Wakalvini

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ukuta wa Matengenezo mjini Geneva, Uswisi, unawaonyesha wanne kati ya Wakalvini wa kwanza; kutoka kushoto kwenda kulia ni: William Farel, John Calvin, Theodore Beza, na John Knox.


Wakalvini ni Wakristo Waprotestanti wanaofuata kimsingi mafundisho yaliyotolewa awali na Uldrik Zwingli na hasa John Calvin katika karne ya 16.

Tofauti na Luther, Zwingli na Calvin walijaribu moja kwa moja kujenga kanisa jipya kwenye msingi wa Biblia.

Hawakupenda kuchukua urithi wowote wa Kanisa Katoliki, wakaunda kila kitu upya kufuatana na jinsi walivyoelewa Biblia.

Katika utawala walikataa cheo cha uaskofu wakaona kanisa liongozwe na wazee wa kuchaguliwa. Kutokana na neno wazee katika lugha ya Agano Jipya (Kigiriki) "presbyuteroi", kanisa lake linaitwa pia la "Wapresbiteri".

Wafuasi wao huitwa pia "Wareformati" (to reform = kutengeneza upya). Maana yake walikataa desturi zote wasizoziona katika Biblia, wakati Luther alizikubali zile alizoziona hazipingi Biblia.

Katika ibada zao, Wareformati wanakataa altari, picha za kupamba kanisa au kuimba liturujia, wakati ibada ya Kilutheri ni Misa ya Kikatoliki iliyobadilishwa kufuatana na mawazo ya Luther. Katika jambo hilo hawakupatana na ndiyo sababu kwa muda mrefu Walutheri na Wareformati walishindwa kuwa na ibada za pamoja, lakini siku hizi wanaelewana.

Mafundisho hayo kutoka Uswisi yalienea katika nchi kama Ufaransa, Uskoti na Uholanzi. Hata Wamoravia walichukua sehemu ya mafundisho ya Wareformati, hasa juu ya Chakula cha Bwana, wakimfuata Luther katika mambo mengine.

Afrika Kusini urithi wa kidini wa Makaburu ni wa Kireformati kwa sababu babu zao walitokea Uholanzi na Ufaransa.

Vilevile ni wamisionari kutoka Uswisi na Uskoti walioanzisha mapema makanisa ya Kipresbiteri Malawi, Kenya na Afrika Magharibi.

Kadiri ya asili, madhehebu yao yanaitwa kwa Kiingereza Reformed, Congregationalists au Presbyterians.

Leo yana jumla ya waamini zaidi ya milioni 80, wengi wao wakiwa wameunganika katika "World Communion of Reformed Churches".

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • Allen, R. Michael (2010). Reformed Theology. Doing Theology. New York: T&T Clark. ISBN 978-0567034304. 
  • Bagchi, David V. N.; Steinmetz, David Curtis, eds. (2004), The Cambridge Companion to Reformation Theology, Cambridge: Cambridge University Press, ISBN 0-521-77662-7 
  • Cottret, Bernard (2000) [1995], Calvin: Biographie [Calvin: A Biography] (in French), Translated by M. Wallace McDonald, Grand Rapids, Michigan: Wm. B. Eerdmans, ISBN 0-8028-3159-1 
  • DeVries, Dawn (2003). "Rethinking the Scripture Principle". In Alston, Wallace M. Jr.; Welker, Michael. Reformed Theology: Identity and Ecumenicity. Grand Rapids, MI: William B. Eerdmans Publishing Company. ISBN 978-0802847768. 
  • Furcha, E. J., ed. (1985), Huldrych Zwingli, 1484–1531: A Legacy of Radical Reform: Papers from the 1984 International Zwingli Symposium McGill University, Montreal: Faculty of Religious Studies, McGill University, ISBN 0-7717-0124-1 .
  • Holder, R. Ward (2004), "Calvin's heritage", in McKim, Donald K., The Cambridge Companion to John Calvin, Cambridge: Cambridge University Press, ISBN 978-0-521-01672-8 
  • Gäbler, Ulrich (1986), Huldrych Zwingli: His Life and Work, Philadelphia: Fortress Press, ISBN 0-8006-0761-9 
  • Ganoczy, Alexandre (2004), "Calvin's life", in McKim, Donald K., The Cambridge Companion to John Calvin, Cambridge: Cambridge University Press, ISBN 978-0-521-01672-8 
  • McGrath, Alister E. (1990), A Life of John Calvin, Oxford: Basil Blackwell, ISBN 0-631-16398-0 .
  • Muller, Richard A. (2004). "John Calvin and later Calvinism". In Bagchi, David; Steinmetz, David C. The Cambridge Companion to Reformation Theology. New York: Cambridge University Press. ISBN 978-0521776622. 
  • Parker, T. H. L. (2006), John Calvin: A Biography, Oxford: Lion Hudson plc, ISBN 978-0-7459-5228-4 .
  • Stephens, W. P. (1986), The Theology of Huldrych Zwingli, Oxford: Clarendon Press, ISBN 0-19-826677-4 .
  • Wikisource link to Westminster Confession of Faith. Wikisource. 1646.

Marejeo mengine[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Wakalvini kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.