Bendera ya Uskoti

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Bendera ya Uskoti
Bendera ya Uskoti kama Sehemu ya Bendera ya Ufalme wa Muungano wa Britania

Bendera ya Uskoti ina rangi ya buluu pamoja na msalaba wa Andrea mweupe. Huu ni msalaba unaolala wenye umbo la "X".

Bendera ya Uskoti ni kati ya bendera za kale kabisa duniani.

Bendera ya Uskoti kama sehemu ya bendera ya ufalme wa muungano wa Uskoti na Uingereza[hariri | hariri chanzo]

Mfalme James VI wa Uskoti alichaguliwa kuwa pia mfalme wa Uingereza kwa jina la James I mwaka 1601 akaunganisha bendera za nchi zote mbili kuwa bendera yake ya kifalme. Sheria ya muungano wa Uingereza na Uskoti ya mwaka 1707 ilifanya bendera hii kuwa bendera ya kitaifa.

Baadaye bendera ya Eire (Ireland) iliingizwa katika bendera ya muungano ya "Union Jack".

Hadithi juu ya asili ya msalaba wa Andrea[hariri | hariri chanzo]

Waskoti hukumbuka hadithi ya kuwa mfalme aliyeitwa Hungus (au:Angus) aliongoza Wapikti na Waskoti vitani dhidi ya Waanglia na Wasaksoni mnamo mwaka 832 BK lakini akajikuta katika hali ngumu pamoja na jeshi lake lote. Alipoomba msaada wa Mungu alimwona Mtume Andrea (aliyesulibiwa kwenye msalaba mwenye umbo la "X") aliyemwahidi ya kwamba atashinda. Asubuhi yake mawingu angani yalipatikana kwa umbo la msalaba wa "X". Waanglia na Wasaksoni walishtuka lakini Waskoti walishika moyo na kushinda.

Tangu wakati ule msalaba wa Andrea umekuwa bendera ya Uskoti.