Mtume Bartolomayo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kifodini cha Mtume Bartholomayo kilivyochorwa na José de Ribera.
Mitume wa Yesu
Mfululizo wa kurasa juu ya Yesu
Jesus
Yesu Kristo na Ukristo

Umwilisho  • Utoto wa Yesu  • Ubatizo
Arusi ya Kana • Utume wa Yesu • Mifano ya Yesu  • Miujiza ya Yesu
Kugeuka sura • Karamu ya mwisho • Msalaba wa Yesu  • Maneno saba
Kifo cha Yesu  • Ufufuko wa Yesu
Kupaa mbinguni  • Ujio wa pili
Injili  • Majina ya Yesu katika Agano Jipya  • Yesu kadiri ya historia  • Tarehe za maisha ya Yesu • Kristolojia

Mazingira ya Yesu

Wayahudi • Kiaramu • Bikira Maria • Yosefu (mume wa Maria) • Familia takatifu • Ukoo wa Yesu • Ndugu wa Yesu • Yohane Mbatizaji

Mitazamo juu ya Yesu

Mitazamo katika Agano Jipya · Mitazamo ya Kikristo • Mitazamo ya Kiyahudi • Mitazamo ya Kiislamu • Yesu katika sanaa

Bartolomayo (kwa Kigiriki Βαρθολομαιος) alikuwa Myahudi wa karne ya 1, mmojawapo kati ya Mitume wa Yesu kadiri ya Injili Ndugu.

Wengi wanaona hilo ni ubini wake (kwa Kiaramu lina maana ya "mwana wa Tolomayo"), kumbe jina lake mwenyewe ni "Natanaeli", kama anavyotajwa na Injili ya Yohane 1:45, rafiki wa Mtume Filipo. Kama ni hivi, alikuwa mwenyeji wa Kana ya Galilaya, na unyofu wake ulisifiwa na Yesu.

Anaheshimiwa na madhehebu karibu yote ya Ukristo kama mtakatifu, hasa tarehe 24 Agosti[1].

Maisha[hariri | hariri chanzo]

Yote tunayoyajua kwa hakika juu yake yanategemea Injili na Matendo ya Mitume anapotajwa tu katika orodha ya Thenashara ambao waliteuliwa na Yesu Kristo kama mwanzo mpya wa taifa la Mungu wakatumwa naye kuhubiri na kuponya.

Baada ya ufufuko wa Yesu na Pentekoste, hakuna habari za hakika, ila kuna masimulizi ya utume wake Mashariki ya Kati hadi India.

Alifia dini ya Ukristo katika nusu ya pili ya karne I labda Syria au Armenia.

Picha[hariri | hariri chanzo]

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Kwa Kiswahili[hariri | hariri chanzo]

  • Thenashara, Mitume Kumi na Wawili – tafsiri ya P. A. Bunju – Toleo la pili – ed. Benedictine Publications Ndanda Peramiho – Ndanda 1984 – ISBN 9976-63-030-1

Kwa lugha nyingine[hariri | hariri chanzo]

  • Easton's Bible Dictionary, 1897.
  • Encyclopedia Anglicana, 1911
  • Dictionary of First Names, Patrick Hanks and Flavia Hodges. Oxford University Press, 1996
  • Attwater, Donald and Catherine Rachel John. The Penguin Dictionary of Saints. 3rd edition. New York: Penguin Books, 1993. ISBN 0-14-051312-4.
  • The Apostles In India by Fr A.C Perumalil SJ 1952
  • For a discussion of Baroque paintings of St. Bartholomew by the Spanish artist Ribera, see: Williamson, Mark A. "The Martyrdom Paintings of Jusepe de Ribera: Catharsis and Transformation", PhD Dissertation, Binghamton University, Binghamton, New York 2000 (available online at myspace.com/markwilliamson13732)

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mtume Bartolomayo kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.