Utukufu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mozaiki ya Kugeuka sura, Monasteri ya Mt. Katerina, Mlima Sinai, Misri.

Utukufu (kwa Kiebrania הוד, hod, na כבד, kabod, "uzito"; kwa Kigiriki δόξα, doxa, "tathmini"; kwa Kiingereza glory kutoka Kilatini gloria, "umaarufu") ni hasa sifa ya Mungu anapojitokeza kwa viumbe.

Katika Biblia na Ukristo utukufu ni muhimu sana, kwa sababu unatazamwa kuwa ndio lengo la uumbaji[1] ili kwa njia hiyo watu waokoke.[2]

Katika Kut 33:20, Musa aliambiwa mtu yeyote hawezi kuona utukufu huo na kuendelea kuishi.

Yesu aliwafundisha wafuasi wake kutenda mema, ili watu wakiona wamtukuze Baba wa mbinguni (Math 5:16).

Kadiri ya Injili Ndugu, Yesu alionekana na wanafunzi watatu akiwa katika utukufu pamoja na Musa na Elia (Lk 9:29-32).

Utukufu utashirikishwa kwa binadamu waadilifu watakapofufuliwa siku ya mwisho

Kinyume cha kulenga utukufu huo kutoka kwa Mungu, mara nyingi watu wanajitafutia sifa kutoka kwa wenzao (Yoh 12:43). Ndiyo dhambi ya majivuno inayozuia imani.[3]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. The Catholic Encyclopedia - Glory
  2. ST, II-II, Q. 132, art. 1.
  3. ST, II-II, Q. 132, art. 4.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Waorthodoksi[hariri | hariri chanzo]

Waprotestanti[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mambo ya dini bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hii kama historia yake au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.