Mungu Baba

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru


Mungu Baba ni nafsi ya kwanza ya Mungu katika imani ya Wakristo (isipokuwa Wasiosadiki Utatu)[1][2].

Katika Uyahudi[hariri | hariri chanzo]

Katika Uyahudi Mungu aliitwa pengine Baba kwa jinsi alivyo asili ya uhai na anavyoshughulikia watu wake, hasa Waisraeli, mfalme wao na mafukara, wanaopaswa kumtegemea kama watoto.[3][4][5][6]

Katika Ukristo[hariri | hariri chanzo]

Kumbe katika Agano Jipya yeye ni hasa Baba wa Yesu, anayejitambulisha kama Mwana pekee wa Mungu. Nafsi hizo mbili pamoja na Roho Mtakatifu zinasadikiwa kuwa Mungu mmoja tu, asiyegawanyika katu.[7][8][9][8]

Kanuni ya Imani ya Nisea-Konstantinopoli tangu mwaka 325 inafafanua kuwa Yesu Kristo "amezaliwa na Baba tangu milele yote", yaani si uzazi uliotokea wakati wowote wala mahali popote duniani. Daima Mungu Baba ni Baba wa Mwana, asingeweza kuwepo bila kumzaa Mwana.

Wakristo wanafurahia kujua na kushirikishwa uhusiano huo wa milele kwa kufanywa na Roho Mtakatifu (Gal 4:4) "wana ndani ya Mwana pekee": ndiyo maana ya kujiita "wana wa kambo" wa Mungu, wakati Yesu ni Mwana asilia.[10][11]

Katika Uislamu[hariri | hariri chanzo]

Uislamu unamuamini Mungu kama muumbaji wa ulimwengu wote, lakini hauhimizi kumuita "Baba" kwa kuwa unataka kusisitiza ukuu wake usio na kifani.[12][13][14][15][16]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. The Oxford Handbook of the Trinity by Gilles Emery O. P. and Matthew Levering (27 Oct 2011) ISBN 0199557810 page 263
  2. Catholic catechism at the Vatican web site, items: 242 245 237
  3. Gerald J. Blidstein, 2006 Honor thy father and mother: filial responsibility in Jewish law and ethics ISBN 0-88125-862-8 page 1
  4. Calling God "Father" by John W. Miller (Nov 1999) ISBN 0809138972 pages x–xii
  5. Diana L. Eck (2003) Encountering God: A Spiritual Journey from Bozeman to Banaras ISBN 0807073024 p. 98
  6. Church Dogmatics, Vol. 2.1, Section 31: The Doctrine of God by Karl Barth (Sep 23, 2010) ISBN 0567012859 pages 15–17
  7. The Doctrine of God: A Global Introduction by Veli-Matti Kärkkäinen 2004 ISBN 0801027527 pages 70–74
  8. 8.0 8.1 The Trinity by Roger E. Olson, Christopher Alan Hall 2002 ISBN 0802848273 pages 29–31
  9. Tertullian, First Theologian of the West by Eric Osborn (4 Dec 2003) ISBN 0521524954 pages 116–117
  10. Paul's Way of Knowing by Ian W. Scott (Dec 1, 2008) ISBN 0801036097 pages 159–160
  11. Pillars of Paul's Gospel: Galatians and Romans by John F. O?Grady (May 1992) ISBN 080913327X page 162
  12. Gerhard Böwering, God and his Attributes, Encyclopedia of the Quran
  13. John L. Esposito, Islam: The Straight Path, Oxford University Press, 1998, p.22
  14. John L. Esposito, Islam: The Straight Path, Oxford University Press, 1998, p.88
  15. "Allah." Encyclopædia Britannica. 2007. Encyclopædia Britannica
  16. Vincent J. Cornell, Encyclopedia of Religion, Vol 5, pp.3561–3562
Makala hii kuhusu mambo ya dini bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hii kama historia yake au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.