Galilaya
Mandhari
Galilaya (kutoka Kiebrania הגליל (ha-galil), yaani "mzunguko" au "mkoa"; kiasili "galil ha-goyim - mkoa wa Wapagani") ni mkoa maarufu kihistoria upande wa kaskazini wa Israeli au Palestina.
Upande wa mashariki mpaka wake ni mto Yordani, ambao sehemu hiyo unaunda ziwa Genesareti (pia: bahari ya Galilaya).
Waisraeli walipohama Misri wakati wa Musa na kuteka nchi ya Kanaani chini ya Yoshua, katika mkoa huo walihamia watu wa makabila ya Dan, Zebuluni, Isakari na Naftali.
Galilaya ndio mkoa ambapo alikulia na kuanza utume wake Yesu, mwanzilishi wa Ukristo.
Kati ya miji na vijiji vya Galilaya vilivyotajwa katika Injili kuna:
| Makala hii kuhusu maeneo ya Asia bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Galilaya kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |