Mtume Andrea

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mtakatifu Andrea, mtume, mchoro wa Yoan wa Gabrovo, karne ya 19.
Kifodini cha Mtume Andrea msalabani
Mitume wa Yesu
Mfululizo wa kurasa juu ya Yesu
Jesus
Yesu Kristo na Ukristo

Umwilisho  • Utoto wa Yesu  • Ubatizo
Arusi ya Kana • Utume wa Yesu • Mifano ya Yesu  • Miujiza ya Yesu
Kugeuka sura • Karamu ya mwisho • Msalaba wa Yesu  • Maneno saba
Kifo cha Yesu  • Ufufuko wa Yesu
Kupaa mbinguni  • Ujio wa pili
Injili  • Majina ya Yesu katika Agano Jipya  • Yesu kadiri ya historia  • Tarehe za maisha ya Yesu • Kristolojia

Mazingira ya Yesu

Wayahudi • Kiaramu • Bikira Maria • Yosefu (mume wa Maria) • Familia takatifu • Ukoo wa Yesu • Ndugu wa Yesu • Yohane Mbatizaji

Mitazamo juu ya Yesu

Mitazamo katika Agano Jipya · Mitazamo ya Kikristo • Mitazamo ya Kiyahudi • Mitazamo ya Kiislamu • Yesu katika sanaa

Mtume Andrea alikuwa Myahudi wa karne ya 1, mmoja kati ya wawili wa kwanza kati ya Mitume wa Yesu.

Anaheshimiwa na Wakristo wote kama mtakatifu, hasa tarehe 30 Novemba iliyo sikukuu yake[1].

Ni msimamizi wa Uskoti, Russia, Ugiriki, Romania, Malta, Prussia, na wa mabaharia, wavuvi, na waimbaji.

Asili na jina[hariri | hariri chanzo]

Inakadiriwa alizaliwa mwaka 6 K.K. huko Bethsaida akauawa 60 hivi huko Patrasso (Ugiriki).

Jina lake asili la Kiyahudi halijulikani. Kwa Kigiriki aliitwa Ανδρέας (Andreas, maana yake Mwanamume, Rijali). Anaitwa pia Protocletos yaani Wa kwanza kuitwa (na Yesu Kristo).

Agano Jipya linasema Andrea alikuwa ndugu wa Mtume Petro, mwana wa Yona au Yohana (Math 16:17; Yoh 1:42).

Wito wake[hariri | hariri chanzo]

Kuitwa kwa mtume Petro na Andrea, mchoro wa Caravaggio.

Wote wawili walihamia Kafarnaumu ili kufanya kazi ya uvuvi, na ndipo walipoitwa na Yesu kuwa "wavuvi wa watu" (ἁλιείς ἀνθρώπων, halieis anthropon).

Injili ya Yohane inaarifu kuwa Andrea aliwahi kuwa mwanafunzi wa Yohane Mbatizaji, mpaka nabii huyo alipomuelekeza amfuate Yesu Kristo, "Mwanakondoo wa Mungu" atakayekamilisha kazi yake mwenyewe (Yoh 1:35-40). Andrea akiwa wa kwanza kumtambua Yesu kuwa Masiya, alimtambulisha kwa ndugu yake (Yoh 1:41).

Ni baada ya hapo kwamba waliitwa kuacha yote wamfuate Yesu (Mk 1:17-18; Math 4:19-20; Lk 5:11).

Baada ya ufufuko wa Yesu[hariri | hariri chanzo]

Katika Injili Andrea anatajwa mara kadhaa kuwa karibu sana na Yesu (Mk 13:3; Yoh 6:8, 12:22), lakini katika Matendo ya Mitume anatajwa mara moja tu, katika orodha ya Mitume (1:13).

Mwanahistoria Eusebius wa Kaisarea anataja Asia Ndogo, Scizia, pwani ya Bahari Nyeusi na mto Volga hadi Kiev kuwa mahali pa utume wake baada ya ufufuko wa Yesu.

Mapokeo yanadai alisulubiwa huko Patrasso juu ya msalaba wenye umbo la X uliopewa jina lake.

Apokrifa za Andrea[hariri | hariri chanzo]

Kati ya vitabu vilivyokataliwa na Kanisa (Decretum Gelasianum ya Papa Gelasio I) kuna Injili ya Andrea na Matendo ya Andrea vilivyoandikwa karne ya 3.

Picha[hariri | hariri chanzo]

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Kwa Kiswahili[hariri | hariri chanzo]

  • Thenashara, Mitume Kumi na Wawili – tafsiri ya P. A. Bunju – Toleo la pili – ed. Benedictine Publications Ndanda Peramiho – Ndanda 1984 – ISBN 9976-63-030-1

Kwa lugha nyingine[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mtume Andrea kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.