Wanamgambo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mwanamgambo wa Kenya.

Wanamgambo (pia: "mgambo" tu) ni askari wa akiba wasioajiriwa na jeshi rasmi la nchi, ila walipitia mafunzo ya awali ya kijeshi ili wasaidie kulinda usalama wa raia na mali yao.

Mara nyingine, wanamgambo wanatumia uzoefu na silaha zao kuunda kikosi cha kupigania sera fulani na hata kuwa kundi la wahalifu katika mazingira ya vita, hasa vya wenyewe kwa wenyewe.