Thomas Aquinas Mtakatifu
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mtakatifu Thomas Aquinas (takriban 1224 – 7 Machi, 1274) alikuwa padri wa Kanisa Katoliki na mtawa wa Shirika la Wahubiri kutoka nchi ya Italia.
Kama mwanateolojia alichunguza hasa mawazo ya mwanafalsafa wa Ugiriki Aristoteli.
Pia anajulikana sana kwa vitabu vyake “Jumla ya Teolojia” (kwa Kilatini Summa theologiae) na “Jumla dhidi ya Wapagani” (kwa Kilatini Summa contra gentiles).
Alitangazwa kuwa mtakatifu 18 Julai 1323, halafu mwalimu wa Kanisa. Sikukuu yake ni tarehe 28 Januari.
| Makala hii kuhusu Mkristo huyu bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Thomas Aquinas Mtakatifu kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |