Maisha ya kiroho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kuungana na Kristo ndiyo lengo la maisha ya Kiroho.


Maisha ya Kiroho katika Ukristo ndiyo maisha ya kuongozwa na Roho Mtakatifu nyuma ya Yesu Kristo kwa utukufu wa Mungu Baba.

Ufuasi huo unafanyika pamoja na waamini wengine katika Kanisa, jumuia ya wanafunzi wa Yesu inayotokana na kundi la kwanza, lililoundwa na Mitume wake.

Mwanzo wake wa kawaida ni ubatizo, uliofananishwa na Yesu mwenyewe na aina ya kuzaliwa upya kwa maji na Roho Mtakatifu.

Uzima huo mpya unalishwa mfululizo na Neno la Mungu na ekaristi.

Lengo ni kufikia muungano na Mungu katika uzima wa milele, lakini huo unaanzia hapa duniani katika ustawi wa maadili makuu ya imani, tumaini na upendo, pamoja na vipaji vya Roho Mtakatifu.

Ni hasa neema kutoka kwa Mwenyezi Mungu, ingawa juhudi za mhusika zinadaiwa vilevile.

Teolojia hiyo ya maisha ya kiroho ya Kikristo inaitwa pia kifupi Teolojia ya Kiroho.

Katika dini tofauti na Ukristo[hariri | hariri chanzo]

Nje ya Ukristo, dini mbalimbali zinazungumzia maisha ya kiroho kama namna ya kuishi kadiri ya roho, si kadiri ya mwili tu.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  • F. VAN VLIJMEN, W.F., Safari ya Kiroho, Mafundisho kwa Watawa (vitabu 2) – ed. T.M.P. Book Department – Tabora 1978
  • R. GARRIGOU-LAGRANGE, O.P., Hatua Tatu za Maisha ya Kiroho, Utangulizi wa Uzima wa Mbinguni – tafsiri fupi ya Rikardo Maria, U.N.W.A. – ed. Ndugu Wadogo wa AfrikaMorogoro 2006

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya dini bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hii kama historia yake au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.