Uswidi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Sweden)
Uswidi


Uswidi (kwa Kiswidi: "Sverige") ni nchi ya Skandinavia katika Ulaya ya Kaskazini. Imepakana na Ufini (Finland) na Norwei.

Jiografia[hariri | hariri chanzo]

Nchi imegawiwa katika mikoa mitatu: Norrland katika kaskazini, Svealand katikati na Götaland katika kusini.

Ina pwani ndefu kwenye bahari ya Baltiki. Kuna daraja la kuvukia mlango wa bahari ya Oresund ya kuunganisha Uswidi na Denmark.

Kuna misitu mikubwa sana na maziwa mengi.

Hali ya hewa ya sehemu kubwa ya Uswidi si baridi kutokana na athira ya mkondo wa Ghuba. Kuna tofauti kati ya urefu wa mchana katika miezi ya Mei hadi Julai na giza wakati wa Desemba. Tarehe 21 Juni ni siku ndefu: hakuna giza kabisa na usiku wake Waswidi hufanya sherehe kubwa ya "midsommar" kwa ngoma na dansi kote nchini.

Mji mkuu ni Stockholm, nao unaongoza kwa wingi wa wakazi.

Milima na vilele[hariri | hariri chanzo]

Vilele vya juu kwa kila "landskap" ni kama ifuatavyo. Kumbuka kwamba "landskap" katika Uswidi ni sahihi kidogo tu. Basi maoni mengine kuwepo.

Landskap Mlima Kimo
Blekinge Rävabacken 189
Bohuslän Björnerödspiggen 222
Dalarna Storvätteshågna 1204
Dalsland Baljåsen 302
Gotland Lojsta hed 83
Gästrikland Lustigknopp 402
Halland Högalteknall 226
Hälsingland Garpkölen 671
Härjedalen Helags 1797
Jämtland Storsylen 1743
Lappland Kebnekaise 2104
Medelpad Myckelmyrberget 577
Norrbotten Vitberget 594
Närke Tomasbodahöjden 298
Skåne Söderåsen 212
Småland Tomtabacken 377
Södermanland Skogsbyås 124
Uppland Tallmossen 118
Värmland Granberget 701
Västerbotten Åmliden 550
Västergötland Galtåsen 361
Västmanland Fjällberget 466
Ångermanland Tåsjöberget 635
Öland Högsrum 55
Östergötland Stenabohöjden 328

Wilaya[hariri | hariri chanzo]

Län Herufi Mji mkuu Eneo Ramani
Blekinge län K Karlskrona 2.947 km²
Dalarnas län W Falun 28.196 km²
Gotlands län I Visby 3.151 km²
Gävleborgs län X Gävle 18.200 km²
Hallands län N Halmstad 5.462 km²
Jämtlands län Z Östersund 49.343 km²
Jönköpings län F Jönköping 10.495 km²
Kalmar län H Kalmar 11.219 km²
Kronobergs län G Växjö 8.467 km²
Norrbottens län BD Luleå 98.249 km²
Skåne län M Malmö 11.035 km²
Stockholms län AB Stockholm 6.519 km²
Södermanlands län D Nyköping 6.103 km²
Uppsala län C Uppsala 8.208 km²
Värmlands län S Karlstad 17.591 km²
Västerbottens län AC Umeå 55.190 km²
Västernorrlands län Y Härnösand 21.685 km²
Västmanlands län U Västerås 5.145 km²
Västra Götalands län O Göteborg 23.956 km²
Örebro län T Örebro 8.546 km²
Östergötlands län E Linköping 10.645 km²
Jumla 410.977 km²

Historia[hariri | hariri chanzo]

Wakazi wa kwanza kujilikana walikuwa makabila ya Kigermanik kama wakazi wote waliowafuata. Huko Roma Tacitus aliandika juu yao mwaka 98 BK.

Kati ya karne ya 8 hadi ya 11 waliitwa mara nyingi "Waviking" wakiogopwa na wenyeji wa Ulaya bara kwa sababu Waviking walivamia mara kwa mara maeneo ya pwani kwa jahazi zao ndogo. Lakini Waviking au Wanormani ni neno la kutaja watu wa Kaskazini waliovamia na kufanya ujambazi kwenye nchi za Ulaya bara si namna jinsi wenyewe walivyojiita.

Nchi na jirani zake mwaka 1219 BK.

Malkia Margarete I wa Udani aliolewa na mfalme wa Norway. Baada ya kifo cha mumewe alitawala nchi zote mbili na baadaye pia Uswidi. Mwaka 1397 wawakilishi wa falme tatu zilikutana katika mji wa Kalmar (Uswidi ya kusini) na kuelewana juu ya "Umoja wa Kalmar" yaliyounganisha nchi zote za Skandinavia chini ya mfalme wa Denmark ilhali kila nchi iliendelea kujitawala. Wakati ule Ufini (Finland) ilikuwa chini ya Uswidi. Iceland na Visiwa vya Faroe ziliingia pia kwa sababu zilikuwa chini ya Norway wakati ule.

Umoja huo uliendela hadi mwaka 1521. Waswidi walianza kuchoka na utawala wa Kidenmark wakaondoka katika umoja huu mwaka 1521 pamoja na Ufini. Lakini Norway iliendela kuwa chini ya Denmark hadi mwaka 1814.

Uswidi ulijiunga na Matengenezo ya Kiprotestanti na kanisa la Kilutheri likawa dini rasmi nchini hadi mwaka 2000. Hivyo Uswidi ikawa kati ya nchi muhimu sana ya Ulutheri.

Uswidi ulistawi na kueneza himaya yake kuanzia karne ya 17 hadi mwanzo wa karne ya 18 kama mojawapo kati ya nchi zenye nguvu zaidi Ulaya.

Baadaye ilirudi nyuma hadi kunyang'anywa kwa Ufini na Warusi (1809).

Kati ya miaka 1814 na 1905 ililazimisha Norwei kukubali mfalme wa Uswidi kama mfalme wa Norwei pia.

Tangu hapo Uswidi umeshika msimamo wa amani na wa kutoshikamana na nchi yoyote.

Kwa sasa Uswidi ni ufalme wa kikatiba yaani Mkuu wa Dola ni mfalme (kwa sasa Carl XVI Gustaf), lakini huyu mfalme anapaswa kufuata sheria ya katiba ya nchi. Utawala umo mikononi mwa serikali iliyochaguliwa kidemokrasia.

Katika karne ya 20 Uswidi umefaulu vizuri kujenga uchumi ili kuondoka katika umaskini na kuwa moja kati ya nchi tajiri za dunia (ikiwa na nafasi ya 8 kwa pato la kichwa).

Nchi ilijiunga na Umoja wa Ulaya mwaka 1995 lakini haikukubali pesa ya Euro ikaendelea na Krona ya Uswidi.

Watu[hariri | hariri chanzo]

Uswidi ni nchi kubwa yenye wakazi wachache: mwaka 2017 kwa mara ya kwanza wamezidi milioni 10, wengi wao wenye asili ya makabila ya Kijerumani, lakini kwa sasa 32.2% wana damu tofauti au mchanganyiko.

Lugha rasmi ni Kiswidi, ambacho kinafanana sana na Kidani na Kinorwe. Lugha ya pili kati ya tano zilizokubalika kwa makundi madogo ya asili ni Kifini (5%), lakini siku hizi uhamiaji umefanya Kiarabu kiwe na watumiaji wengi zaidi.

Asilimia 89 wanaweza kuongea Kiingereza pia.

Upande wa dini, 57.7% ni Walutheri, lakini kati yao 2% tu wanashiriki ibada ya kila wiki. Waprotestanti wengine ni 275,000, Waorthodoksi wa Mashariki 100,000 na Wakatoliki 92,000.

Waislamu ni kama 600,000, lakini wengi hawashiriki, na 25,000 tu wanafuata swala tano.

Picha[hariri | hariri chanzo]

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Tovuti rasmi
Habari
Biashara
Utalii


Nchi za Umoja wa Ulaya Bendera ya Umoja wa Ulaya
Austria | Bulgaria | Eire | Estonia | Hispania | Hungaria | Italia | Kroatia | Kupro | Latvia | Lituanya | Luxemburg | Malta | Polandi | Slovakia | Slovenia | Romania | Ubelgiji | Ucheki | Udeni | Ufaransa | Ufini | Ugiriki | Uholanzi | Ujerumani | Ureno | Uswidi
Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Uswidi kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.