Nouadhibou
Mandhari
Nouadhibou | |
Majiranukta: 20°56′0″N 17°2′0″W / 20.93333°N 17.03333°W | |
Idadi ya wakazi (2013) | |
- Wakazi kwa ujumla | 118,167 |
---|

Nouadhibou (kwa Ar. نواذيبو Nuadhibu, jina la zamani Port-Étienne) ni mji mkubwa wa pili nchini Mauritania na bandari kubwa ya nchi hiyo. Iko kwenye rasi inayoingia katika Bahari Atlantiki kilomita chache kusini kwa mpaka wa Sahara Magharibi.
Idadi ya wakazi ni takriban watu 120,000[1]. Mji ni kitovu cha kiuchumi kwa sababu ya bandari inayohudumia taifa lote pamoja na kuwa mahali pa kupeleka madini ya chuma ya Zouérate kwenda soko la dunia. Upande mwingine wa uchumi ni uvuvi.
Mji ulianzishwa mwaka 1906 na wakoloni Wafaransa kama kituo cha uvuvi kwa jina la Port Etienne.
Tazama pia
[hariri | hariri chanzo]Tanbihi
[hariri | hariri chanzo]![]() |
Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Nouadhibou kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |