Nenda kwa yaliyomo

Mauritania

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Jamhuri ya Mauritania)
الجمهورية الإسلامية الموريتانية
Al-Ǧumhūriyyah al-Islāmiyyah al-Mūrītāniyyah
République Islamique de Mauritanie

Jamhuri ya Kiislamu ya Mauritania
Bendera ya Mauritania Nembo ya Mauritania
Bendera Nembo
Kaulimbiu ya taifa: Kiarabu: شرف إخاء عدل;
Kifaransa: Honneur, Fraternité, Justice
(Heshima, Undugu, Haki)
Wimbo wa taifa: كن للاله ناصرا وأنكر المناكر
(Uwe msaidizi wa Mungu)
Lokeshen ya Mauritania
Mji mkuu Nouakchott
18°09′ N 15°58′ W
Mji mkubwa nchini Nouakchott
Lugha rasmi Kiarabu
Serikali Jamhuri, serikali ya kirais
Mohamed Ould Ghazouani
Uhuru
 - Tarehe
Kutoka Ufaransa
28 Novemba 1960
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
1,030,700 km² (ya 29)
0.03
Idadi ya watu
 - 2005 kadirio
 - 2013 sensa
 - Msongamano wa watu
 
3,086,859 (129)
3,537,368
3.2/km² (ya 221)
Fedha Ouguiya (MRO)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
GMT (UTC+0)
-- (UTC+0)
Intaneti TLD .mr
Kodi ya simu +222

-


Mauritania ni nchi ya Afrika kaskazini-magharibi. Upande wa magharibi kuna pwani ya bahari ya Atlantiki, upande wa kusini imepakana na Senegal, upande wa mashariki na Mali na Algeria, upande wa kaskazini na Sahara ya Magharibi inayotawaliwa na Moroko. Mji mkuu ni Nouakchott. Mji wa pili na kitovu cha uchumi ni bandari ya Nouadhibou karibu na mpaka wa Sahara Magharibi.

Jina limeteuliwa kutokana na Mauritania ya kale iliyokuwa ufalme wa Waberber kusini kwa Mediteranea katika eneo la Algeria na Moroko ya leo.

Wilaya za Mauritania

[hariri | hariri chanzo]

Mauritania ina wilaya 12 (zinaitwa "wilāyah").

  1. Adrar (Atâr)
  2. Assaba (Kifa)
  3. Brakna (Aleg)
  4. Dakhlet Nouâdhibou (Nouâdhibou)
  5. Gorgol (Kaédi)
  6. Guidimaka (Sélibabi)
  7. Hodh ech Chargui (Néma)
  8. Hodh el Gharbi (‘Ayoûn el ‘Atroûs)
  9. Inchiri (Akjoujt)
  10. Nouakchott (mji mkuu)
  11. Tagant (Tidjikja)
  12. Tiris Zemmour (Zouérat)
  13. Trarza (Rosso)
Ramani ya wilaya za Mauritania

Siasa ya Mauritania

[hariri | hariri chanzo]

Mnamo Machi 2007 wananchi walipata nafasi ya kumchagua rais kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi tangu uhuru. Sidi Ould Cheikh Abdallahi alishinda katika duru ya pili kwa 53% za kura zote akaapishwa tarehe 20 Aprili 2007. Lakini mwaka 2008 JeneralI Mohamed Ould Abdel Aziz alimpindua, akashinda uchaguzi miaka 2009 na 2014. Baada ya uchaguzi wa mwaka 2019 alianza kutawale jenerali Mohamed Ould Ghazouani na serikali yake isiyojali sana haki za binadamu.

Wakazi wengi (70%) ni Wamori, mchanganyiko wa Waarabu, Waberber na Waafrika waliotokana na watumwa kutoka kusini kwa Sahara. Asilimia 30 zilizobaki ni makabila ya Kiafrika yasiyoongea Kiarabu, ambacho ndicho lugha rasmi.

Pamoja na hayo, hadi leo asilimia 2.1 za wakazi ni watumwa, ingawa mwaka 2007 ilifutwa haki ya kuwamiliki.

Upande wa dini, karibu wote ni Waislamu (hasa Wasuni). Uhuru wa dini unabanwa sana kwa nyingine zote na ukanamungu unaadhibiwa kwa kifo. Wakristo ni 10,000 hivi, karibu wote wageni.

Tazama pia

[hariri | hariri chanzo]
  • Foster, Noel (2010). Mauritania: The Struggle for Democracy. Lynne Rienner Publishers. ISBN 978-1935049302.
  • Hudson, Peter (1991). Travels in Mauritania. Flamingo. ISBN 978-0006543589.
  • Murphy, Joseph E (1998). Mauritania in Photographs. Crossgar Press. ISBN 978-1892277046.
  • "Slavery's last stronghold". CNN. Iliwekwa mnamo 3 Februari 2014.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  • Pazzanita, Anthony G (2008). Historical Dictionary of Mauritania. Scarecrow Press. ISBN 978-0810855960.
  • Ruf, Urs (2001). Ending Slavery: Hierarchy, Dependency and Gender in Central Mauritania. Transcript Verlag. ISBN 978-3933127495.
  • Sene, Sidi (2011). The Ignored Cries of Pain and Injustice from Mauritania. Trafford Publishing. ISBN 978-1426971617.

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:


Nchi za Afrika Bara la Afrika
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad | Cote d'Ivoire | Eritrea | Eswatini | Ethiopia | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Jibuti | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesotho | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Sudan Kusini | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Zambia | Zimbabwe
Maeneo ya Afrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika
Hispania: Kanari · Ceuta · Melilla | Italia: Pantelleria · Pelagie | Ufaransa: Mayotte · Réunion | Uingereza: · St. Helena · Diego Garcia | Ureno: Madeira
Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Mauritania kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.