Nenda kwa yaliyomo

Cabo Verde

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Cape Verde)
Jamhuri ya Cabo Verde
República de Cabo Verde (Kireno)
Kaulimbiu:
Unidade, Trabalho, Progresso (Kireno)
"Umoja, Kazi, Maendeleo"
Wimbo wa taifa: Cântico da Liberdade (Kireno)
"Mkarara wa Uhuru"
Mahali pa Cabo Verde
Ramani ya Cabo Verde
Mji mkuu
na mkubwa
Praia
20°54′ N 156°22′ W
Lugha rasmiKireno
Kikaboverde
SerikaliJamhuri
 • Rais
 • Waziri Mkuu
José Maria Neves
Ulisses Correia e Silva
Eneo
 • Jumlakm2 4,033[1]
Idadi ya watu
 • Kadirio la 2023603,901[1]
PLT (PPP)Kadirio la 2023
 • JumlaOngezeko USD bilioni 5.717[2]
 • Kwa kila mtuOngezeko USD 9,909[2]
PLT (Kawaida)Kadirio la 2023
 • JumlaOngezeko USD bilioni 2.598[2]
 • Kwa kila mtuOngezeko USD 4,503[2]
HDI (2021)Ongezeko 0.662[3] - kati
SarafuEscudo ya Cabo Verde
Tovuti rasmi:
.cv

Cabo Verde,rasmi Jamhuri ya Cabo Verde (kwa Kireno: República de Cabo Verde), ni nchi ya visiwa iliyoko katika Bahari ya Atlantiki ya Kaskazini, takriban kilomita 570 magharibi mwa pwani ya Afrika ya Magharibi. Inajumuisha visiwa kumi vya asili ya volkeno vilivyogawanywa katika makundi mawili: Visiwa vya Barlavento (kaskazini) na Visiwa vya Sotavento (kusini). Mji mkuu wake ni Praia, ulioko katika kisiwa cha Santiago, ambacho pia ni kisiwa chenye watu wengi zaidi. Cabo Verde ina wakazi takriban 603,901 (2023) na eneo la kilomita za mraba 4,033.

Cabo Verde ni jamhuri ya bunge yenye serikali thabiti ya kidemokrasia, ikiongozwa na Rais José Maria Neves na Waziri Mkuu Ulisses Correia e Silva. Lugha rasmi ni Kireno, ingawa Kikaboverde kinazungumzwa sana katika maisha ya kila siku. Uchumi wa nchi unategemea zaidi sekta ya huduma kama vile utalii, fedha kutoka kwa raia wanaoishi ughaibuni, na uvuvi. Pato la taifa kwa kila mtu lilifikia dola 4,503 kwa mwaka 2023. Licha ya kuwa na rasilimali chache za asili, Cabo Verde imepata mafanikio makubwa katika elimu, afya, na utawala bora, na inaonyesha kiwango cha juu cha maendeleo ya binadamu katika Afrika ya Magharibi.

Jiografia

[hariri | hariri chanzo]

Eneo la visiwa vyake kwa jumla ni km² 4,033.

Funguvisiwa lake lina visiwa 15 katika vikundi viwili:

Mji mkuu ni Praia katika kisiwa cha Santiago.

Miji mikubwa zaidi ni (takwimu za mwaka 2010): Praia (wakazi 127,832), Mindelo (wakazi 70,468), Santa Maria (wakazi 23,839), Assomada (wakazi 12,026), Pedra Badejo (wakazi 9,345) na São Filipe (wakazi 8,125).

Historia

[hariri | hariri chanzo]

Hadi kufika kwa Wareno katika karne ya 15 visiwa vya Cabo Verde havikuwa na watu.

Wareno walianzisha mashamba ya miwa na kuleta watumwa kutoka bara la Afrika.

Cabo Verde ilikuwa pia kituo muhimu cha biashara ya watumwa kati ya Afrika na Amerika.

Wahamiaji kutoka Ulaya walikuwa pia Wahispania, Waitalia pamoja na Wayahudi na Waislamu waliokataliwa kukaa kwao Ureno.

Kutokana na historia hiyo, leo idadi kubwa ya wakazi ni machotara waliozaliwa na Waafrika (waliochangia 56% ya DNA) na Wazungu (waliochangia 44%).

Lugha rasmi ni Kireno, lakini wakazi wanazungumza zaidi aina mbalimbali za Krioli iliyotokana na lugha hiyo.

Upande wa dini, walau 89.1% ya wakazi ni Wakristo, hasa wa Kanisa Katoliki (78.7%), lakini pia wa madhehebu mbalimbali ya Uprotestanti (10.4%).

Kutokana na hali ngumu ya uchumi, wananchi wanaoishi nje ya Cabo Verde ni mara mbili kuliko wale wanaoishi nchini. Kati ya waliohama baada ya uhuru (1975), 500,000 wanaishi Marekani na 150,000 Ureno. Hata hivyo kuna wahamiaji vilevile, hasa kutoka nchi za Afrika bara.

Tazama pia

[hariri | hariri chanzo]
  1. 1.0 1.1 "Cabo Verde". The World Factbook (kwa Kiingereza) (tol. la 2025). Shirika la Ujasusi la Marekani. Iliwekwa mnamo 23 Machi 2024.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link) (Archived 2023 edition)
  2. 2.0 2.1 2.2 2.3 "World Economic Outlook Database, October 2023 Edition. (Cape Verde)". IMF.org. International Monetary Fund. 26 Machi 2024. Iliwekwa mnamo 26 Machi 2024.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  3. Human Development Report 2020 The Next Frontier: Human Development and the Anthropocene (PDF). United Nations Development Programme. 15 Desemba 2020. ku. 343–346. ISBN 978-92-1-126442-5. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo (PDF) mnamo 15 Desemba 2020. Iliwekwa mnamo 16 Desemba 2020.{{cite book}}: CS1 maint: date auto-translated (link)

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:


Nchi za Afrika Bara la Afrika
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad | Cote d'Ivoire | Eritrea | Eswatini | Ethiopia | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Jibuti | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesotho | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Sudan Kusini | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Zambia | Zimbabwe
Maeneo ya Afrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika
Hispania: Kanari · Ceuta · Melilla | Italia: Pantelleria · Pelagie | Ufaransa: Mayotte · Réunion | Uingereza: · St. Helena · Diego Garcia | Ureno: Madeira
Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Cabo Verde kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.