Yakobo Mdogo

Mitume wa Yesu |
---|
|
Yakobo Mdogo ni jina la mmojawapo kati ya Mitume wa Yesu. Anaitwa hivyo ili kumtofautisha na mtume mwenzake, Yakobo wa Zebedayo.
Katika Injili anaitwa Yakobo wa Alfayo na kutajwa na Injili ya Mathayo 10:3, Injili ya Marko 3:18, Injili ya Luka 6:15, mbali ya Matendo ya Mitume 1:13.
Kutokana na wingi wa Wayahudi waliotumia jina hilo la babu wa taifa la Israeli, ni vigumu kuelewa kama ndiye Yakobo anayetajwa kama mmoja kati ya nguzo za Kanisa la Yerusalemu aliyekubali pendekezo la Mtume Petro kuhusu suala la tohara kwa wasio Wayahudi wanaoongokea Ukristo na hasa kama ndiye mwandishi wa Waraka wa Yakobo [1].
Kama ndiye, aliuawa Yerusalemu mwaka 62 kwa himizo la kuhani mkuu Anna II.
Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 3 Mei pamoja na Mtume Filipo [2][3].
Tazama pia
[hariri | hariri chanzo]- Watakatifu wa Agano la Kale
- Orodha ya Watakatifu Wakristo
- Orodha ya Watakatifu wa Afrika
- Orodha ya Watakatifu Wafransisko
Tanbihi
[hariri | hariri chanzo]- ↑ https://www.santiebeati.it/dettaglio/21000
- ↑ Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107
- ↑ https://www.santiebeati.it/dettaglio/94044
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- Thenashara, Mitume Kumi na Wawili – tafsiri ya P. A. Bunju – Toleo la pili – ed. Benedictine Publications Ndanda Peramiho – Ndanda 1984 – ISBN 9976-63-030-1
Viungo vya nje
[hariri | hariri chanzo]- Catholic Forum Patron Saints Index: James the Lesser Ilihifadhiwa 25 Juni 2007 kwenye Wayback Machine.
![]() |
Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Yakobo Mdogo kama habari za maisha au kazi yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |