Afrika Kusini : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
d r2.5.2) (roboti Nyongeza: pap:Sur Afrika
Mstari 325: Mstari 325:
[[roa-rup:Africa di Not]]
[[roa-rup:Africa di Not]]
[[ru:Южно-Африканская Республика]]
[[ru:Южно-Африканская Республика]]
[[rw:Afurika y’Epfo]]
[[sa:दक्षिण अफ्रीका]]
[[sa:दक्षिण अफ्रीका]]
[[sah:Соҕуруу Африка]]
[[sah:Соҕуруу Африка]]

Pitio la 19:42, 4 Januari 2011

Afrika Kusini


Afrika Kusini ni nchi kubwa ya Afrika ya Kusini yenye wakazi takriban milioni 45. Imepakana na Namibia, Botswana, Zimbabwe, Msumbiji na Uswazi. Nchi ya Lesotho iko ndani ya eneo la Afrika Kusini.

Mji mkubwa ni Johannesburg. Wajibu wa mji mkuu yamegawiwa kwa mji mitatu: Cape Town ni makao ya Bunge, Pretoria ni makao ya Serikali na Bloemfontein ni makao ya Mahakama Kuu.

Nchi ina majina rasmi 11 kutokana na lugha rasmi 11. Ndizo Kiafrikaans, Kiingereza, Kizulu, Kixhosa, Kiswati, Kindebele, Kisotho cha Kusini, Kisotho cha Kaskazini, Kitsonga, Kitswana, Kivenda.

Kati ya watu mashuhuri sana wa Afrika Kusini ni Nelson Mandela aliyekuwa rais kati ya 1994 hadi 1999. Wengine ni Christiaan Barnard (daktari wa kwanza duniani aliyehamisha moyo wa mtu kwa mtu mwingine) na Shaka Zulu aliyekuwa kiongozi wa kijeshi kabla ya ukoloni.

Uchumi

Kiuchumi Afrika Kusini ni nchi yenye pande mbili kabisa. Sehemu ya uchumi ina hali ya kimaendeleo kabisa ikiwa viwanda na huduma za Afrika Kusini zinalingana na hali ya juu kabisa duniani na hali ya maisha ya wananchi waliomo katika sekta hii inalingana na nchi kama Australia au Ulaya ya magharibi. Kwa upande mwingine hali ya maisha ya sehemu kubwa ya wananchi ni umaskini kama katika sehemu nyingine za Afrika au Uhindi wa mashambani. Lakini kwa ujumla hali ya maisha iko juu kuliko nchi nyingi za Afrika.

Sekta muhimu za uchumi ni migodi ya kuchimba dhahabu au almasi, viwanda na huduma kama benki au bima.


Utawala na muundo wa shirikisho

Afrika Kusini ni shirikisho. Katiba mpya ya 1997 iliendeleza muundo huu uliundwa kama "Umoja wa Afrika Kusini" baada ya vita ya makaburu dhidi Uingereza. Afria ya Kusini ya kale ilikuwa na majimbo manne ya (Rasi, Natal, Dola Huru la Mto Orange na Transvaal). Maeneno makubwa yaliyokaliwa na Waafrika yalibaki nje katika katiba ya Apartheid yakiitwa bantustan (au: homeland). Katiba mpya ilichora mipaka upya.

Majimbo ya Afrika Kusini

Ramani ya majimbo na wilaya za Afrika Kusini

Mji mkuu wa jimbo watajwa katika mabano.

  1. Rasi ya Magharibi (Western Cape)¹ (Cape Town) kifupi: WC
  2. Rasi ya Kaskazini (Northern Cape) (Kimberley) kifupi: NC
  3. Rasi ya Mashariki (Eastern Cape) (Bhisho) kifupi: EC
  4. KwaZulu-Natal (Pietermaritzburg²) kifupi: KZ, KZN or KN
  5. Dola Huru (Free State) (Bloemfontein) kifupi: FS
  6. Kaskazini-Magharibi (Mafikeng) kifupi: NW
  7. Gauteng (Johannesburg) kifupi: GT or GP
  8. Mpumalanga (Nelspruit) kifupi: MP
  9. Limpopo (Polokwane) kifupi: LP

Miji Mikubwa

Ramani ya Afrika Kusini

Hii ni miji/ manisipaa/ jiji kumi yenye wakazi wengi nchini.

Na. Munisipaa au Jiji Wakazi (2001) Wakazi (1996) Asilimia ya badiliko
1996-2001
1. Johannesburg, Gauteng 3,225,812 2,639,110 22.2%
2. Durban, KwaZulu-Natal 3,090,117 2,751,193 12.3%
3. Cape Town, Rasi ya Magharibi 2,893,251 2,563,612 12.9%
4. East Rand, Gauteng 2,480,282 2,026,807 22.4%
5. Pretoria, Gauteng 1,985,984 1,682,701 18.0%
6. Port Elizabeth, Rasi ya Mashariki 1,005,776 969,771 3.7%
7. East London, Rasi ya Mashariki 701,881 682,287 2.9%
8. Vereeniging, Gauteng 658,422 597,948 10.1%
9. Bloemfontein, Dola Huru 645,441 603,704 6.9%
10. Thohoyandou, Limpopo 584,469 537,454 8.7%

Jeshi

Jeshi la Afrika Kusini ina silaha za kisasa kushinda nchi zote za majirani. Uchumi unawezesha nchi ya kutumia kiasi kikubwa kwa ajili ya jeshi kuliko nchi zote za Afrika kusini ya Sahara.

Afrika Kusini iliwahi kuwa na silaha za kinyuklia lakini ilizibomoa baada ya mwaka 1993.

Viungo vya nje

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:


Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika Kusini bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Afrika Kusini kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.



Nchi za Afrika Bara la Afrika
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad | Cote d'Ivoire | Eritrea | Eswatini | Ethiopia | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Jibuti | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesotho | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Sudan Kusini | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Zambia | Zimbabwe
Maeneo ya Afrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika
Hispania: Kanari · Ceuta · Melilla | Italia: Pantelleria · Pelagie | Ufaransa: Mayotte · Réunion | Uingereza: · St. Helena · Diego Garcia | Ureno: Madeira

Kigezo:Link FA Kigezo:Link FA Kigezo:Link FA