Kamerun

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Camerun)
Jamhuri ya Kameruni
République du Cameroun (Kifaransa)
Republic of Cameroon (Kiingereza)
Kaulimbiu ya taifa:
Paix – Travail – Patrie (Kifaransa)
Peace – Work – Fatherland (Kiingereza)
"Amani – Kazi – Nchi"
Wimbo wa taifa: Chant de Ralliement
Mahali pa Kamerun
Mahali pa Kamerun
Mji mkuuYaunde
3°52′ N 11°31′ E
Mji mkubwa nchiniDuala
04°03′ N 09°41′ E
Lugha rasmi
SerikaliJamhuri yenye mdikteta
 • Rais
 • Waziri Mkuu
Paul Biya
Joseph Dion Ngute
Eneo
 • Eneo la jumlakm2 475 440[1]
 • Maji (asilimia)0.57[1]
Idadi ya watu
 • Kadirio la 202330 135 732[1]
Pato la taifaKadirio la 2023
 • JumlaOngezeko USD bilioni 49.262[2]
 • Kwa kila mtuOngezeko 1 721[2]
Pato halisi la taifaKadirio la 2023
 • JumlaOngezeko USD bilioni 133.335[2]
 • Kwa kila mtuOngezeko USD 4 660[2]
Maendeleo (2021)Imara 0.576[3] - wastani
SarafuFaranga ya CFA
Majira ya saaUTC+1
(Afrika Magharibi)
Upande wa magariKulia
Msimbo wa simu+237
Msimbo wa ISO 3166CM
Jina la kikoa.cm

Kameruni, kirasmi Jamhuri ya Kameruni, ni jamhuri ya muungano katika Afrika ya Magharibi.

Imepakana na Nijeria, Chadi, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Jamhuri ya Kongo, Gabon, Gine ya Ikweta na Ghuba ya Gine.

Lugha rasmi na lugha za taifa ni Kifaransa (kinachoongoza kwa zaidi ya asilimia 80) na Kiingereza.

Jiografia[hariri | hariri chanzo]

Mpare kwa mlima Kameruni
Mlima Kamerun kutoka Tiko, Mkoa wa Kusini-Magharibi

Maeneo kiutawala[hariri | hariri chanzo]

Kameruni imegawiwa katika mikoa (regions) 10 na wilaya (départements) 58.

Mikoa ni:


Ona pia: Orodha ya miji ya Kameruni

Historia[hariri | hariri chanzo]

Historia ya awali[hariri | hariri chanzo]

Katika karne za BK Wabantu wenye ujuzi wa kilimo na uhunzi walianza uenezi wao kutoka huko kwenda kutawala maeneo mengi ya Afrika ya Kati, Kusini mwa Afrika na Afrika Mashariki.

Wakati wa ukoloni[hariri | hariri chanzo]

Kameruni ilikuwa koloni la Ujerumani hadi Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia. Baada ya Ujerumani kushindwa vita, nchi ikagawiwa kati ya Uingereza na Ufaransa chini ya mamlaka ya Shirikisho la Mataifa kama eneo la kudhaminiwa.

Tangu uhuru hadi leo[hariri | hariri chanzo]

Mwaka wa 1960, Wafaransa waliacha Kameruni ikawa nchi huru. Wananchi wa Kameruni ya Kiingereza walipiga kura kuamua kama walitaka kuwa sehemu ya Nigeria au ya Kameruni. Kaskazini wengi walipendelea kukaa Nigeria, hivyo maeneo hayo sasa ni sehemu ya Nigeria. Wananchi wengi wa kusini waliamua wajiunge na Kameruni[4]. Kwa kusudi la kuheshimu tofauti za kiutamaduni kulikuwa na katiba mpya kwenye mwaka 1961 Shirikisho la Jamhuri ya Kameruni.

Tangu 1972 muundo wa nchi ulibadilishwa kuacha mfumo wa shirikisho na kuwa jamhuri ya muungano inayokazia zaidi matumizi ya lugha ya Kifaransa ingawa Kiingereza bado ni moja ya lugha rasmi. Jina la nchi pia likabadilishwa kuwa Jamhuri ya Muungano ya Kameruni mwaka wa 1972. Hapo sehemu ya Wakamerun wanaotumia lugha ya Kiingereza walijisikia kuwa wananyimwa haki zao.[5] Baadaye, mwaka wa 1984 jina likabadilishwa tena kuwa Jamhuri ya Kameruni (kwa Kifaransa République du Cameroun).

Tangu mwaka 2016 upinzani uliongezeka kati ya watu wa magharibi wanaotumia Kiingereza. Harakati hiyo ilijibiwa na serikali na polisi kwa ukali na hii umeleta kuanzishwa kwa wanamgambo wenye silaha wanaoshambulia polisi na jeshi la serikali kuu. Tangu mwaka 2017 wapinzani wamedai uhuru wa sehemu yenye lugha ya Kiingereza wakitangaza wameunda nchi mpya ya "Ambazonia". Serikali iliundwa inayokaa Nigeria; lakini kuna vikundi tofauti ambavyo wanapigana kati yao[6]. Nchi hii haitambuliwi kimataifa. Mwaka 2021 kulikuwa na majadiliano kuhusu amani kati kundi linalojiita serikali ya Ambazonia na serikali ya Kameruni[7], lakini makundi mengine yaliendelea na mapigano ya silaha[8].

Siasa[hariri | hariri chanzo]

Rais wa Kameruni Paul Biya (kulia)
Makala kuu: Siasa za Kamerun

Uchumi[hariri | hariri chanzo]

Majani chai inayotoka Kameruni
Makala kuu: Uchumi wa Cameroon

Watu[hariri | hariri chanzo]

Yaoundé, mji mkuu wa Kameruni (2003)
Picha, kaskazini mwa Kameruni
Ikulu ya sultani wa Bamun kwa Foumban, Mkoa wa Magharibi

Wakazi walikuwa 22,534,532 mwaka 2013, ambao wamegawanyika sawasawa kati ya wanaoishi mijini na wale wa vijijini.

Lugha rasmi ni Kifaransa pamoja na Kiingereza. Hata hivyo wakazi wanaongea pia lugha za makabila yao mengi.

Upande wa dini, 70% ni Wakristo (40% Wakatoliki na 30% Waprotestanti), 18% ni Waislamu, 3% ni wafuasi wa dini asilia za Kiafrika. 6% hawana dini yoyote.

Utamaduni[hariri | hariri chanzo]

Nyumba ya Njem
Mwanamke wa Maka akienda shamba
Familia ya Tikar, Kaskazini magharibi

Elimu[hariri | hariri chanzo]

Makala kuu: Elimu Kamerun

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. 1.0 1.1 1.2 "Cameroon § Summary". The World Factbook (kwa Kiingereza). Shirika la Ujasusi la Marekani. Iliwekwa mnamo 31 March 2024.  Check date values in: |accessdate= (help)
  2. 2.0 2.1 2.2 2.3 "World Economic Outlook Database, October 2023 Edition. (Cameroon)". International Monetary Fund. 10 October 2023. Iliwekwa mnamo 14 October 2023.  Check date values in: |date=, |accessdate= (help)
  3. "Human Development Report 2021/2022" (kwa Kiingereza). United Nations Development Programme. September 8, 2022. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2022-09-08. Iliwekwa mnamo September 8, 2022.  Unknown parameter |url-status= ignored (help); Check date values in: |date=, |accessdate= (help)
  4. 1961 British Cameroons Plebiscite, kwenye tovuti ya africanelections.tripod.com/referenda, iliangaliwa Januari 2019
  5. Anglophone crisis: Cameroon must return to federal system abolished under Ahidjo, Abdur Rahman Alfa Shaban kwenye tovuti ya africanews.com tar. 11/03/2018
  6. Ahead of peace talks, a who’s who of Cameroon’s separatist movements, tovuti ya The New Humanitarian tar. 8 July 2020
  7. Cameroon's separatist leader is willing to talk peace, but only with UN backing, Tovuti ya Deutsche Welle ya 23.03.2020
  8. Cameroon Events of 2020, tovuti ya Human Rights Watch, taarifa kuhusu Kamerun mwaka 2021

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:

Serikali

Habari

Elimu

Uchambuzi

Makabila na koo

Miongozo

Utalii


Nchi za Afrika Bara la Afrika
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad | Cote d'Ivoire | Eritrea | Eswatini | Ethiopia | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Jibuti | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesotho | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Sudan Kusini | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Zambia | Zimbabwe
Maeneo ya Afrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika
Hispania: Kanari · Ceuta · Melilla | Italia: Pantelleria · Pelagie | Ufaransa: Mayotte · Réunion | Uingereza: · St. Helena · Diego Garcia | Ureno: Madeira
Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Kamerun kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.