Eire

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Ireland)
Eire
Bendera
Nembo
Mji mkuu (na mkubwa zaidi){{{mji_mkuu}}}
53°26′ N 6°15′ W
Lugha rasmi{{{lugha_rasmi}}}
Serikali{{{serikali}}}
{{{vyeo_viongozi}}}{{{majina_viongozi}}}
{{{muundo_uhuru}}}{{{tarehe_uhuru}}}
Eneo
 • Eneo la jumla{{{eneo_jumla}}}
 • Maji (%){{{maji}}}
Idadi ya watu
 • Kadirio la 2023{{{watu_kadirio}}}
Pato la TaifaKadirio la 2023
 • Jumla{{{pato}}}
 • Kwa kila mtu{{{pato_kwa_mtu}}}
Pato Halisi la TaifaKadirio la 2023
 • Jumla{{{pato_halisi}}}
 • Kwa kila mtu{{{pato_halisi_kwa_mtu}}}
Maendeleo ({{{mwaka_maendeleo}}}){{{maendeleo}}}
Fedha{{{fedha}}}
Majira ya saa{{{majira_saa}}}
Muundo wa tareheDD/MM/YYYY

Eire (pia: Ireland, Ayalandi; kwa Kiingereza mara nyingi Republic of Ireland) ni nchi ya kisiwani katika funguvisiwa la Britania ya Ulaya.

Eire ilitawaliwa na Uingereza hadi mwaka 1922. Sehemu ya kaskazini ya kisiwa imebaki kama sehemu ya Ufalme wa Muungano (pamoja na Uingereza, Uskoti na Welisi).

Mji mkuu ni Dublin.

Jiografia[hariri | hariri chanzo]

Kijiografia Eire ni kisiwa kilichogawiwa kati ya Jamhuri ya Eire inayokalia sehemu kubwa ya kisiwa na Northern Ireland ambayo ni jimbo la Ufalme wa Maungano. Kisiwa chote kina eneo la km² 84,421 na 83% zake ni Jamhuri ya Eire.

Upande wa magharibi kuna Bahari ya Atlantiki, upande wa mashariki Bahari ya Eire inayokitenga na kisiwa cha Britannia.

Jiografia[hariri | hariri chanzo]

Kitovu cha kisiwa kuna tambarare inayozungukwa nje upande wa pwani na vilima.

Mlima mrefu zaidi ni Carrauntoohil wenye kimo cha mita 1,038.

Mto mkubwa ni Shannon ambao kutoka kaskazini unaelekea kusini. Kwenye tambarare ya katikati kuna maziwa kadhaa.

Hali ya hewa inaathiriwa na Atlantiki: ni ya wastani, hakuna baridi kali wala joto kali.

Bahari inaleta mvua nyingi na hivyo Eire huitwa "Kisiwa cha Kijani".

Miji mikubwa ni Dublin (wakazi milioni 1), Cork (watu 190,000), Limerick (90,000), Galway (72,000) na Waterford (49,000).

Historia[hariri | hariri chanzo]

Kwa karne kadhaa Eire ilitawaliwa na Uingereza.

Sheria ya mwaka 1800 iliunganisha Ufalme wa Britania Kuu na Ufalme wa Eire na hivyo kuunda Ufalme wa Muungano (United Kingdom of Great Britan and Ireland).

Baada ya Vita vya uhuru vya Eire bunge la London kwa sheria ya mwaka 1920 (Government of Ireland Act 1920) liligawa Ireland katika sehemu mbili za Northern Ireland na Southern Ireland.

Wabunge waliochaguliwa katika Ireland ya Kusini walijitangaza kuwa bunge la Eire na kwa mapatano ya mwaka 1922 uhuru wa Eire ulitambuliwa. Nchi mpya ilijiita tangu 1937 "Jamhuri ya Eire" na kuendelea kama nchi ya pekee.

Baada ya uhuru wa sehemu kubwa ya kisiwa hicho, ile ya kaskazini-mashariki imebaki kama sehemu ya Ufalme wa Muungano.

Watu[hariri | hariri chanzo]

Wakazi walio wengi (82.2%) ni Waeire asili, Wazungu wengine ni 9.5%, Waasia 2.1%, Waafrika 1.2% n.k.

Wengi hutumia lugha ya Kiingereza lakini lugha ya Kieire ni lugha ya kwanza ya taifa. Kinazungumzwa katika maeneo kadhaa ya vijijini na hufundishwa shuleni, lakini kutokana na uhamiaji, Kipolandi kina wasemaji wengi zaidi.

Upande wa dini, 78.3% ni Wakatoliki na 4.2% ni Wakristo wa madhehebuya Uprotestanti na 1.3% ni Waorthodoksi. Ushiriki wa ibada ni wa juu sana. Waislamu ni 1.3% na 9.8% hawana dini.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Gilland, Karin (2001). Ireland: Neutrality and the International Use of Force. Routledge. ISBN 0-415-21804-7. 
  • Greenwood, Margaret (2003). Rough guide to Ireland. Rough Guides. ISBN 1-84353-059-7. 
  • Mangan, James Clarence (2007). James Clarence Mangan – His Selected Poems. Read Books. ISBN 1-4086-2700-0. 
  • Meinardus, Otto Friedrich August (2002). Two thousand years of Coptic Christianity. American Univ in Cairo Press. ISBN 977-424-757-4. 
  • Moody, Theodore William (2005). A New History of Ireland: Prehistoric and early Ireland. Oxford University Press. ISBN 0-19-821737-4. 

Marejeo mengine[hariri | hariri chanzo]

  • Bunreacht na hÉireann (the 1937 constitution)
  • The Irish Free State Constitution Act, 1922
  • J. Anthony Foley and Stephen Lalor (ed), Gill & Macmillan Annotated Constitution of Ireland (Gill & Macmillan, 1995) (ISBN 0-7171-2276-X)
  • FSL Lyons, Ireland Since the Famine
  • Alan J. Ward, The Irish Constitutional Tradition: Responsible Government and Modern Ireland 1782–1992 (Irish Academic Press, 1994) (ISBN 0-7165-2528-3)
  • Michael J. Geary, An Inconvenient Wait: Ireland's Quest for Membership of the EEC, 1957–73 (Institute of Public Administration, 2009) (ISBN 978-1-904541-83-7)

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Serikali
Taarifa za jumla


Nchi za Umoja wa Ulaya Bendera ya Umoja wa Ulaya
Austria | Bulgaria | Eire | Estonia | Hispania | Hungaria | Italia | Kroatia | Kupro | Latvia | Lituanya | Luxemburg | Malta | Polandi | Slovakia | Slovenia | Romania | Ubelgiji | Ucheki | Udeni | Ufaransa | Ufini | Ugiriki | Uholanzi | Ujerumani | Ureno | Uswidi
Makala hii kuhusu maeneo ya Ireland bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Eire kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.