Kroatia
Kroatia Republika Hrvatska | |
---|---|
Kaulimbiu: "Lijepa naša domovino" (Kikroatia kwa "Nchi Yetu Nzuri") | |
Wimbo wa taifa: "Lijepa naša domovino" | |
Mji mkuu na mkubwa | Zagreb |
Lugha rasmi | Kikroatia |
Kabila (2021) | 91.6% Wakroatia 4.4% Waserbia 4% wengine |
Serikali | Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kikatiba |
• Rais | Zoran Milanović |
• Waziri Mkuu | Andrej Plenković |
Historia | |
• Kujitenga na Yugoslavia | 25 Juni 1991 |
• Kutambuliwa kimataifa | 15 Januari 1992 |
• Katiba ya sasa | 22 Desemba 1990 |
Eneo | |
• Jumla | km2 56,594 (ya 124) |
• Maji (asilimia) | 1.09% |
Idadi ya watu | |
• Kadirio la 2021 | 3,855,641 |
• Msongamano | 68.3/km2 |
PLT (PPP) | Kadirio la 2024 |
• Jumla | ▲ $174.8 B [1] (ya 78) |
• Kwa kila mtu | ▲ $45,290 [1](ya ) |
PLT (Kawaida) | Kadirio la 2024 |
• Jumla | ▲ $83.2 B [1] |
• Kwa kila mtu | ▲ $21,570 [1] |
HDI (2022) | ▲ 0.858 |
Sarafu | Euro (€) EUR |
Majira ya saa | UTC+1 |
Upande wa magari | Kulia |
Msimbo wa simu | +385 |
Jina la kikoa | .hr |

Kroatia pia korasia (kwa Kikroatia: Hrvatska), rasmi Jamhuri ya Kroatia, ni nchi iliyoko katika Ulaya ya Kati na Kusini-Mashariki, ikipakana na Bahari ya Adriatic upande wa magharibi. Inapakana na Slovenia upande wa kaskazini-magharibi, Hungaria upande wa kaskazini, Serbia upande wa kaskazini-mashariki, Bosnia na Herzegovina upande wa mashariki, na Montenegro upande wa kusini-mashariki. Mji wake mkuu na mkubwa zaidi ni Zagreb. Kroatia ina eneo la 56,594 km² na idadi ya watu inayokadiriwa kuwa 3.8 milioni.
Kroatia ilikuwa kati ya majimbo ya Yugoslavia na ilipata uhuru wake mwaka 1991.
Imejiunga na Umoja wa Ulaya tarehe 1 Julai 2013.
Historia
[hariri | hariri chanzo]Maeneo ya Kroatia yalikuwa sehemu ya Illyria wakati wa Dola la Roma na kutawaliwa kama mikoa ya dola hilo.
Mnamo mwaka 395 Dola la Roma liligawiwa katika sehemu ya magharibi na sehemu ya mashariki. Sehemu hizo mbili ziliendela baadaye kwa namna mbili tofauti.
Kuanzia mwaka 600 makabila ya Waslavoni walianza kuingia na kukaa. Wakroatia waliunda utemi wao wa kwanza. Kroatia ilikuwa upande wa magharibi wa mstari wa mwaka 395, hivyo chini ya athira ya Kanisa Katoliki, ikaendelea kuwa sehemu ya utamaduni wa Ulaya ya magharibi. Kumbe Waslavoni wa jirani wanaotumia lugha ileile waliishi chini ya athira ya Bizanti na Kanisa la Kiorthodoksi, hivyo kuendelea kama sehemu ya Ulaya ya Mashariki na kuitwa Waserbia.
Mtemi Tomislav (910–928) alichukua cheo cha mfalme mwaka 925. Huo Ufalme wa Kroatia uliendelea hadi mwaka 1102. Wakati ule mfalme wa mwisho hakuwa tena wa watoto na mfalme wa Hungaria alichaguliwa kuwa mfalme wa Kroatia pia. Maungano hayo na Hungaria yaliendelea kwa karne nyingi.
Tangu maungano wa Hungaria na Austria ni Kaisari wa Austria aliyekuwa na cheo cha mfalme wa Krotia hadi vita kuu ya kwanza ya dunia (1914-1918).
Mwaka 1918 Dola la Austria liliporomoka. Waslavoni wa Kusini waliamua kuunda ufalme wa pamoja kwa jina la Yugoslavia. Kroatia ilikuwa sehemu ya Yugoslavia kuanzia 1918; kwanza katika ufalme wa Yugoslavia, halafu katika jamhuri ya kisoshalisti ya Yugoslavia hadi 1991.
Miaka 1990 / 1991 Yugoslavia iliporomoka na majimbo yake zilitafuta uhuru kama nchi za kujitegemea.
Demografia
[hariri | hariri chanzo]Kulingana na sensa ya mwaka 2021, Kroatia ilikuwa na idadi ya watu 3,855,641, ikiwa ni upungufu mkubwa kutoka watu 4,284,889 waliorekodiwa kwenye sensa ya 2011. Kupungua huku kunahusishwa na viwango vya chini vya kuzaliwa, uhamiaji wa watu kwenda nje ya nchi, na mabadiliko ya kijamii na kiuchumi.
Muundo wa Idadi ya Watu
[hariri | hariri chanzo]- Wakroatia ndio kundi kubwa zaidi la kikabila, wakiwa 91.6% ya idadi ya watu.
- Waserbia ni kundi kubwa la wachache, wakiwa 4.4% ya idadi ya watu.
Makundi mengine madogo ni pamoja na Wabosnia, Waitalia, Wamongolia, Waslovakia, Waroma, na Wajerumani, ambao kwa pamoja hufanya takriban 4% ya idadi ya watu.
Lugha
[hariri | hariri chanzo]Kikroatia ni lugha rasmi ya nchi, inayozungumzwa na takriban 95.6% ya wakazi. Lugha za wachache zinatambulika kisheria katika maeneo yenye jamii kubwa za watu wa kabila fulani, kama Kiserbia, Kihungaria, Kiitaliano, na Kislovakia.
Dini
[hariri | hariri chanzo]Ukristo], hasa Ukatoliki wa Kikatoliki ndio dini kubwa, ikiwa takriban 78.97% ya wakazi.
- Waorthodoksi wa Kiserbia wanajumuisha 3.32% ya idadi ya watu.
- Waislamu ni takriban 1.32%, wengi wao wakiwa Wabosnia na Waalbania.
- Takriban 4.71% ya wakazi hawana dini au hawajitambulishi na dini yoyote.
Muundo wa Umri
[hariri | hariri chanzo]Umri wa wastani wa raia wa Kroatia ni 44.3 miaka, ukiashiria mwelekeo wa taifa lenye idadi kubwa ya watu wazee.Asilimia 21.8% ya wakazi wana umri wa zaidi ya miaka 65.Idadi ya vijana chini ya miaka 14 ni 14.7% ya wakazi wote.
Uhamiaji
[hariri | hariri chanzo]Kroatia imekumbwa na uhamiaji wa watu kwenda nchi nyingine za Ulaya, hasa baada ya kujiunga na Umoja wa Ulaya mwaka 2013. Mataifa mengi ya Magharibi, kama Ujerumani, Austria, na Ireland, yamekuwa maeneo maarufu ya uhamiaji kwa vijana wa Kikroatia wanaotafuta kazi na maisha bora.
Tazama pia
[hariri | hariri chanzo]
Nchi za Umoja wa Ulaya | ![]() |
---|---|
Austria | Bulgaria | Eire | Estonia | Hispania | Hungaria | Italia | Kroatia | Kupro | Latvia | Lituanya | Luxemburg | Malta | Polandi | Slovakia | Slovenia | Romania | Ubelgiji | Ucheki | Udeni | Ufaransa | Ufini | Ugiriki | Uholanzi | Ujerumani | Ureno | Uswidi |
![]() |
Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Kroatia kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
- ↑ 1.0 1.1 1.2 1.3 "Croatia GDP". 2024.