Liturujia ya Vipindi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Breviari binafsi ya malkia wa Uskoti Mary Stuart, aliyokwenda nayo siku ya kuuawa kama alivyohukumiwa na dada yake Elizabeti I wa Uingereza.
Hii ni sehemu ya mfululizo kuhusu
Kanisa Katoliki
Imani

Umoja wa Mungu
Utatu (Baba, Mwana, Roho Mtakatifu)
Umwilisho Maisha ya Yesu
Msalaba Ufufuko Kupaa
Historia ya Wokovu Ufunuo
Biblia Mapokeo Ualimu Dogma
Neema Dhambi Wokovu Sakramenti
Watakatifu Bikira Maria

Muundo

Papa: Fransisko
Urika wa maaskofu Mitaguso mikuu
Kundi la Makardinali
Kanisa la Kilatini
Makanisa Katoliki ya Mashariki

Historia

Historia Ukristo
Ukatoliki Mlolongo wa Kitume
Sifa nne za Kanisa Utetezi Ekumeni
Maisha ya kiroho Amri Kumi Utawa
Sala Falsafa Teolojia
Muziki Sanaa Sayansi

Ibada

Liturujia Mwaka wa Kanisa
Ekaristi Liturujia ya Vipindi

Mapokeo ya liturujia

Liturujia ya Kilatini (Roma Liturujia ya Trento Milano Toledo Braga Lyon Canterbury)
Liturujia ya Armenia Liturujia ya Misri
Liturujia ya Ugiriki Liturujia ya Antiokia
Liturujia ya Mesopotamia

Liturujia ya Vipindi ni sala rasmi ya Kanisa kama inavyoadhimishwa katika madhehebu mbalimbali ya Ukristo, lakini ni jina hasa la mpangilio unaofuatwa na Kanisa la Roma baada ya Mtaguso wa pili wa Vatikano (kwa Kilatini jina ni Liturgia Horarum).

Kwa njia yake wakleri, watawa na waamini wote wa Yesu wa madhehebu hayo wanaungana naye katika sala yake ya kudumu, na wanasaidiwa kuishi kitakatifu saa zote za siku kwa kumkumbuka Mungu mara kwa mara.

Inaitwa hivyo kwa sababu inafanyika kwa vipindi mbalimbali kadiri ya mwendo wa siku (usiku na mchana): muhimu zaidi ni vipindi vya asubuhi (Masifu ya asubuhi) na jioni (Masifu ya jioni), lakini kuna pia vipindi vya usiku kati au alfajiri (Kipindi cha masomo), mchana (Sala ya kabla ya adhuhuri, Sala ya adhuhuri na Sala ya baada ya adhuhuri) na kabla ya kulala (Sala ya mwisho).

Katika Kanisa la Kilatini hiyo sala ya Kanisa inategemea hasa Biblia ya Kikristo kwa kutumia Zaburi na masomo kutoka kwake.

Matini yake yote yamekusanywa pamoja katika kitabu kimoja ambacho kwa sababu hiyo kilizoeleka kuitwa breviari (yaani: "matini kwa ufupi", badala ya kuzagaa katika vitabu mbalimbali kama zamani).

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala[hariri | hariri chanzo]

Matini na sauti[hariri | hariri chanzo]

Miongozo[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Liturujia ya Vipindi kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.