Ukulu mtakatifu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ukulu wa Papa ndani ya Kanisa kuu la Roma, yaani Basilika la Mt. Yohane huko Laterani, ni ishara ya Ukulu mtakatifu.
Hii ni sehemu ya mfululizo kuhusu
Kanisa Katoliki
Imani

Umoja wa Mungu
Utatu (Baba, Mwana, Roho Mtakatifu)
Umwilisho Maisha ya Yesu
Msalaba Ufufuko Kupaa
Historia ya Wokovu Ufunuo
Biblia Mapokeo Ualimu Dogma
Neema Dhambi Wokovu Sakramenti
Watakatifu Bikira Maria

Muundo

Papa: Fransisko
Urika wa maaskofu Mitaguso mikuu
Kundi la Makardinali
Kanisa la Kilatini
Makanisa Katoliki ya Mashariki

Historia

Historia Ukristo
Ukatoliki Mlolongo wa Kitume
Sifa nne za Kanisa Utetezi Ekumeni
Maisha ya kiroho Amri Kumi Utawa
Sala Falsafa Teolojia
Muziki Sanaa Sayansi

Ibada

Liturujia Mwaka wa Kanisa
Ekaristi Liturujia ya Vipindi

Mapokeo ya liturujia

Liturujia ya Kilatini (Roma Liturujia ya Trento Milano Toledo Braga Lyon Canterbury)
Liturujia ya Armenia Liturujia ya Misri
Liturujia ya Ugiriki Liturujia ya Antiokia
Liturujia ya Mesopotamia

Ukulu mtakatifu au Ukulu wa Kitume (kwa Kiingereza: Holy See au Apostolic See) kwa maana asili ni kiti maalumu alichowekewa Papa katika Kanisa kuu la Roma, ambacho ni ishara ya mamlaka ya kiaskofu ambayo Wakatoliki wanasadiki anayo ya kufundisha, kutakasa na kuongoza Taifa la Mungu kokote duniani.

Katika imani ya Kikatoliki[hariri | hariri chanzo]

Kwa msingi huo, ukulu unamwakilisha Papa kama kiongozi wa Kanisa Katoliki lote duniani na kuhusiana na dogma ya kwamba ana karama ya kutodanganyika anapofundisha "rasmi" (kwa Kilatini "ex cathedra", yaani "kutoka ukulu") kama mkuu wa kundi la maaskofu.

Katika liturujia[hariri | hariri chanzo]

Sikukuu ya ukulu huo inaadhimisha kila mwaka tarehe 22 Februari[1] kwa jina la Ukulu wa Mtume Petro, ambaye aliambiwa na Bwana, “Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huo nitalijenga Kanisa langu” (Math 16:18) na anayeaminiwa kuwa ndiye aliyewarithisha Mapapa mamlaka yake kama mkuu wa Mitume wa Yesu.

Siku hiyo, ambayo Warumi walikuwa na desturi ya kufanya ukumbusho wa wafu wao, Wakatoliki wanaheshimu ukulu wa Mtume huyo, aliyemfia Yesu kitukufu katika kilima cha Vatikano, ambao unatakiwa kusimamia ushirika wa kimataifa wa upendo wa Kikristo.

Katika sheria za Kanisa[hariri | hariri chanzo]

Kadiri ya Mkusanyo wa Sheria za Kanisa la Kilatini (kanuni 361), "Ukulu mtakatifu" ni jina rasmi linalotumika kuwamaanisha Papa na miundo yote inayomsaidia kuongoza Kanisa Katoliki duniani ikiwa na makao makuu mjini Roma.

Ukulu usipokuwa na Papa[hariri | hariri chanzo]

Wakati Kanisa linapobaki halina Papa (kutokana na kifo au kujiuzulu), uongozi wake unashikwa na Kundi la Makardinali ambalo pia lina wajibu na haki ya kumchagua mwandamizi wake.

Katika mafungamano ya kimataifa[hariri | hariri chanzo]

Nchi zenye uhusiano na Ukulu mtakatifu.      Uhusiano wa kibalozi      Uhusiano mwingine      Bila uhusiano rasmi

Ukulu mtakatifu una hadhi ya nafsi ya kisheria katika sheria za kimataifa kutokana na umbile lake, mapokeo ya historia na mahitaji ya utume wake.

Ukulu mtakatifu unawakilisha kwa pamoja Kanisa Katoliki na nchi huru ya Mji wa Vatikani (ambayo iko chini ya mamlaka yake) katika mafungamano ya kimataifa na nchi yoyote duniani na miundo ya kimataifa kama vile Umoja wa Mataifa, ambapo unatambulika kama mojawapo kati ya watazamaji wa kudumu.

Ukulu mtakatifu na Vatikani[hariri | hariri chanzo]

Kisheria, ukulu mtakatifu ni tofauti na Mji wa Vatikani ambayo ni nchi huru inayotawaliwa na Papa na ilianzishwa rasmi tarehe 11 Februari 1929 kwa makubaliano kati ya Ukulu mtakatifu na Ufalme wa Italia. Eneo dogo la nchi hiyo (kilometa mraba 0.44) linadaiwa na kutosha ili kuhakikisha uhuru wa miundo ya Kanisa katika kutekeleza majukumu yake, lisije likaingiliwa na serikali yoyote kama ilivyotokea mara nyingi katika historia ya Kanisa.

Katika diplomasia ya kimataifa, mabalozi wanaowakilisha nchi huru nyingine (184, mwanzoni mwa mwaka 2023) wanatumwa kwa Ukulu mtakatifu, si kwa nchi ya Vatikani, na huitwa "balozi kwa Ukulu mtakatifu".

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Kuhusu kiti kama ishara ya mamlaka: Kikalio cha dhahabu

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu Kanisa Katoliki bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Ukulu mtakatifu kama historia yake au maelezo zaidi?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.