexiko.
  • Ufilipino kwa sababu ilikuwa koloni la Hispania

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]