Uskoti

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Scotland (Kiingereza)
Alba (Kigaeli)
Uskoti
Bendera ya Uskoti
Bendera Nembo
Wito: Nemo me impune lacessit
(Kilatini: Hakuna anayenichokoza bila adhabu)
Uskoti katika Ulaya


Uskoti katika Ulaya

Uskoti (kijani cheusi) katika kisiwa cha Britania
Uskoti (kijani cheusi) katika kisiwa cha Britania (Uingereza)
Lugha Kiingereza, Kigaeli, Kiskoti
Mji mkuu Edinburgh
Mji mkubwa Glasgow
Waziri Mkuu Nicola Sturgeon
Eneo
- Total
- % water

78,782 km²
1.9%
Wakazi
- Jumla (2001)
- msongamano

5,062,011
64/km²
GDP (PPP)
 • Total
 • Per capita
2002 est.
$130 Billioni
$25,546
Pesa Pound sterling (£) (GBP)
Time zone
 - Summer (DST)
GMT (UTC+0)
BST (UTC+1)
Internet TLD .uk
Calling Code 44

Uskoti ni nchi ya Ulaya. Iko kaskazini mwa kisiwa cha Britania Kuu ikiwa sehemu ya Ufalme wa Muungano wa Britania na Eire ya Kaskazini.

Jiografia[hariri | hariri chanzo]

Uskoti ni theluthi ya kaskazini ya kisiwa cha Britania. Eneo lake ni km² 78,772. Upande wa kusini Uskoti umepakana na Uingereza wenyewe.

Upande wa mashariki kuna Bahari ya Kaskazini, upande wa kaskazini na magharibi ile ya Atlantiki pamoja na bahari ya Eire.

Ndani ya nchi kuna kanda tatu:

Mlima mkubwa wa Uskoti ni Mlima Nevis karibu na Fort William wenye kimo cha mita 1,344.

Mbali ya bara Uskoti ina visiwa 790. Upande wa magharibi wa Uskoti bara liko funguvisiwa la Hebridi. Upande wa kaskazini kuna visiwa vya Orkney na vya Shetland.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Kihistoria Uskoti uliwahi kuwa nchi ya pekee, mpaka ikaunganishwa chini ya Ufalme wa Uingereza tangu mwaka 1603 BK.

Tangu mwaka 1707 Uskoti haukuwa tena na bunge la pekee lakini ulikuwa na wawakilishi katika bunge la London. Bunge la Uskoti lilirudishwa tena mwaka 1999 nalo linasimamia mambo ya ndani.

Mnamo Septemba 2014, wananchi walipiga kura kuhusu uhuru wa nchi yao, lakini wengi waliamua kudumisha Ufalme wa Muungano. Hata hivyo, baada ya Ufalme huo kujitoa katika Umoja wa Ulaya, kuna mpango wa kupiga tena kura mwaka 2023.

Miji kumi mikubwa ya Uskoti[hariri | hariri chanzo]

Mji Wakazi
5 Aprili 1991
Wakazi
29 Aprili 2001
Glasgow (Glaschu) 658.379 629.501
Edinburgh (Dùn Èideann) 400.632 430.082
Aberdeen (Obar Dhèathain) 182.133 184.788
Dundee (Dùn Dè, Dùn Dèagh) 157.808 154.674
Paisley (Paislig) 73.925 74.170
East Kilbride (Cille Bhrìghde an Ear) 70.579 73.796
Hamilton (Hamaltan) 49.988 48.546
Cumbernauld (Comainn nan Allt) 49.507 49.664
Greenock (Grianaig) 49.267 45.467
Ayr (Àir) 47.962 46.431

Picha za Uskoti[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Uskoti kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.