Teresa wa Mtoto Yesu : Tofauti kati ya masahihisho
d r2.6.4) (roboti Ondoa: rw:Mutagatifu Tereza w'Umwana Yezu |
d r2.6.4) (roboti Nyongeza: he:הקדושה תרזה של התינוק ישו המשיח |
||
Mstari 106: | Mstari 106: | ||
[[ga:Naomh Thérèse de Lisieux]] |
[[ga:Naomh Thérèse de Lisieux]] |
||
[[gd:Naomh Thérèse de Lisieux]] |
[[gd:Naomh Thérèse de Lisieux]] |
||
[[he:הקדושה תרזה של התינוק ישו המשיח]] |
|||
[[hr:Sveta Mala Terezija]] |
[[hr:Sveta Mala Terezija]] |
||
[[hu:Lisieux-i Szent Teréz]] |
[[hu:Lisieux-i Szent Teréz]] |
Pitio la 10:34, 13 Aprili 2011
Teresa wa Mtoto Yesu na wa Uso Mtakatifu ni jina la kitawa la Thérèse Françoise Marie Martin, maarufu pia kwa jina la Teresa wa Lisieux, anayeheshimiwa na Kanisa Katoliki kama mtakatifu mwenye sifa za bikira na mwalimu wa Kanisa.
Tangu mwaka 1927 ni msimamizi wa wamisionari wote (pamoja na Fransisko Xavier), na tangu mwaka 1944 wa Ufaransa (pamoja na Yoana wa Arc).
Alizaliwa Alençon tarehe 2 Januari 1873. Wazazi wake walikuwa Louis Martin na Marie-Azélie Guérin, ambao wanaheshimiwa kama wenye heri.
Sikukuu yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe 1 Oktoba.
Maisha
Teresa, mtoto wa tisa na wa mwisho wa Louis Martin na Marie-Azélie Guérin (Zélie), alizaliwa tarehe 2 Januari 1873 kwenye barabara rue Saint-Blaise 42, huko Alençon (Ufaransa).
Walipokuwa vijana wazazi wake walitaka kuingia utawani, wasiweze. Baada ya kuoana, maisha yao yote yaliongozwa na imani na maadili ya Ukristo.
Teresa alipozaliwa, watoto 4 walikuwa wameshafariki.
Teresa alifiwa mama yake alipokuwa na umri wa miaka 4 tu. Hapo mjomba wake, Isidore Guerin, aliteuliwa kuwa mlezi msaidizi wa mabinti watano wa marehemu. Hivyo, tarehe 15 Novemba 1877, Louis Martin alihamia Buissonnets, kitongoji cha Lisieux, awe jirani na shemeji yake mwenye famasia. Huko alijenga uhusiano mkubwa na binamu yake Maria.
Uhusiano wa pekee hasa alikuwa nao kwa dada zake Paulina na Maria, akiwaona kama mama zake.
Mwaka 1882, Paulina alipoingia monasteri ya Wakarmeli ya Lisieux, angetaka kumfuata, lakini hakuweza kutokana na umri wake mdogo. Zaidi tena alitaka kufanya hivyo Maria pia alipoingia monasteri hiyo mwaka 1886.
Usiku wa Noeli iliyofuata, alishinda moja kwa moja huzuni yake iliyomfanya alielie daima. Alielewa anahitaji kumtafuta Mungu zaidi na kujipatia hivyo "Elimu ya upendo.
Alipofikia umri wa miaka 14 Teresa alianza kupigania wito wake dhidi ya upinzani wa watu mbalimbali waliotaka kuahirisha hatua ya kujiunga na utawa. Kwa ajili hiyo alisafiri hadi Roma ili akaombe ruhusa ya Papa Leo XIII, lakini alikataliwa kwa wema, kitu kilichomsikitisha lakini bila ya kumhangaisha, akijua amefanya kila aliloweza ili kuitikia wito wake mapema.
Wakati wa kurudi Ufaransa, askofu wake aliamua kubadili msimamo wake na kumruhusu. Hivyo tarehe 9 Aprili 1888 msichana Teresa alingiia Karmeli, akiwa na miaka 15 tu.
Mwaka 1893 aliteuliwa kuwa mlezi msaidizi wa wanovisi, kazi aliyofanya kwa bidii na ufanisi mkubwa.
Mwaka 1894, baada ya ugonjwa wa muda mrefu, mzee Louis Martin alifariki, na binti yake mwingine, Selina, aliyekuwa anamtunza, aliweza kujiunga na monasteri hiyo. Kamera yake imetuachia picha halisi za Teresa.
Mwezi Aprili 1896, alipatwa na TB, ugonjwa ambao ukaja kumuua baada ya miezi 18. Mateso ya mwili yaliendana na yale ya ndani yanayojulikana kama "usiku wa roho".
Tarehe 10 Julai 1897 udhaifu ulimzuia asiendelee kuandika habari za maisha yake kama alivyoagizwa. Neno la mwisho aliloliandika katika sentensi isiyomalizika ni "upendo".
Alifariki tarehe 30 Septemba, mnamo saa 19:20.
Heshima baada ya kufa
Mara baada ya kufa maandishi yake yalianza kusambaa kwa namna ya ajabu na kumvutia heshima ya wengi. Pia ilipatikana miujiza iliyopatikana kwa maombezi yake.
Mwaka 1925 Papa Pius XI alimtangaza mtakatifu, na mwaka 1997 Papa Yohane Paulo II alimtangaza mwalimu wa Kanisa kutokana na mchango wake mkubwa katika teolojia ya Kiroho alioutoa kupitia maandishi yake, yaliyoenea upesi ajabu duniani kote.
Tafsiri ya Kiswahili na ya Kihaya
THERESIA WA MTOTO YESU, Ua la Upendo, Maisha ya Mtakatifu Theresia wa Mtoto Yesu Aliyoyaandika Yeye Mwenyewe – tafsiri ya J. J. Rwechungura – ed. Paulines Publications Africa – Nairobi 1992 – ISBN 9966-21-021-0 THEREZA OW’OMWANA YEZU – Akamuli k’engonzi, Oburora bw’Omutakatifu Thereza Ow’omwana Yezu Obwo Yayehandikire Wenene – tafsiri ya J. J. Rwechungura – ed. Marianum Press Kisubi – Kisubi 1960
Viungo vya nje
- Maandishi yake yote kwa Kifaransa
- Maandishi juu yake kwa Kifaransa
- Kurasa juu ya Teresa wa Lisieux katika tovuti ya shirika lake
- Tovuti ya Shirika la Wakarmeli
Filamu juu yake
- Beatification de la Bienheureuse soeur Thérèse de l'Enfant-Jésus, ya Michel Coissac (1923)
- La rose efeuillée, ya George Pallu (1926)
- La vie miraculeuse de Thérèse Martin, ya Julien Duvivier (1929)
- Thérèse Martin, ya Maurice de Canonge (1939)
- Procès au Vatican, ya André Haguet (1951)
- Le Vrai visage de Thérèse de Lisieux ya Philippe Agostini (1964)
- Il processo di Santa Teresa del Bambin Gesù, ya Vittorio Cottafavi (1967)
- Thérèse, ya Alain Cavalier, (1986), "Prix du Jury" kwenye festival de Cannes.
- Vous m'appellerez petite Thérèse, ya Anne Foumier (1998)
- Thérèse - The Story of Saint Thérèse, ya Leonardo Defilippis (2003)
Picha zake
-
Thérèse Martin alipokuwa na umri wa miaka 13 (Februari 1886)
-
Teresa ni wa pili kushoto wakati wa kufua kwenye udobi wa monasteri ya Lisieux (1894)
-
Teresa wa Lisieux akiigiza kama Yoana wa Arc (1895)
-
Adolphe Roulland, mmoja wa mafrateri wawili ambao Teresa alikabidhiwa kuwaombea
Makala hii bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake? Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari. |